racka98
JF-Expert Member
- Jul 7, 2020
- 1,042
- 1,547
Contactless payment. Unalipia vitu pale checkout kwa kugusisha simu yako kwenye ile machine kma unavyogusisha card ya bank. Hii ni kma una payment app inayosupport hcho kitu kma Google Pay na Samsung pay (hii kitu bado haijawa adopted kwenye nchi yetu).Hvi hii kazi ya NFC ni nini hasa??
Inaweza tumika kunlock magari. Baadala ya kuwa na funguo au remote unatumia simu yako unagusisha kwenye kitasa cha mlango gari linafunguka. Hii keyless entry kwa sasa iko supported Tesla, Honda na Hyundai newer models.
Inaweza tumika kusoma NFC tags ambazo zinakua zina store information kma contacts, web address, commands ambazo ukigusisha simu inawasha hotspot, inafungua app flani, au inakuonesha location flani, n.k
Inatumika pia kuconnect headphones na earphones za bluetooth. Kwa mfano kuna headphones za Sony ambazo ukitaka kupair kwa haraka unagusisha simu na heaphone yenyewe ina pair na kuconnect kabisa. Sio mpk uanze kusearch kwenye bluetooth settings ili kupair heaphone zako.
Inatumika kushare mafile madogo kutoka simu moja kwenda nyingine. Unashare contact alaf unagusisha simu yako na simu nyingine kisha inatuma hilo file. Hii pia inatumika kma kwenye headphones hapo juu. Una pair simu mbili bila kwenda kuhangaika kuitafta kwenye bluetooth settings.
Hivi ni baadhi ya vitu ambavyo NFC kwenye simu zinafanyia kazi.
Kama simu yako ina NFC unaweza kutest information zilizopo kwenye card yako ya bank. Nenda playstore na download app ya NFC Reader (NFC Reader - Apps on Google Play). Ifungue na uwashe NFC kisha gusisha hyo card nyuma ya simu yako utaona kuna number zipo stored kwenye yako ambazo zinatumika kwenye contactless payment. Card yako lazima iwe ya contactless payment na inakua na kialama flani hvi kma hapo kwenye picha. NMB na CRDB wanatoa card za aina hii sikuhz. Nadhan na bank zingine nazo wanatoa.
Simu inaweza kua NFC reader na transmitter lakini card hyo inakua ni transmitter tu.
Sent from my Pixel 3a using JamiiForums mobile app
