Saikolojia ya fedha (The Psychology of money, by Morgan Housel)

Amani Dimile

JF-Expert Member
Jul 27, 2022
243
395
Baada ya kusoma kitabu chote cha Morgan Housel hakika nasema kuwa kuna madini mengi sana kwenye vitabu ila ikiwa tu tutazingatia kuyasoma. Haya yafuatayo ni baadhi ya mambo 10 kwa ufupi sana ambayo Morgan Housel ameyasema ndani ya kitabu chake chenye chapter 20 na page zaidi ya 200.

•Kutafuta fedha na kuzimudu fedha ni vitu viwili tofauti. Lakini hiko cha kwanza hakiwezi kutokea bila hicho cha pili. Jifunze kumudu fedha zako ili uweze kuzitafuta kwa uhuru. Usipoweza kumudu fedha zako basi utateseka maisha yako yote ukiwa unazitafuta.

•Kutumia sana fedha sio kipimo cha kuwa wewe ni tajiri bali kuzitunza na kumudu ndio kila kitu. Morgan anasema kuna utofauti mkubwa sana kati ya Rich man na Wealthy man, na kutokujua utofauti wake basi ni chanzo kikubwa cha kuwa na matumizi mabaya ya fedha.

• Usitumie fedha kwa ajili ya kuwaonesha watu ni jinsi gani una fedha. Hiyo ni njia ya haraka sana itakayokuua.

• Jifunze kutunza sana fedha, kuwa na akiba. Akiba itakupa uhuru wa kupambana na baadhi ya mambo au shida ambazo huwa hazipigi hodi kwenye dunia hii ya mshangao.
Morgan anasema kwamba, tunza tu hela hata kama huna sababu maalumu ya kutunza we tunza tu !

• Usitumie fedha zako zote kununua kitu. Yaani usipende kuchukua hela zako zote (hadi akiba yako) kununua kitu huku ukitegemea kesho ni siku utapata tena fedha zingine.

•Epuka tamaa na ujifunze kuishi bila kushawishika au kukwazika na mitazamo au maisha ya wengine. Housel anaelezea nadharia ya watu wengi kuwa huwa wanatumia fedha zao ili waonekane na wengine kuwa na hela au kuishi maisha ya kushindana.

•Hakikisha unatumia fedha kidogo zaidi ya zile unazoingiza, kamwe usijaribu kutumia kiasi kikubwa kuliko kile unachoingiza. Utakufa ..

•Usifanye biashara kwa kuambiwa na watu. Muandishi anasema kwamba kila kazi ni rahisi sana ukiwa unahadithiwa lakini sio kwa kuifanya. Hivyo ogopa sana kuingia kwenye biashara kwa maneno tu.

•Hakuna kitu cha bure. Morgan anasema kwamba kila kitu duniani kina gharama hata kama gharama zake hazionekani wazi wazi. Hivyo kabla hujafanya jambo lolote linalohusiana na fedha ni lazima ujue gharama za jambo hilo ili lisikusumbue.

•Hasara ni sehemu ya maisha ya fedha, makosa pia ni mapungufu ya mwanadamu. Kamwe usikate tamaa mambo hayo yakitokea kwenye maamuzi yako ya hela..

Tamati, Morgan Housel anatoa mifano mingi ya maisha ya kweli kila anapoelezea jambo Moja. Hakika, kitabu chake kimesheheni mambo mengi sana kuhusu saikolojia ya fedha na kufanya kitabu hiko kuwa kwenye mauzo makubwa sana katika soko la vitabu la dunia.

Ahsante kwa kunisikiliza, naitwa Amani Dimile
1_pk9uzxch4ywrvrxy2-crwg.jpg
 
The best way to save ur money is to spend less and to spend less is to care less about what peoples think about you

Hicho kitabu kina madini Sana I read some chapters i got something new .

Kufanya kazi na Kupata pesa ni Jambo moja ila kumiliki pesa ikae on ur side it's jus hard hii naiona kwa most of peoples Mtu anakula kiunua mgongo mil 80 within three years unamkuta yupo O-O as the same most of imployed hawana Huwezo wa kuimiliki pesa that good book
 
Baada ya kusoma kitabu chote cha Morgan Housel hakika nasema kuwa kuna madini mengi sana kwenye vitabu ila ikiwa tu tutazingatia kuyasoma. Haya yafuatayo ni baadhi ya mambo 10 kwa ufupi sana ambayo Morgan Housel ameyasema ndani ya kitabu chake chenye chapter 20 na page zaidi ya 200.

