Uchaguzi 2020 Saashisha Mafuwe: Jimbo la Hai limepata Mwakilishi Sahihi aliyekuwa anahitajika

Jul 19, 2020
39
128
Mapema Baada ya kuapa ndani ya Bunge la 12 Mjini Dodoma, Mbunge wa Hai Saashisha Mafuwe akihojiwa na chombo cha Habari cha Dar Mpya amenukuliwa akisema.

Jimbo la Hai lilikosa uwakilishi sahihi kwa zaidi ya miaka 15 na ndicho kilichomsukuma yeye kwenda kuchukua nafasi hiyo maana wananchi wa Hai walichoshwa na uwakilishi wa kiharakati ulikokuwa unalenga masuala binafsi na sio mahitaji ya WanaHai.

"Tulikuwa hatuna uwakilishi sahihi katika jimbo letu, nikaamua niende kugombea ili nitoe uwakilishi sahihi kutoka chama sahihi na kwa serikali sahihi.

Saashisha Mafuwe ameendelea kusema Watu wa Hai walikuwa na uchumi mzuri kabla ya kuingia kwa chama cha upinzani katika jimbo hilo hali iliyofanya kukosekana kwa kiungo kati ya wananchi na Serikali yao.

Saashisha ameng'ara sana kwenye kampeni zake kutokana na Sera yake ya kilimo na viwanda akijinasibu kufufua na kuuhuisha upya Kilimo cha mazao ya asili na mapya katika jimbo hilo ili kuujenga uchumi wa mtu mmojammmoja, Kwa upande wa vijana amedai atahakikisha mikipo yao kutoka taasisi mbalimbali za kiserikali na binafsi inawafikia ili wawekeze kwenye kilimo.

"Jimbo la Hai lina ukanda rafiki sana kwa kilimo cha aina zote, tuna mito mikubwa mitatu inayotiririsha maji Januari mpaka December ,tunayo mifereji ya Asili,Ardhi yenye rutuba hivyo tutafanya kilimo cha Biashara ili tupate faida kwajili ya kuujenga uchumi wa mtu mmojammoja"

Saashisha anasema watu wa hai wanasherekea ushindi wa Chama cha mapinduzi na Uapisho wake kwa kuwa lilikuwa ni hitaji lao la muda mrefu,Pia amesema uchaguzi katika jimbo la Hai ulikuwa huru na haki.

View attachment 1624608
 
Kabla haijaanza Kazi rasmi naomba Uitishe Vikao vya WanaHai Kwa Kata na Tarafa zake tukupe ya kwenda Kufanya Hai. Anza na Wanaoishi DSM na Namba ya Watsup utoe Mheshimiwa Mbunge
 
Hakuna Cha ziada utakachoweza kuwafanyia watu wa hai bro.unajidanganya.ilani yenyewe ya ccm 2020-2025 ni msalaba kwako. Utekelezaji wake ni zaidi ya USD 17 trillion. Pesa mnatoa wapi na corona hii.
 
Ujitahidi zaidi huko hai utaweza kuzalisha waendesha Boda Boda wengi. Hakuna any sustainable development project inaweza kuanzisha Hai. Mradi rahisi Sana pale Hai,malizia ujenzi wa jengo la ofisi ya makao makuu ya ccm Wilaya ya Hai, lilianza kujengwa mwaka 1977 Hadi leo ni gofu .

Hutaweza.
 
Ujitahidi zaidi huko hai utaweza kuzalisha waendesha Boda Boda wengi. Hakuna any sustainable development project inaweza kuanzisha Hai. Mradi rahisi Sana pale Hai,malizia ujenzi wa jengo la ofisi ya makao makuu ya ccm Wilaya ya Hai, lilianza kujengwa mwaka 1977 Hadi leo ni gofu .Hutaweza
Tumtakie kila la heri. Huu mkataba CCM waliouingia 2020-2025 tuwatakie kila la heri.
 
Tumtakie kila la heri. Huu mkataba CCM waliouingia 2020-2025 tuwatakie kila la heri.
Mkataba ccm walioingia na Wananchi 2020-2025 itawasumbua Sana. Na hivi TL anaende kuwachinjia baharini huko donors walipo plus coronavirus crisis Duniani, ccm imejichimbia shimo 2025 hawezi toka kwenye Hilo shimo.maendeleo hayana chama
 
Mkataba ccm walioingia na Wananchi 2020-2025 itawasumbua Sana. Na hivi TL ansende kuwachinjia bahati huko donors walipo plus coronavirus crisis Dunia, ccm imejichimbia shimo 2025 hawezi toka kwenye Hilo shimo.maendeleo hayana chama
Hakika, kila mtu anasubiria kutekelezwa kwa ahadi tamu tamu. Binafsi nimeahidiwa California ndo naingojea kwa hamu.
 
Aache ushamba huyo. Anafahamu wazi hakushinda bali katangazwa kwa nguvu. Sasa aache porojo afufue zao la kahawa na kile kiwanda cha Machinery Tools. Hivyo vyote vilijifia wakati wa ccm wakiwa wameshikilia Majimbo karibu yote Mkoani Kilimanjaro.

Ufufuaji wa viwanda vya zamani siyo kazi ndogo wala siyo masuala ya siasa. Mitambo ya viwanda vile imepitwa na wakati. Makampuni yaliyotengeneza mitambo ile hivi sasa hazipo tena. Kama vipo basi hawazalishi tena vipuri kwani teknolojia imebadilika.

Ni bora mara kumi zaidi kujenga vipya kuliko kuhangaikia vile vya zamani.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom