Ruto regime ni "State Capture"dhidi ya "State Cartel"

voicer

JF-Expert Member
Jul 13, 2020
5,553
11,885
Hakuna "Hustler" bali wakenya wameingizwa mkenge!

Hii inatokana na nilichokiona na kuwasikia mawaziri wateule wa Serikali ya Ruto, mbele ya kamati ya bunge inayohusika na uthibitisho wa mawaziri hao(Vetting).

Nimetafakari sana kusikia kwamba Ukwasi walioutaja leo ambapo wamehojiwa Mawaziri watatu pekee.

Kwanza nianze na Rais Ruto pekee ambaye yuko kwenye orodha ya matajiri kumi wa Kenya akiwa na ukwasi wa 41 billions Kenya shillings.

Halafu makamu wake Richard Gachagua yeye anao ukwasi wa 800millios, Kenya shillings,pamoja na zile 200 millions Kenya shillings,ambazo zilikuwa zimetaifishwa na serikali anafikisha jumla ya ukwasi wa 1 bilion,Kenya shillings.

Leo hii Musalia Mudavadi ambae ni waziri mkuu mteule, Ametaja kuwa ukwasi wake ni 4.1bilions Kenya shillings.

Kuna mwanasheria mkuu mteule Justin Muturi ambae amesema ana ukwasi wa 700 millions, Kenya shillongs.

Mwingine aliefika leo mbele ya kamati hiyo ni Waziri wa Ulinzi mteule Hassan Dualle ambaye ametaja ukwasi wake kuwa ni 851 millions, Kenya shillings.

Kesho orodha itaendelea kwenye kamati hiyo.

MY Take!

Rutto aliweza kuwaaminisha walalahoi wa Kenya kuwa anatetea hustlers wa Kenya akijinasibu na lile toroli.

Lakini ukweli ni kwamba uchaguzi ule ulikuwa ni upinzani kati ya kambi mbili ambazo ni:
Ile ya watoto wa wanasiasa wenye majina katika historia ya Kenya kina Uhuru Kenyatta, Gideon Moi, Raila Odinga na wenzao wengine...
Dhidi ya kundi la waliowahi kuwa watumishi wa umma na kujitajirisha kupitia ufisadi mbalimbali, kulingana na nafasi walizowahi kuhudumu hapo awali, wakiongozwa na William Samoei Ruto, Musalia Mudavadi na Richard Gachagua na wenzao.

Kwa ukwasi huo hapo juu ni wazi kwamba wakenya wameruka matope na kukanyaga maji.

"Mwanasiasa akikwambia usiku umeingia, huku mkiwa ndani,vema utoke nje ukajiridhishe mwenyewe"

Alamsikhi.

View attachment 2390283View attachment 2390284
 
Yale yale!watamalizana wenyewe kwa wenyewe tu!!
Yani kwa mara ingine wakenya wameingia cha kike.

Imagine Makamu wa Rais ameingia Ikulu huku akiwa na kesi ya ufisadi mahakamani.
Halafu cha kwanza alichokifanya Rutto ni kuwafutia mashitaka yote ya kifisadi wateule wake akiwa Aisha Jumwa na Richard Gachagua!

Time will tell....
 
Uko sahihi...na matokeo yake walianza kwa kupunguza kodi kwa makampuni makubwa huku makabwela wakizidi kukamuliwa.
Na kusha wakafuta mpango wa matibabu rahisi kwa wananchi maarufu kama #Obamacare!
Uhuru alijisemea japo kuwa Wakenya wamemchagua Ruto, yeye rais wake ni Odinga🤣🤣🤣
 
Uko sahihi...na matokeo yake walianza kwa kupunguza kodi kwa makampuni makubwa huku makabwela wakizidi kukamuliwa.
Na kusha wakafuta mpango wa matibabu rahisi kwa wananchi maarufu kama #Obamacare!
Lazima wafute Kama huku KWETU NHIF inavokufa kifo cha mende na Michango yake hazijulikani itaenda wapi HALAFU wanakuja na Bima KWA wote!!