•Kutafuta fedha na kuzimudu fedha ni vitu viwili tofauti. Lakini hiko cha kwanza hakiwezi kutokea bila hicho cha pili. Jifunze kumudu fedha zako ili uweze kuzitafuta kwa uhuru. Usipoweza kumudu fedha zako basi utateseka maisha yako yote ukiwa unazitafuta.

•Kutumia sana fedha sio kipimo cha kuwa wewe ni tajiri bali kuzitunza na kumudu ndio kila kitu. Morgan anasema kuna utofauti mkubwa sana kati ya Rich man na Wealthy man, na kutokujua utofauti wake basi ni chanzo kikubwa cha kuwa na matumizi mabaya ya fedha.

• Usitumie fedha kwa ajili ya kuwaonesha watu ni jinsi gani una fedha. Hiyo ni njia ya haraka sana itakayokuua.

• Jifunze kutunza sana fedha, kuwa na akiba. Akiba itakupa uhuru wa kupambana na baadhi ya mambo au shida ambazo huwa hazipigi hodi kwenye dunia hii ya mshangao.
Morgan anasema kwamba, tunza tu hela hata kama huna sababu maalumu ya kutunza we tunza tu !

• Usitumie fedha zako zote kununua kitu. Yaani usipende kuchukua hela zako zote (hadi akiba yako) kununua kitu huku ukitegemea kesho ni siku utapata tena fedha zingine.

•Epuka tamaa na ujifunze kuishi bila kushawishika au kukwazika na mitazamo au maisha ya wengine. Housel anaelezea nadharia ya watu wengi kuwa huwa wanatumia fedha zao ili waonekane na wengine kuwa na hela au kuishi maisha ya kushindana.

•Hakikisha unatumia fedha kidogo zaidi ya zile unazoingiza, kamwe usijaribu kutumia kiasi kikubwa kuliko kile unachoingiza. Utakufa ..

•Usifanye biashara kwa kuambiwa na watu. Muandishi anasema kwamba kila kazi ni rahisi sana ukiwa unahadithiwa lakini sio kwa kuifanya. Hivyo ogopa sana kuingia kwenye biashara kwa maneno tu.

•Hakuna kitu cha bure. Morgan anasema kwamba kila kitu duniani kina gharama hata kama gharama zake hazionekani wazi wazi. Hivyo kabla hujafanya jambo lolote linalohusiana na fedha ni lazima ujue gharama za jambo hilo ili lisikusumbue.

•Hasara ni sehemu ya maisha ya fedha, makosa pia ni mapungufu ya mwanadamu. Kamwe usikate tamaa mambo hayo yakitokea kwenye maamuzi yako ya hela..

Tamati, Morgan Housel anatoa mifano mingi ya maisha ya kweli kila anapoelezea jambo Moja. Hakika, kitabu chake kimesheheni mambo mengi sana kuhusu saikolojia ya fedha na kufanya kitabu hiko kuwa kwenye mauzo makubwa sana katika soko la vitabu la dunia.

Ahsante kwa kunisikiliza, naitwa Amani Dimile View attachment 2685946

Sent from my TECNO KE5 using JamiiForums mobile app
Mkuu hiki kitabu nakihitaji,naweza kukipata wapi na gharama zake
 
The best way to save ur money is to spend less and to spend less is to care less about what peoples think about you

Hicho kitabu kina madini Sana I read some chapters i got something new .

Kufanya kazi na Kupata pesa ni Jambo moja ila kumiliki pesa ikae on ur side it's jus hard hii naiona kwa most of peoples Mtu anakula kiunua mgongo mil 80 within three years unamkuta yupo O-O as the same most of imployed hawana Huwezo wa kuimiliki pesa that good book
Na Ile "don't spend money to show people how much money you have" .
Sasa Dr Haya Land, nawe unashauri eti watu wasikisome mpka wajitafute wajipate ????

Sent from my TECNO KE5 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom