Si jambo geni na wala siyo mtindo mpya kwa wapiga kura kupewa vijihela (Tshs 1,500 labda mpaka 10,000) ili wampgie kura mgobea fulani bila kujali ana sela gani.
Pamoja na kuwa kura ni siri, ila mtanzania uliyempa vihela akupigie kura atakupgia tu hata kama huna sera (kwa sababu ni waaminifu)
Na vyama vya siasa ndiyo vinatumia huu mwanya,
pamoja na machungu ya nchi yetu nzuri tuliyo nayo sisi great thinkers, lakini kuna hili kundi la watanzania wenzetu ambao na ni wala rushwa ndogo ndogo (haswa wakati wa uchaguzi)
Hii kweli inarudisha nyuma sana juhudi za ukombozi na kuleta maendeleo
... na huu kweli ndiyo umekuwa mtaji kwa wanasiasa, na inauma sana tena sana kwani unakuta mara nyingi wanaopkea hizo rushwa ni wenye vipato vya chini sana, na hali zao ni duni, na unakuta wanahitaji nukombozi wa kisiasa na kiuchumi, lakini maskini akishachukua hicho ki hela basi anasubiri tena mpaka uchaguzi unaofuata,