Saed Kubenea: Sirro atengwe, asulubiwe

Saed Kubenea: Sirro atengwe, asulubiwe

Mwanahabari Huru

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2015
Posts
14,242
Reaction score
34,917
KAULI ya mkuu wa jeshi la polisi nchini, Simon Sirro, kuwa mwa ndishi wa habari, Silas Mbise, aliyepigwa na askari polisi kwenye uwanja wa taifa jijini Dar es Salaam, alishambuliwa kwa kuwa aliingia kwenye eneo ambalo halifuhusiwi, haikubariki na imelenga kutetea uhalifu nchini.

Hii ni kwa sababu, ndani ya uwanja wa taifa hakuna mahali kokote ambako kumepigwa marufuku waandishi wa habari kufika.

Aidha, mwandishi aliyepigwa alikuwa yuko kazini- kama ambavyo polisi walikuwa wakifanya kazi zao- kitendo cha kumshambulia; na au kumzuia kufanya kazi zake, ni uvunjifu wa katiba.

Hivyo basi, hatua ya Sirro kutetea kitendo cha askari wake kupiga mwandishi, kinapaswa kujibiwa mara moja na waandishi na wahariri kwa kuchukua hatua ya kutangaza, kuchapisha, kusambaza na kupiga picha, habari zote zinazomhusu Sirro na jeshi lake kwa ujumla.

Kwani hiyo ndio silaha pekee ya waandishi ambayo tumekuwa tukiitumia kwa miaka nenda rudi.
 
kwa mfano wakichukua hatua hizo ndo suluhu ambayo itafanya jeshi la polisi kurudi katika misingi yake? kuna mda kubenea anakurupuka sana.
 
itakua kama ya yule jambazi kuvamia claudisi usiku na kushurutisha kipindi chake kirushwe, mashilawadu mliungana lakini baadae sijui ni nini kilitokea, anyway na hili mtampa kifungo cha siku saba baadae anawaomba msamaha na mambo yataendelea kama kawaida!
 
Nchi hii inahitaji katiba mpya basi ni hilo tu. Vyama vya upinzani anza kushughulika na mchakato wa kupata katiba mpya achana na ishu za uchaguzi....... Hazina tija tena na ninyi hadi pale katba mpya itakapopatkana.
 
Mnaanzaje kuacha kutangaza habari za makamanda sasa? Jaribuni muone kama hatujaanza kutekeleza sheria inayokataza kuchapisha magazeti binafsi isipokuwa ya Chama na Serikali tu. Na hatutakuwa na mzaha katika hilo😱😈

KAULI ya mkuu wa jeshi la polisi nchini, Simon Sirro, kuwa mwa ndishi wa habari, Silas Mbise, aliyepigwa na askari polisi kwenye uwanja wa taifa jijini Dar es Salaam, alishambuliwa kwa kuwa aliingia kwenye eneo ambalo halifuhusiwi, haikubariki na imelenga kutetea uhalifu nchini.

Hii ni kwa sababu, ndani ya uwanja wa taifa hakuna mahali kokote ambako kumepigwa marufuku waandishi wa habari kufika.

Aidha, mwandishi aliyepigwa alikuwa yuko kazini- kama ambavyo polisi walikuwa wakifanya kazi zao- kitendo cha kumshambulia; na au kumzuia kufanya kazi zake, ni uvunjifu wa katiba.

Hivyo basi, hatua ya Sirro kutetea kitendo cha askari wake kupiga mwandishi, kinapaswa kujibiwa mara moja na waandishi na wahariri kwa kuchukua hatua ya kutangaza, kuchapisha, kusambaza na kupiga picha, habari zote zinazomhusu Sirro na jeshi lake kwa ujumla.

Kwani hiyo ndio silaha pekee ya waandishi ambayo tumekuwa tukiitumia kwa miaka nenda rudi.[/QUOTE
 
Kubenea anamaanisha waandishi walitenge jeshi la polisi? Jeshi la polisi halihitaji kutangazwa, matokeo ya kazi zake ni matangazo tosha kwa wananchi. Kubenea atakua anashida sehemu kichwani kwake.
 
kwa mfano wakichukua hatua hizo ndo suluhu ambayo itafanya jeshi la polisi kurudi katika misingi yake? kuna mda kubenea anakurupuka sana.
amekurupuka vipi? Polisi walimpiga Mwandishi alafu wanaochunguza tukio ni hao hao Polisi unategemea kupata matokeo ya ukweli? Lazima watamsingizia chochote huyo Mwandishi ili kuharalisha Uonevu wao.
 
Walishindwa kijisimamia kwa kitendo cha kuvamiwa clous tv
Hapo hawawezi hata kwa saa 24
mchunguzi wa Tukio la kupigwa Mwandishi ni Polisi na huyo huyo Polisi ndiyo mtuhumiwa unategemea nini?
 
Huyu Kubenea naye kichwa chake naona dishi limeyumba, kadri siku zinavyoenda ndivyo anazidi kuwa na hoja za ovyo ovyo tu shithole
 
...wakichukua hatua hizo ndo suluhu ambayo itafanya jeshi la polisi kurudi katika misingi yake?


Na kwamba kwa kufanya hivyo wata undo kipigo alichokipata huyo mwandishi?
 
kwa mfano wakichukua hatua hizo ndo suluhu ambayo itafanya jeshi la polisi kurudi katika misingi yake? kuna mda kubenea anakurupuka sana.
Wewe ambae haujakurupuka kutoa coment ebu tuambie waandishi wanatakiwa kufanya nini badala yake?
 
Jamani si kuna eneo maalumu kabisa la watu wa 'PRESS'. wakati wa mechi tena wengine upewa beji kabisa kuwatambulisha. Ebu tuwekeeni hiyo clip huyo mwandishi aki'elekezwa' sehemu salama ya kufanya kazi yake ili tuone kama kuna hitilafu za taarifa.
 
Kubenea anamaanisha waandishi walitenge jeshi la polisi? Jeshi la polisi halihitaji kutangazwa, matokeo ya kazi zake ni matangazo tosha kwa wananchi. Kubenea atakua anashida sehemu kichwani kwake.
acha hizo kule Dodoma Kamanda kutwa yupo na vyombo vya habari hata makamanda wengi wanapenda vyombo vya habari ili waonekane wapande vyeo.
 
Saed Hamad Kubenea Mbunge mtarajiwa wa Ubungo kupitia CCM
 
Back
Top Bottom