pepsin
JF-Expert Member
- Apr 23, 2015
- 3,486
- 6,172
Lowassa atahama CCM na kwenda chama cha upinzani kwa sababu zifuatazo,
1. Afya yake: Lowassa anajua kuwa afya yake haipo imara sana kumfanya asogeze matumaini mbele ya kuwa rais.
2. Fedha: Lowassa ametumia pesa nyingi sana kwa ajili ya marafiki.Hatakubali kusalimu amri na kuwasaliti marafiki na wafadhili.Atagombea urais ili hata asipoupata,atapata wabunge kadhaa (marafiki) na hivyo kurejesha sehemu ya fadhila.
3. Kukubalika sana: Kwa ushawishi,Lowassa ndio amejitengenezea ushawishi mkubwa kuliko Mtanzania yeyote (Labda Dr.Slaa).
Ushawishi unatokana na rekodi ya utendaji kazi alipokuwa PM na kugawa pesa kwa makundi karibia yote.
4. Kulipa kisasi kwa Kikwete na CCM: Inasemekana kuwa Lowassa ndiye aliyemwingiza Kikwete ikulu kwa makubaliano maalum.Kikwete hajaonekana kumjali na kulipa fadhila,hivyo Lowassa anaona bora Kikwete na CCM yake wapate maumivu ya usaliti.
5. Uhakika wa kuiondoa CCM madarakani: Lowassa anakubalika na ana pesa.Anajua kabisa akiondoka ,CCM itabaki skeleton na hata kama yeye hatashinda urais,UKAWA watashinda tena kirahisi na hivyo kinga dhidi ya Kikwete na watu wake haitakuwepo na yeye atashiwishi(akiwa kama kiongozi mkuu wa upinzani) kushughulikiwa kwa Kikwete.
Kwa sababu hizi na zingine, simuoni Lowassa akiendelea kuimba iyena iyena.
1. Afya yake: Lowassa anajua kuwa afya yake haipo imara sana kumfanya asogeze matumaini mbele ya kuwa rais.
2. Fedha: Lowassa ametumia pesa nyingi sana kwa ajili ya marafiki.Hatakubali kusalimu amri na kuwasaliti marafiki na wafadhili.Atagombea urais ili hata asipoupata,atapata wabunge kadhaa (marafiki) na hivyo kurejesha sehemu ya fadhila.
3. Kukubalika sana: Kwa ushawishi,Lowassa ndio amejitengenezea ushawishi mkubwa kuliko Mtanzania yeyote (Labda Dr.Slaa).
Ushawishi unatokana na rekodi ya utendaji kazi alipokuwa PM na kugawa pesa kwa makundi karibia yote.
4. Kulipa kisasi kwa Kikwete na CCM: Inasemekana kuwa Lowassa ndiye aliyemwingiza Kikwete ikulu kwa makubaliano maalum.Kikwete hajaonekana kumjali na kulipa fadhila,hivyo Lowassa anaona bora Kikwete na CCM yake wapate maumivu ya usaliti.
5. Uhakika wa kuiondoa CCM madarakani: Lowassa anakubalika na ana pesa.Anajua kabisa akiondoka ,CCM itabaki skeleton na hata kama yeye hatashinda urais,UKAWA watashinda tena kirahisi na hivyo kinga dhidi ya Kikwete na watu wake haitakuwepo na yeye atashiwishi(akiwa kama kiongozi mkuu wa upinzani) kushughulikiwa kwa Kikwete.
Kwa sababu hizi na zingine, simuoni Lowassa akiendelea kuimba iyena iyena.