Tuisubiri!

Tuliamua Kuwa popo, USA ataacha kutoa misaada kwa who halafu SISI Ndio tumekuja na Bima KWA WOTE ! CHANJO tu za Watoto zimeanza Kuwa adimu sasa hivi effect ya America KWA WHO ngoja Tuone
 
Kenya ni taifa ambalo mabilionea ni mabilionea haswa na wanawatawala maskini ambao ni maskini kwelikweli.
 
Ila huwa nikiifikiria kwa wigo mpana,ninahisi kama Rutto na Uhuru kama vile walifanya kamchezo flani hivi.
Hakuna mchezo. Ruto alijiandaa kuwa rais mara tu alipoapishwa kuwa makamu ile awamu ya kwanza. Ni kama Lowasa alivyokuwa akijiandaa kuwa rais kwenye awamu ya kwanza ya JK yeye Lowasa akiwa PM, sema wenzake wakamuwahi na kumtoa kwenye uPM japo alijiandaa na kuweka matajiri wote upande wake kuondolewa kwake kulimponza.

Uhuru hakujua mchezo wa Ruto, amekuja kushtuka muda umeenda na hawezi mfanya kitu. Akamgeuga kwenye uchaguzi lakini Ruto na genge lake la madon walishajimilikisha njia zote za ushindi
 
Lazima wafute Kama huku KWETU NHIF inavokufa kifo cha mende na Michango yake hazijulikani itaenda wapi HALAFU wanakuja na Bima KWA wote!!

Tuisubiri!

Tuliamua Kuwa popo, USA ataacha kutoa misaada kwa who halafu SISI Ndio tumekuja na Bima KWA WOTE ! CHANJO tu za Watoto zimeanza Kuwa adimu sasa hivi effect ya America KWA WHO ngoja Tuone
Ni kweli kabisaaa!
 
Hakuna mchezo. Ruto alijiandaa kuwa rais mara tu alipoapishwa kuwa makamu ile awamu ya kwanza. Ni kama Lowasa alivyokuwa akijiandaa kuwa rais kwenye awamu ya kwanza ya JK yeye Lowasa akiwa PM, sema wenzake wakamuwahi na kumtoa kwenye uPM japo alijiandaa na kuweka matajiri wote upande wake kuondolewa kwake kulimponza.

Uhuru hakujua mchezo wa Ruto, amekuja kushtuka muda umeenda na hawezi mfanya kitu. Akamgeuga kwenye uchaguzi lakini Ruto na genge lake la madon walishajimilikisha njia zote za ushindi
Hakuna uchaguzi uliowahi kutumia pesa katika historia ya kenya,kama huu!
 
Mbona hujalist pesa za matajiri wengine wa Azimio🚮🚮 Kama Uhuru,Gedion Moi,Raila,Kalonzo,Murathe,Anyang Nyongo,Joho,Junet,Gladis wanga,Ngilu!!!
Kwanza hawa👆ndio wezi wakuu pamoja na marafiki zao!!
Jee unajua walivyo campaign pesa walizotumia Azimio??Pesa,magari,Ndege,Na vitu vyote vya serikali Azimio walitumia na bado walianguka kura ata Kama walikuwa na Deepstate!!!🚮
 
MY Take!

Rutto aliweza kuwaaminisha walalahoi wa Kenya kuwa anatetea hustlers wa Kenya akijinasibu na lile toroli.

Lakini ukweli ni kwamba uchaguzi ule ulikuwa ni upinzani kati ya kambi mbili ambazo ni:
Ile ya watoto wa wanasiasa wenye majina katika historia ya Kenya kina Uhuru Kenyatta, Gideon Moi, Raila Odinga na wenzao wengine...
Dhidi ya kundi la waliowahi kuwa watumishi wa umma na kujitajirisha kupitia ufisadi mbalimbali, kulingana na nafasi walizowahi kuhudumu hapo awali, wakiongozwa na William Samoei Ruto, Musalia Mudavadi na Richard Gachagua na wenzao.

Kwa ukwasi huo hapo juu ni wazi kwamba wakenya wameruka matope na kukanyaga maji.

"Mwanasiasa akikwambia usiku umeingia, huku mkiwa ndani,vema utoke nje ukajiridhishe mwenyewe"

Alamsikhi.

View attachment 2390283View attachment 2390284
Nimekubali hii analysis yako.., umegonga ndipo..,
 
Hakuna "Hustler" bali wakenya wameingizwa mkenge!

Hii inatokana na nilichokiona na kuwasikia mawaziri wateule wa Serikali ya Ruto, mbele ya kamati ya bunge inayohusika na uthibitisho wa mawaziri hao(Vetting).

Nimetafakari sana kusikia kwamba Ukwasi walioutaja leo ambapo wamehojiwa Mawaziri watatu pekee.

Kwanza nianze na Rais Ruto pekee ambaye yuko kwenye orodha ya matajiri kumi wa Kenya akiwa na ukwasi wa 41 billions Kenya shillings.

Halafu makamu wake Richard Gachagua yeye anao ukwasi wa 800millios, Kenya shillings,pamoja na zile 200 millions Kenya shillings,ambazo zilikuwa zimetaifishwa na serikali anafikisha jumla ya ukwasi wa 1 bilion,Kenya shillings.

Leo hii Musalia Mudavadi ambae ni waziri mkuu mteule, Ametaja kuwa ukwasi wake ni 4.1bilions Kenya shillings.

Kuna mwanasheria mkuu mteule Justin Muturi ambae amesema ana ukwasi wa 700 millions, Kenya shillongs.

Mwingine aliefika leo mbele ya kamati hiyo ni Waziri wa Ulinzi mteule Hassan Dualle ambaye ametaja ukwasi wake kuwa ni 851 millions, Kenya shillings.

Kesho orodha itaendelea kwenye kamati hiyo.

MY Take!

Rutto aliweza kuwaaminisha walalahoi wa Kenya kuwa anatetea hustlers wa Kenya akijinasibu na lile toroli.

Lakini ukweli ni kwamba uchaguzi ule ulikuwa ni upinzani kati ya kambi mbili ambazo ni:
Ile ya watoto wa wanasiasa wenye majina katika historia ya Kenya kina Uhuru Kenyatta, Gideon Moi, Raila Odinga na wenzao wengine...
Dhidi ya kundi la waliowahi kuwa watumishi wa umma na kujitajirisha kupitia ufisadi mbalimbali, kulingana na nafasi walizowahi kuhudumu hapo awali, wakiongozwa na William Samoei Ruto, Musalia Mudavadi na Richard Gachagua na wenzao.

Kwa ukwasi huo hapo juu ni wazi kwamba wakenya wameruka matope na kukanyaga maji.

"Mwanasiasa akikwambia usiku umeingia, huku mkiwa ndani,vema utoke nje ukajiridhishe mwenyewe"

Alamsikhi.

View attachment 2390283View attachment 2390284

African politics is a game of the rich.
Unlike the US where tens of millions donate small dollar amounts to their candidate, in Africa, politicians rely heavily on their personal fortune.

Ata Raila angeingia, mawaziri wake pia wangekuwa mabilionea.
 
Mbona hujalist pesa za matajiri wengine wa Azimio Kama Uhuru,Gedion Moi,Raila,Kalonzo,Murathe,Anyang Nyongo,Joho,Junet,Gladis wanga,Ngilu!!!
Kwanza hawandio wezi wakuu pamoja na marafiki zao!!
Jee unajua walivyo campaign pesa walizotumia Azimio??Pesa,magari,Ndege,Na vitu vyote vya serikali Azimio walitumia na bado walianguka kura ata Kama walikuwa na Deepstate!!!
Rudia soma hoja yangu vizuri,ili kujua nilikuwa nikimaanisha nini kuhusu huo uchaguzi.

"State Capture" v/s "State Cartel"....that was my opinions mkuu!
 
Back
Top Bottom