Russia yatishia kujibumapigo ya Marekani

Russia yatishia kujibumapigo ya Marekani

wrong turn

JF-Expert Member
Joined
Feb 17, 2013
Posts
438
Reaction score
170
Russia imeitahadharisha Marekani kuhusu mpango wake wa kupeleka mabomu 20 ya kisasa ya nyuklia kwenye kituo chake cha kijeshi nchini Ujerumani.
Msemaji wa Ikulu ya ya Rais wa Russia Kremlin,
Dmitry Peskov amesema hatua hiyo itavuruga mlingano wa kistratijia barani Ulaya na utajibiwa kwa hatua za kurejesha mlingano huo. Msemaji wa Kremlin ameongeza kwamba hiyo ni hatua nyingine hatari ya kuzidisha mivutano barani Ulaya. Amesema hatua hiyo haiwezi kuimarisha utulivu, kujenga imani na kuimarisha usalama barani Ulaya.
Msemaji wa ikulu ya Rais wa Russia hakusema ni hatua gani zitakazochukuliwa na Moscow iwapo Marekani itatekeleza azma yake ya kupeleka mabomu ya kisasa ya nyuklia kwenye kambi yake huko Ujerumani lakini shirika la habari la Interfax la Russia limenukuu maafisa wa jeshi la nchi hiyo wakisema kuwa yumkini Russia ikajibu hatua hiyo kwa kupeleka makombora yake mapya ya nyuklia ya Iskander-M katika eneo la Kaliningrad huko Ulaya mashariki kwenye mipaka ya nchi za Poland na Lithuania.
 
Back
Top Bottom