Salam zenu Tigo

Salam zenu Tigo

bnhai

JF-Expert Member
Joined
Jul 12, 2009
Posts
2,846
Reaction score
2,401
Jana nilifika Tigoo baada ya line yangu kushindwa kusoma network. Hii ilitokea ghafla tu nilipoamka.
Haya kituko chake.

1. Unatakiwa kutoa photocopy kitambulisho chako kwa shs 300. Hapa nikajiuliza uhalali wa wao kupandisha hiyo bei na kuwa mia tatu na kutofautiana kabisa na maduka mengine. Hii nii Tigo Mlimani City. Nikauliza nyie ni tigo au wakala? Wakasema ni Tigo. Lakini ishu hasa mteja anayekuja kusajili line yake aidha imeharibika au anakuwa mteja kwa mara ya kwanza kampuni kama Tigo ina chaji shs 300. Hii ni aibu kubwa saana. Hata kama makusudio ni kuongeza mapato, mteja huyu atanunua vocha na atatumia huduma nyingine kama Tigo pesa, halafu mnadai shs 300. Hizi nii aibu kwa kweli, lazima awepo mtu mmoja aliyefanya uamuzi wa kufanya bei iwe ya ajabu halafu pia mteja adaiwe.

2. Mteja amekwenda ku-renew line anadaiwa shs 500. Hili ni debatable. Lakini kwa nini msijitahidi line zikawa bure kwa wale wanao renew na hizo mia tano kwa mpya? Nazungumza hivi nadhani huenda shs 500 imeweka kudiscourage wale wanaotaka kuwa na line nyingi bila sababu.

3. Nimemaliza kurenew, naambiwa line yako itafanya kazi baada ya masaa 72 kwa kuwa wewe ni post paid. What? Unaadhibiwa kwa kuwa PostPaid. Nikawaambia nitoeni haraka saana. Oh inabidi uandike barua ya kujitoa. Hii haikuwepo kwenye terms and conditions. Nyie Tigo?

4. Kuna foleni ya ajabu kwa huduma ndogo kwenye duka lao Mlimani City. haivumiliki kwa kweli. Sisi ni wateja bwana lazima tuthaminiwe.
Mwishoni nikatoka nje nikaanza transition ya kuhama mtandao, salam kwenu Tigo toka enzi za Mobitel, naondoka.

Kwaherini.
 
5. ukiwa unatumia micro sim card(sim card ndogo zaidi ya zile wanazouza wenyewe) utaambiwa kukata hiyo line tsh 3000... yani hawa watu wanavimiradi ndani ya mradi wao wa kuuza line, siku ntawaomba lisit kwa kila sh wanazodai
 
kuna watu sijui ndo mateam leader wao pale ubungo millenium business park wanakaa tu kupiga story toka asubuhi mpaka jioni...lakini mwishowe hela zinaingia...

4G internet yao imejaa uongo tu yaani upo chini ya mnara kabisaa but network zero ha ha ha ha mkowapi voda egeee
 
Nilichokigundua toka tigo nikuwa wao kama wao hawana maduka ila watu wanapewa uwakala ili watoe huduma za tigo,mikoa yote ndio hivyo hivyo mpk tigo pesa ipo mikononi mwa watu ambao ni wezi balaa.hv vi super dealer sijui vinaitwa vinawapiga hela Sana mawakala....mfano ile style ya kumpigia simu Wakala na kumwanbia ingiza namba furani na furani then salio linatoweka mtu wa mtaani hawezi kujua hizo mbinu.ni hao hao ma super dealer wao.
 
Magufuli. Amulike na haya makampuni ya simu. Kuna ufisadi wa kutisha.
 
Niliomba line ya tigo pesa sasa ni mwaka, hawana maelezo
 
Ufanyaji kazi wa walio wengi unaupata Tigo. Tigo wanafanya kazi kama Halmashauri kabla ya Magufuli. Unamuuliza mtu juu ya huduma fulani anakwambia hajui na hata hakushauri ufanye nini. Hivi hawa wanalipa kodi inayotakiwa kweli.
 
kuna watu sijui ndo mateam leader wao pale ubungo millenium business park wanakaa tu kupiga story toka asubuhi mpaka jioni...lakini mwishowe hela zinaingia...

4G internet yao imejaa uongo tu yaani upo chini ya mnara kabisaa but network zero ha ha ha ha mkowapi voda egeee

Pole sana ndugu kwa usumbufu ulioupata. Ila pale Shekilango ni ofisi ya mauzo. Huduma kwa wateja inatolewa tu kwa baadhi ya huduma, huduma zingine unatakiwa uende ofisi za huduma kwa wateja kama Manzese, Mliman City na ofisi zingine kama hizo.

Karibu tena na tuendelee kuwa pamoja kwenye mtandao wenye kasi zaidi wa tigo 4G
 
Pole sana ndugu kwa usumbufu ulioupata. Ila pale Shekilango ni ofisi ya mauzo. Huduma kwa wateja inatolewa tu kwa baadhi ya huduma, huduma zingine unatakiwa uende ofisi za huduma kwa wateja kama Manzese, Mliman City na ofisi zingine kama hizo.

Karibu tena na tuendelee kuwa pamoja kwenye mtandao wenye kasi zaidi wa tigo 4G

Sasa Hapo umejibu nini? Jibu Tuhuma za msingi wewe acha kukurupuka, umesoma alichosema muanzisha uzi?

Jana nilifika Tigoo baada ya line yangu kushindwa kusoma network. Hii ilitokea ghafla tu nilipoamka.
Haya kituko chake.

1. Unatakiwa kutoa photocopy kitambulisho chako kwa shs 300. Hapa nikajiuliza uhalali wa wao kupandisha hiyo bei na kuwa mia tatu na kutofautiana kabisa na maduka mengine. Hii nii Tigo Mlimani City. Nikauliza nyie ni tigo au wakala? Wakasema ni Tigo. Lakini ishu hasa mteja anayekuja kusajili line yake aidha imeharibika au anakuwa mteja kwa mara ya kwanza kampuni kama Tigo ina chaji shs 300. Hii ni aibu kubwa saana. Hata kama makusudio ni kuongeza mapato, mteja huyu atanunua vocha na atatumia huduma nyingine kama Tigo pesa, halafu mnadai shs 300. Hizi nii aibu kwa kweli, lazima awepo mtu mmoja aliyefanya uamuzi wa kufanya bei iwe ya ajabu halafu pia mteja adaiwe.

2. Mteja amekwenda ku-renew line anadaiwa shs 500. Hili ni debatable. Lakini kwa nini msijitahidi line zikawa bure kwa wale wanao renew na hizo mia tano kwa mpya? Nazungumza hivi nadhani huenda shs 500 imeweka kudiscourage wale wanaotaka kuwa na line nyingi bila sababu.

3. Nimemaliza kurenew, naambiwa line yako itafanya kazi baada ya masaa 72 kwa kuwa wewe ni post paid. What? Unaadhibiwa kwa kuwa PostPaid. Nikawaambia nitoeni haraka saana. Oh inabidi uandike barua ya kujitoa. Hii haikuwepo kwenye terms and conditions. Nyie Tigo?

4. Kuna foleni ya ajabu kwa huduma ndogo kwenye duka lao Mlimani City. haivumiliki kwa kweli. Sisi ni wateja bwana lazima tuthaminiwe.
Mwishoni nikatoka nje nikaanza transition ya kuhama mtandao, salam kwenu Tigo toka enzi za Mobitel, naondoka.
 
Hvi kuna binadamu makini anaetumia mtandao wa tigo mpaka leo?
 
Tigo hamna kitu, hata jana nilipost thread kuhusu Internet Yao ipo very slow, yani ni kichefchef, hawafai
 
Wafanyakazi wa tigo ni wezi hizo gharama zote ulizosema ulipewa risiti? Nilishawahi kwenda kurenew line pale mlimani city nukaambiwa nilipe 500 ya line mpya nilipodai risiti fasta yule mhudumu akanirudishia hela yangu
 
Hvi kuna binadamu makini anaetumia mtandao wa tigo mpaka leo?
Hili nalo ni neno. Halafu watumiaji wao wengi wapo Dar. Mie walinipata wakati huo ila kwa sasa inatosha. Mpaka watu wengine watakapogundua, sisi tuseme angalau soko liamue.
 
Back
Top Bottom