Joel kaigarula
Member
- Jun 3, 2014
- 28
- 16
[h=3][/h]
Hapo jana kampuni ya Samsung imezindua simu ya kwanza duniani inayotumia mfumo wa uendeshaji wa Tizen badala ya Android kama ilivyozoeleka. Samsung Z yenye uwezo unaolingana na simu ya Galaxy S5, ikiwa na vitu kama fingerprint scanner na vinginevyo, inatarajiwa kuingia sokoni baadae mwaka huu.
Lakini wakati Samsung ndio mtengenezaji mkubwa wa simu zinazotumia mfumo wa Android duniani, kampuni ya Google ndiyo inayomiliki mfumo huo. Na hivyo inalazimu watengenezaji wa simu kama Samsung, HTC na wengineo kujumuisha apps kama vile Gmail, na Google+ kwenye simu zao kama moja ya masharti ya mkataba wa matumizi ya mfumo huu kutoka Google.
Kuhama huku kwa Samsung kunaweza kufanya mfumo wa Android kuwa matatani. Kwa sasa Samsung ndio kampuni inayoongoza kwa uuzaji wa simu za mkononi. Mauzo ya Samsung kwa mwanzo wa mwaka huu ni makubwa kuliko jumla ya mauzo ya simu ya washindani wake wanaofuatia; Apple, Huawei, Lenovo na LG. Hapo hapo Samsung inashikilia asilimia 65 ya simu zote zenye mfumo wa Android. Endapo Samsung itahama ghafla, na Tizen itakuwa na mafanikio sokoni, itasababisha Android kushuka thamani. Kampuni ya Google inayoendesha Android yenyewe haitengenezi simu, na hata kwa sasa Android haiingizi mapato makubwa kwa Google. Kuondoka kwa mtumiaji mkubwa wa Android kutafanya Android kuwa mradi wenye hasara zaidi kuliko sasa kwani Google itajikuta inamiliki mfumo ambao una soko dogo sana.
Vile vile kitu kingine kinachotishia uhai wa Android ni kuwa ingawa Tizen ni huru (open source) kama ilivyo Android, Tizen haina utata wa hataza zake (patents). Android inakabiliwa na mashtaka makubwa juu ya baadhi ya vipengele vyake kudaiwa kuingilia hataza za makampuni kama Apple na Oracle. Hivyo watengenezaji waliobakia kama HTC, Huawei na wengineo wanaotumia Android sasa, hawatasita kuhama kambi kwenda Tizen ambako hawatakuwa na wasiwasi wa kushitakiwa kama ilivyoshitakiwa Samsung hapo nyuma kuhusu matumizi ya Android.
Jambo lililo wazi ni kuwa Tizen itachukua muda kukubalika. Mtumiaji wa kawaida huhama mfumo baada ya kuridhika na uwapo wa uchaguzi mpana wa programu (apps). Mpaka pale soko la apps la Tizen (ambalo bado halijaanza) litakapokuwa na apps mbadala wa zile zinazopatikana soko la Google, Google Play, na soko la apps za iPhone, App Store, ndipo Tizen inatarajiwa kutoa ushindani mkubwa katika soko la mifumo ya simu.
source: bofyatz.com
samsung Z. chanzo: samsung
Lakini wakati Samsung ndio mtengenezaji mkubwa wa simu zinazotumia mfumo wa Android duniani, kampuni ya Google ndiyo inayomiliki mfumo huo. Na hivyo inalazimu watengenezaji wa simu kama Samsung, HTC na wengineo kujumuisha apps kama vile Gmail, na Google+ kwenye simu zao kama moja ya masharti ya mkataba wa matumizi ya mfumo huu kutoka Google.
Kuhama huku kwa Samsung kunaweza kufanya mfumo wa Android kuwa matatani. Kwa sasa Samsung ndio kampuni inayoongoza kwa uuzaji wa simu za mkononi. Mauzo ya Samsung kwa mwanzo wa mwaka huu ni makubwa kuliko jumla ya mauzo ya simu ya washindani wake wanaofuatia; Apple, Huawei, Lenovo na LG. Hapo hapo Samsung inashikilia asilimia 65 ya simu zote zenye mfumo wa Android. Endapo Samsung itahama ghafla, na Tizen itakuwa na mafanikio sokoni, itasababisha Android kushuka thamani. Kampuni ya Google inayoendesha Android yenyewe haitengenezi simu, na hata kwa sasa Android haiingizi mapato makubwa kwa Google. Kuondoka kwa mtumiaji mkubwa wa Android kutafanya Android kuwa mradi wenye hasara zaidi kuliko sasa kwani Google itajikuta inamiliki mfumo ambao una soko dogo sana.
Vile vile kitu kingine kinachotishia uhai wa Android ni kuwa ingawa Tizen ni huru (open source) kama ilivyo Android, Tizen haina utata wa hataza zake (patents). Android inakabiliwa na mashtaka makubwa juu ya baadhi ya vipengele vyake kudaiwa kuingilia hataza za makampuni kama Apple na Oracle. Hivyo watengenezaji waliobakia kama HTC, Huawei na wengineo wanaotumia Android sasa, hawatasita kuhama kambi kwenda Tizen ambako hawatakuwa na wasiwasi wa kushitakiwa kama ilivyoshitakiwa Samsung hapo nyuma kuhusu matumizi ya Android.
Jambo lililo wazi ni kuwa Tizen itachukua muda kukubalika. Mtumiaji wa kawaida huhama mfumo baada ya kuridhika na uwapo wa uchaguzi mpana wa programu (apps). Mpaka pale soko la apps la Tizen (ambalo bado halijaanza) litakapokuwa na apps mbadala wa zile zinazopatikana soko la Google, Google Play, na soko la apps za iPhone, App Store, ndipo Tizen inatarajiwa kutoa ushindani mkubwa katika soko la mifumo ya simu.
source: bofyatz.com