Salaam kwa Mh. Edward Lowassa na wenzake


Acha kuwa bongo lala hakuna kilichopitwa na wakati lowasa ni mnyonyaji fisadi mkubwa tatizo mshakula vya watu hivyo lazima msifie hata ujinga
 

wezi wazoefu tu nyie mnatumia jina la mwizi mwenzenu kutuibia. UKAWA yatosha Lowa hasa mwizi wa nini?
 
samahani mkuu , kuuliza si ujinga hivi huyu mzee kisori yuko hai kweli mpaka leo ?
Alisha wahi kutishiwa mara kibao na vibaraka wa mafisadi, lakini walimshindwa! yupo nyumbani kwake Arusha akipumzika! Muulize mkuu Ngongo nadhani ni jirani yake.
 
Nia ya Mzee Kasori hapa ni kuchafua jina la Lowasa ili asipate nafasi ya Urais - period. Kwahiyo strategically kwake huu ni wakati muafaka kuibua tuhuma hizi za Mwalimu za takriban miaka 20 iliyopita potelea mbali kama hakuziibua alipoteuliwa kuwa Waziri Mkuu. Makala hii ni marudio, ameshaitoa Raia Mwema huko nyuma ila hapa kapachika nukuu ya Bacon ili kuipamba na kuiongezea uzito. Lakini Mwl. Nyerere mwenyewe alisema yeye hakuwa malaika angeweza kukosea kama binadamu mwingine. Sasa kuhusu hizo mali za Lowasa alizozungumzia Nyerere, Mzee Kassori hazitaji, lakini hata akizitaja hatuna ushahidi kuwa Lowasa alizipata kwa njia haramu! Ni kweli Mwalimu aliwachukia sana viongozi wanaopenda mali, lakini ni ukweli pia kwamba kwa msimamo huu he was in the tiny minority. Watanzania wengi na viongozi wote wanapenda mali. Nina imani majority of current CCM and government leaders are milllionaires by Tanzania standards and this is acceptable because of Azimio la Zanzibar. Na hakuna ushahidi popote duniani kwamba nchi zilizoendelea ni kutokana na viongozi wasiopenda mali. Kwa hiyo Mzee Kasori kumsakama Lowassa kwa vigezo vya Mwalimu ni sawa na kupiga mluzikwenye upepo mkali. Hiyo sakata ya Richmond Lowassa kisha wajibika na kwa dalili za wazi kabisa watanzania wameshamsafisha, bila shaka amejifunza mengi kuweza kuwa kiongozi bora zaidi. The finest steel must go through the hotest fire.
 

mkuu hapa unaandika pumba sana. hivi kweli kwa akili yako unafikiri kuna mtu anachukia kuwa tajiri? Kama tulivyo watanzania leo, isipokuwa watanzania wachache tu waovu kama wewe, mwalimu hakuwa anachukia mtu kupata mali bali alikuwa anachukia mtu kupata mali kwa njia ovu na hasa njia ovu hizo zinapokuwa ni zile za kukwapua mali za umma.

Hueleweki unaposema hakuna ushahidi wa wizi wa mamvi huku ukifahamu kuwa kwa muda wote wa maisha yake ya kazi amekuwa ni mwajiriwa, "mtumishi" wa umma. Hakuna mahali popote tumewahi kuona au kusikia mamvi akifanya biashara japo hata ile ya kuuza mapera au malimao. Hivi huyu mzee, kwa mali zinazotajwa anazo, analipwa shillingi ngapi kwa mwezi na umma wa watanzania hadi aweze kujikusanyia utajiri wote huo? na ujue unapozungumzia mshahara wa mamvi maana yake unazungumzia kodi za watanzania ambao wengi wao ni maskini hohehahe, unazungumzia kodi anayokatwa bibi na babu yangu kule kijijini anapoenda dukani kununua mafuta ya taa au kibiriti au mafuta ya kupikia nusu na robo. Hizo ndo zinakusanywa kwa pamoja ndo mamvi, kama mtumishi wa umma, analipwa mshahara. Hivi ni vikodi hivyo ndo vimemtajirisha huyu fisadi? Kama si hizo ni biashara gani anafanya au amewahi kufanya huyu mzee kiasi cha kujikusanyia hizo pesa anazogawa Kila mahali Tanzania kwa nia ya kununua ikulu ya nchi hii?

Ni kweli kama ulivosema kuwa nchi zilizoendelea si kwa sababu ya viongozi wasiopenda mali, sawa kabisa. Hata hivyo wewe, kilaghai na kiuovu, unatwist maneno ili yasuit context yako. Sentensi sahihi ni kuwa nchi zilizoendelea si kwa sababu ya viongozi wasiopenda mali bali ni kwa sababu ya viongozi wasiopenda mali za wizi hasa wizi wa mali za umma.

