Sakata la chaguzi za Meya

Sakata la chaguzi za Meya

mastersajenti

Senior Member
Joined
Dec 4, 2015
Posts
165
Reaction score
24
Ninashangazwa sana Na vitendo vinavyofanywa Na viongozi Wa CCM ikiwaagiza watendaji wake "WAKURUGENZI" kuhakikisha Mgombea Wa CCM anakuwa Meya .

Hali hiyo tumeishuhudia maeneo mengi yakiwemo ya Kinondoni , Tanga n.k.Maeneo yote ambayo CCM ina madiwani wachache ndio maeneo ambayo kunatokea vurugu kwani CCM inalazimisha kushinda licha ya kuwa ina madiwani wachache ukweli Vitendo vinavyofanywa Na viongozi Wa CCM na Serikali in kutaka kuiingiza nchi kwenye migogoro Na chuki Kwa wananchi Kwa nini CCM haikubali kushindwa pale inapoona inatakiwa kushindwa?

Suala la Zanzibar no CCM hiyo hiyo imeuvuruga uchaguzi baada ya kuona imeshindwa.Leo unataka mazungumzo Na CUF wakati unaendelea kumpoka ushindi?

Viongozi Wa Dini nao wako kimya wakati wanaona CCM inavuruga Amani wakati wanaona CCM inadhurumu Haki.
 
Kasi ya Serikali awamu ya 5 nilitegemea ingekuwa kwenye kila nyanja.CCM imekuwa inafanya vurugu katika Chaguzi za "Meya" karibu nchi nzima kutaka kulazimisha Ushindi huku ikiwa Na madiwani wachache Na kupelekea kuleta madiwani mamluki Kutika mikoa Na wilaya pia Zanzibar kinyume cha Sheria .Ninashangazwa Na Waziri Mwenye Kasi ya Magufuli amekaa kimya je wangekuwa Wapinzani wanafanya hivyo nadhani wangekuwa Polisi pia Mahakamani Na Viongozi Wa Dini zetu wangewalaamu sana wapinzani kuwa wanachochea Fujo lakini Waziri, Viongozi Wa Dini Na Wanasheria wetu wako kimya.Hivi in haki CCM kuleta madiwani nje ya halmashauri husika kuja kupiga kura?Chonde chonde CCM suala la Zanzibar bado linatusumbua mlipoona mmeshindwa mkavuruga uchaguzi Na kwenye Halmashauri mnafanya hivyo hivyo.
 
Huyo mkurugenzi wa Tanga kawazidi nini wana Tanga? Mfanyizieni!
 
Huu ukondoo wa watanganyika ni laana sio amani. Ni ujinga wa hatari!
 
Kama haya wanafanya kweupe mangapi wanafanya Gizani ccm ni wezi na hawawezi kuruhusu kura halali Ndio maana Zanzibar wamefuta uchaguzi ccm wanatoa vyeo vya u DED kwa maslahi yao
 
hakuna tatizo lolote mameya wanashinda na wanaendelea kutangazwa
na cuf wanampigia ccm
 
hatuna viongozi wa dini wala wanasheria
Viongozi wa Dini ya KIKRISTO wanajua kilicho mpata YOHANA MBATIZAJI,MaAskofu/MASHEHE ni jukumu lenu kuwasemea wanaichi amasivyo Mungu aliye hai atawahukumu.(KAZI MLIYONAYO NI KUFUNDISHA NENO LA MUNGU NA KUKEMEA MAOVU KWA WANAICHI NA WATAWALA)
 
ukitaka kuongoza halmashauri inabidi muwapite ccm madiwani zaidi ya 20 , lakini chini ya hapo watasomba wapiga toka kenya uganda na zanzibar.
 
Wakuu vp huko tanga wamefikia wapi? Shida yote nini ukitaka usipate usumbufu wa ccm muache mbali. Mfano babati mjini chadema 8 ccm 4. Sasa kwenye mayor/ mwenye kiti tumeshinda kilaini bila hata jecha kufuta matokeo
 
Kwa wanadamu haiwezekani kuondoa dhuluma bali tukiamua wacha Mungu tufunge nakuomba tumkabidhi fadhaa zetu.Mungu atasikia atashusha hukumu ya haki kwa kila jambo kwani hakuna kiongozi aliyeapa bila ya kushika vitabu vitakatifu BIBLIA au MSAHAFU.
 
Viongozi wa dini ni wanafiki. Magufuli nae ni mtu wa dhuluma ndio maana anafurahia hayo kwa sababu ndio mfumo uliomuweka hapo. Wizi wizi tu!
 
Huyo mkurugenzi wa Tanga kawazidi nini wana Tanga? Mfanyizieni!
Watamfanyizia wapi wakati hiyo mission ilishajulikana mapema kwa hiyo kuna madefender yalikuwa yamekaa standby.
Kwa hiyo mara tu alipotangaza vyombo vya usalama vikamtorosha chapu chapu na kwenda kumficha mahali kusikojulikana.
 
Back
Top Bottom