Na hakuna wengine Zaidi Ya CCM, watanzania wenzangu iambieni CCM basi imetosha.
Tunatamani kuziona na sisi Air Tanzania zikiruka kama zilivo ndege za Ethiopia, Rwanda na Kenya.
Jaman tunatamani kuiona TTCL ya Tanzania iking'aa zaidi ya Vodacom, Tigo na Airtel.
Jaman watanzania wenzangu mbona hatuipendi nchi yetu hivi? Au ninyi mnaoishabikia CCM ni wa Burundi?
Tunahtaji kuiona reli ya Kati na Tazara zikibeba watu kila siku na mizigo kupunguza malori barabarani, Watanzania tusife tena kwa ajali za barabarani.
Watanzania wenzangu CCM imewaloga na nini?
Mnahtaji Maombi?
Au mnaitaji kupelekwa kwa mganga ili ilo limbwata litoke?
Semeni basi tuwasaidie kabla ya October 25, tunahtaji Mabadiliko jaman, Tunahtaji nchi Mpya, tunahtaji watu watakaoiondoa nchi hapa ilipokwamia.
Natamani kusikia Mutex, Mwatex ikifanya kazi, watu wakibadilishana shift Usiku na mchana kuingia kazini. Natamani, natamani.
Natamani kuona Twiga hawapandi ndege mimi. Nataman kuona UMEME haukatiki siku 365 za mwaka, natamani.
Watanzania wenzangu tamanini basi kama mimi.
Uwezi panga nyumba moja baba mwenye nyumba anakusumbua unakomaa tu eti nikihama huko pia mwenye nyumba atakuwa kama huyu, mmh si kweli hama, watu hawafanani.
Hata CHADEMA na CCM havifanani. Ikomboe Tanzania. Lete kura yako UKAWA, wakishindwa miaka Mitano kuonesha njia, tuwawatoa kwani TATIZO LIPO WAPI?
Tanzania sio ya CCM, Tanzania sio ya CHADEMA, Tanzania sio ya CUF, Tanzania ni nyumbani kwangu mimi na wewe.
IPENDE TANZANIA WEWE MTANZANIA, HII NI NYUMBA YAKO, NI NYUMBA YA WANAO, NA VIZAZI VYAKO VYOTE VITAIJIVUNIA nyumbani TANZANIA milele
MABADILIKO NI SASA CHUKUA HATUA.