GE2025 Said Miraj: Athari za kususia Uchaguzi ni kubwa. Sijui kama CHADEMA wamejaribu kutazama faida na hasara zake

GE2025 Said Miraj: Athari za kususia Uchaguzi ni kubwa. Sijui kama CHADEMA wamejaribu kutazama faida na hasara zake

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Mafyangula

JF-Expert Member
Joined
Jan 16, 2025
Posts
505
Reaction score
887
Mchambuzi wa siasa na mwanasiasa mkongwe Said Miraj amesema kuna athari kubwa sana kwa chama cha upinzani CHADEMA kususia Uchaguzi Mkuu ujao, akitaja mifano kadhaa ya makosa kama hayo yaliyowahi kufanywa na chama chake cha zamani, CUF.

“Ni Uchaguzi wenye sura tofauti. Chaguzi nyingi zilizopita zilikuwa ni baina ya wapinzani na CCM, lakini Uchaguzi huu kwa kiasi kikubwa wimbi la ushindani lipo ndani ya CCM yenyewe kuliko kwa wapinzani. Mimi sitaki kuzungumzia CHADEMA kwenye Uchaguzi huu kwa sababu wenyewe wamesusa, wamesusa,” amesema Miraj.

Aidha, Miraj amefafanua zaidi kuhusu athari za uamuzi wa chama kikuu cha upinzani kususia Uchaguzi huo, akitoa mifano ya matukio yaliyowahi kutokea Zanzibar.

“Labda niseme tu, athari za kususia ni kubwa. Sijui kama wamejaribu kutazama faida na hasara zake. Nikupe mifano sisi Zanzibar tuliwahi kususia mambo kadhaa. Kwanza, tuligoma wanafunzi kwenda shule, serikali ikawazuia kuendelea na masomo, ikabidi tuwatafutie vituo vya kufanyia mitihani Bara. Tulipata gharama kubwa na usumbufu mkubwa.

 
CHADEMA wamefanya uamuzi sahihi sana. Kwa sababu kutoshiriki kwao kwenye huu uchafuzi, kumewasaidia kuwatambua mamluki wote waliokuwa wanakihujumu chama.

CHADEMA iko mioyoni mwa watu wengi. Ikirejea hata kesho kwenye ulingo wa siasa, bado itaungwa mkono na wananchi walio wengi.
 
Hata kama CHADEMA kingeingia kwenye huu uchaguzi mambo yangekuwa ni yale yale ya uchafuzi wa serikali za mitaa 24 na ule uchafuzi mkuu wa Magufuli 2020.

Uamuzi wa CHADEMA ulikuwa ni sahihi.
 
Back
Top Bottom