Yaani wewe sijui hata unaandika pumba za wapi?!! kwa hiyo unataka kuhalalisha wizi wa mali za umma eti tu kwa sababu, afta all, viongozi wengi wa ccm wanaiba? akili za wapi hizo?!! au ni za ki-uvccm?

Nakushauri Acha kutumia vibaya elimu yako kutetea ujinga kwa faida ya watu wachache au faida ya muda mfupi. Mamvi ni mwizi, hafai kabisa kuwa kiongozi, ni mfano mbaya sana kwa watoto, wajukuu zetu na kizazi kijacho cha Tanzania. Achilia mbali kuwa Rais hata hiyo kutangaza tu nia hakustahili. Ukiachilia mbali wizi hata afya yenyewe ni mgogoro ulio dhahiri. Huhitaji daktari kudhibitisha, ukimwangalia tu hata jukwaani unaona kabisa. Anajitahidi kweli kujikakamaza lakini ukwel ni ukweli tu, sepeto ni sepeto na kijiko ni kijiko tu. huwezi kuficha uhalisia wa sepeto kwa kuliita kijiko kikubwa badala ya kuliita kwa jina lake halisi SEPETO

Akapumzike na wajukuu zake huyo.
 
hizu makala za kinafiki zulikua wapi kama kweli huyu mzee na wengine mnaobwabwaja humu MNA mapenzi mema na hii nchi?tufike pahala tukubali kumpata ati MTU sahihi mwenye hana dosari ndani ya ccm na nnje ya ccm sio rahisi hata kidogo so hayo mapovu yanayowatoka hapa jaribuni kuwa na kiasi lowasa upepo unamwelekea acheni apepee
 
Wewe unaweza kuhoji maoni ya Mwl Nyerere.Kweli nimeamini kupenda kweli upofu.Unataka facts zipi zaidi alizotoa Mwl Nyerere kwenye NEC !.Kwahiyo Mwl Nyerere alikuwa na chuki binafsi na Lowassa Ndossy.

Mwl. Nyerere angeweza kuhojiwa msimlishe Nyerere Maneno!
 
thanks brave man
 
Jambazi sugu na fisadi papa lowasa kamwe hawezi kuwa rais wa tz. Ni mwizi ana fitina hana hoja hawezi kujieleza. Hana ubobezi wa aina yoyote.
Nguvu yake kubwa ni kinunua watz kwa nguvu ya pesa.
 

Sasa wewe Kasori ulikuwa mwandishi wa mwalimu kwa muda mrefu. Serikali ilimwekea utaratibu wa kupata huduma zote ikiwemo na kuletewa magaze,vitabu na majarida aliyopenda kusoma na wapo wa kufanya kazi hizo.Sasa wewe kuacha majukumu yako na kuingia mitaani kusakanya gazeti lenye uteuzi wa Lowassa kama waziri ni kujipendekeza kwa boss au ulitaka asononeke zaidi? Ulikuwa na chuki gani na mh. Lowassa ambayo hadi leo bado unayo kwa kuleta chapisho hili? Sasa mwanae ametangaza nia mwombee mafanikio ukaendeleze ajira yako lakini nina wasiwasi umeshaachwa na umri.
 
Na kweli nimepoteza mda wangu kusoma post ndefu, isiyo na maana yoyote. Umri mwingi huondoa hadi akili mtoa mada baki ucheze na wajukuu, ushapitwa na wakati. El ndio jibu.

ukizoea kujisaidia kwenye kichaka siku kikifyekwa utajisaidia kwenye nguo
 
Moshdar unawajibika kujibu hoja kwa mantiki na busara na siyo jazba inayotawaliwa na chuki yako dhidi ya Lowasa. Hivi aliyekwambia mwajiriwa wa umma/serikali haruhusiwi au hatarajiwi kuwa na mali ni nani hasa baada kufa azimio la zANZIBAR? Je? waajiriwa hawa hawaruhusiwi kuwa na vitega uchumi? Hawaruhusiwi kupangisha nyumba walizojenga kihalali (pengine kwa mikopo)? Are you coming from Mars? Wewe mapato, uwekezaji na vitega uchumi vya viongozi wa Tanzania unavijua? Ninachosema mimi ni kuwa hii stori ndefu ya Kasori haina maana yoyote, na inatakiwa iangaliwe katika mazingira ya azimio la zanzibar (la CCM) na ukweli kuhusu mali walizonazo viongozi wetu hasa tangu utawala wa Mwinyi. Kasori asitishwe mzigo wa kumshauri Lowassa eti asinunue Ranchi. Mbona Mkapa, Sumaye na wengine wanayo mamia ya ekari za mashamba. Au ni ile hadithi ya ndege na bundi???? Ukweli maelfu ya Watanzania wanaomuunga mkono Lowasa wanajua ukweli na hali halisi ya siasa na viongozi wa TZ. Hatuchagui Rais malaika - hayupo popote duniani. Ndiyo maana changamoto kubwa inayotukabili kama taifa ni kuwa katiba inayodhiti/punguza madaraka ya Rais na kuimarisha taasisi zinazojitegemea ili kukabiliana na rushwa. Haya mambo ya Richmond wote walihusika na ilikuwa kwa nia njema kupambana na mgao wa umeme - ufisadi was just a by-product of an already precarious national emergency.
 

Nakuunga mkono sana kwa mawazo yako.Huna haja ya kupoteza nguvu kupambana na nyoka asie na sumu badala yake poteza nguvu kumshughulikia mwenye sumu kwani ana uwezo wa kudhuru na kuua. STRIKE THE IRON WHEN IT IS HOT.Kuendelea kutuletea yaliyopita na mliyoshindwa kuyashughulikia mkiwa madarakani hayatusaidii kitu. Kama ulivyosema wewe mwenyewe ni kiongozi yupi mwenye huo uthubutu wa kuyahoji hadharani maovu yanayotendeka kwenye serikali iliyopo madarakani na abaki salama? Hao waliothubutu leo hii bado tunao? Wakikupenda sana watakupa cheo uwe sehemu ya serikali yao bado huo uthubutu utaendelea kuwa nao?Sasa na wewe mzee Kasori ufisadi ulioujua ni wa Lowassa tu katika awamu zote? Nao ulithibitishwa na mahakama gani? Ni kweli katika uongozi wa boss wako hakuna maovu yaliyotendewa taifa hili? Mbona huyasemi? Tuwaachie wananchi wanajua wampendae kuwaongoza kwani sio lazima atoke ccm.
 

acha kutwist sentest kihunihuni ili kukidhi matakwa yako ya kibinafsi. hakuna anayekataa viongozi wa umma wasiwe matajiri. tunachokataa na vingozi wa umma kuwa matajiri kwa kuiba mali za umma. Kiongozi wa umma ukiwa na mali zinatakiwa ziwe justfiable, uweze kueleza ulivozipata hatua kwa hatua. ni tofauti na kina bakheresa au mengi, wao wakiwa na mali zao, na maadam hawajakamatwa wakimwibia mtu, hakuna atakayehoji. lakini si kwa kiongozi wa umma kama mamvi ambaye, kwa kodi zetu maskini wa nchi hii, tunamhudumia, kisheria na kikanuni, kwa kila kitu mpaka kijiko cha kulia ubwabwa nyumbani kwake.

halafu hii logic yako ya kihuni ya kwamba eti lowasa hapaswi kuhukumiwa kwa mali zake za wizi kisa tu eti mbona na viongozi wote wa ccm wanaiba? huo sasa ni n uhuni. acha uhuni.

Ningekuelewa kama ungesema kuwa, afta all, viongozi wote wa ccm ni wezi na kwa hiyo, logically, ccm yote haifai..hapo walau tungefanya mjadala. ungeeleweka. sasa hii logic yako ya kwamba eti maadam wanaccm wote ni wezi basi na tumchukue aliye mwizi hodari kuliko wote huyo ndo tumpe uongoz mkuu wa nchi ni sawa na kusema "aha, bhanaee, kama mbwai basi na iwe mbwai tu...yaan kama moja limeshaharibika basi potelea mbali, acha yaharike yote kabisa tujue moja"....sasa hiyo ni kuponya au kuangamiza? unatushauri turekebishe kosa kwa kufanya kosa jingine? Achilia mbali watu kama sisi hata watu wa vijijini tu siku hizi hawawezi kukubaliana na ushauri uchwara kama huo wa kwako. watakupinga tu.

tena koma kabisa kusema eti lowasa ana watu wengi, watu wengi wapi? yeye ana watu wa kununua kwa pesa za wizi.

na tena ujue ukishakuwa kiongozi au mtendaji wa umma huishi ishi tu unavopenda wewe, kuwa ukiamua tu, mathalan, kufanya biashara unafanya, ukiamua kuimba tu unaimba....noooooo, kuna utaratibu wake. kiongozi na/au mtendaji wa umma anaongozwa kwa sera, sheria, kanuni na taratibu za uongozi na utendaji wa umma. kuna sheria za kazi na kuna miiko ya uongozi...ukizivunja unashughulikiwa kwazo na, kisheria, hakuna utetezi wa kusema eti mtu asihukumiwe kwa wizi just because na yule pale kaiba?!!!!! what is that wewe??????!!!!!

mzee mamvi akupumzike richmonduli na wajukuze.
 
Watakuja wajinga watabisha ingawa muhusika hawezi kubisha kwani hayo maandiko yapo kitambo muhusika hajawai kukanusha ila wagalatia walivyo wasahaulifu watatetea mpaka mwisho
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…