Sababu za hasira na msongo wa mawazo

Sababu za hasira na msongo wa mawazo

said1994

Member
Joined
Dec 3, 2016
Posts
99
Reaction score
35
Habari wana MMU,

Baada ya kuona kuwa kumekithiri matukio kama, mauaji,vipigo,kufokewa,kutukanwa,kudharuliwa kwa baadhi ya watu nimekuja kugundua yafuatayo

Hasira ina hasara kubwa sana kiafya!!!!
Wengi huwa hawana furaha ila hawajui chanzo cha wao kukosa furaha ni kitu gani!

Basi hapa nakuletea baadhi ya niliyogundua kuhusu hasira na msongo wa mawazo kwanzia vyanzo,athari na matokeo,njia nzur za kuzuia hasira na njia mbaya za kuzuia hasira

1.Mtu mwenye hasira hupata maradhi ya kiafya kama
-Insomnia
-depression
-heart attack
-ulcers
-fatigue
-blood pressure disorder

Kwa jamii mtu mwenye hasira au msongo wa mawazo anapatwa na
1.kugombana na wasiomsababishia hasira
2.kupiga
3.kuua
4.kujeruhi
5.kutukana
6.kufokea wengine
7.kuwakera wengine kwa makusudi

Zifuatazo ni njia mbaya za kupunguza hasira au msongo wa mawazo

1.Vilevi
2.sigara
3.Kutukana
4.kufokea wengine
5.kubwatuka
6.kutukana
7.kuwachukia wenye kuleta msongo wa mawazo
8.kununa

Hayo ni madhara ya kuwa na hasira mtu mwenye hasira uwezo wa kufikiri hupungua na hufanya vitu kwa kukosea zaidi kuliko kupatia!!
Wafanya kazi wengi maofisini wanamatatizo ya kisaikolojia ola wengi hawajijui!!!

Zifuatazo ni sifa za watu wenye matatizo ya kisaikolojia

1.Hukasirika bila sababu za msingi
2.Hutaka kubadili tabia za watu wengine kwa lazima
3.hutukana hovyo
4.Hawawezi kutabsamu akikutana na mgeni ofisini au nyumbani
5.hupelekesha wenzao waliopo chini yao
6.Hulazimisha hoja kwenye mijadala
7.Hawawez zuia hasira hata kwa kitu kidogo

Njia nzuri za kupunguza hasira na msongo wa mawazo
1. Kula vizuri
2.kuweka ratiba ya kujipa furaha
3.Kukikwepa chanzo cha hasira
4.kukubaliana na chanzo cha hasira kama msiba au tabia za watu wengine ambazo huwezi kuzibadili

Vyanzo vingine vya kujipa hasira mwenyewe
1.kutaka kubadiliaha tabia za wengine kwa lazima
2.kutegemea furaha alete mtu mwengine badala ya wewe mwenyewe
3.kuweka mategemeo makubwa kwa wanadamu mfn kuomba kazi kisha mtu akakataliwa huamua kumchukia mwajiri!! Kisha hasira hiyo huzalisha sumu na kumdhuru mwenye kukasirka!!!!

Watu wengi hupata msongo wa mawazo kwa kutaka wengine wawe chanzo cha furaha zao!

Watu wenye matatizo ya kisaikolojoa wapo negative siku zote huona ugumu kwenye kila hali

Hayo ni baadhi niliyogundua watu wengi wanakosa furaha kwa kujitakia!!!!

Hitimisho
Furaha yako ipo mikononi mwako hakuna mwenye wajibu wa kukupa furaha
unaetaka akupe furaha ndiyo wa kwanza kukufanyia maudhi

Umetuma sms kwa mtu hakujibu ukikasirika siyo suluhusho la tatizo
na ukikasirika unazalisha sumu inaua kinga ya mwili wako mwenyewe

Kwa mantiki hiyo wenye afya ndiyo wenye furaha

Na wenye akili chanya hata wakiugua hupata nafuu ya haraka

Mtu mwenye mtazamo hasi hujidhuru mwenyewe kwa kubeba chui moyoni!!

Chanzo cha furaha ni wewe mwenyewe ukitaka uwe na furaha mpaka mwengine aamue basi umepanga kuwa na huzuni!!!!

Umemtumia mtu sms hajakujibu unakasirika !!! Kukasirika siyo suluhisho
 
mimi sipendi kuwa karibu na watu.. nadhani kesi yangu ni nzito zaidi
 
said1994,
Nimeshindwa ku-attach pdf file la kitabu cha saikolojia chenye kuelezea namna gani mtu ataepuka msongo wa mawazo na kujitengenezea furaha yake mwenyewe
bila kutegemea mke,mume,rafiki,mpenzi,ndugu au jirani

Yaani ni practical procedure za kurejesha furaha bila gharama yeyote

Matatizo yote yana suluhisho kama wanadamu watafikiri kwenye kitabu cha Edward De Bono cha "Think before its too late"

Pia pitia kitabu cha ' Stress Proof Brain'
Ingia pdfdrive.com andika utakipata ni kitabu kizuri sana kitakusaidia kuishi kwa furaha bila kuathiriwa na negative influence

Au kwa whatsap
+255766862579 nitakutumia pdf hapa nimeshindw kuiweka
ahsante na uwe na furaha tele
 
Kimsingi ukitenga muda wa kufanya shughuli zako ambazo zinakuletea kipato kukupa maisha utapunguza sehemu kubwa sana ya msongo wa mawazo unaotokana na kuingiliana na watu....

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom