Rushwa Chaguzi za CCM na ukimya wa Tendwa

Rushwa Chaguzi za CCM na ukimya wa Tendwa

mdhalendo

JF-Expert Member
Joined
Dec 14, 2011
Posts
282
Reaction score
273
Msajili wa vyama vya siasa nchini Mheshimiwa John Tendwa amekuwa mstari wa mbele kutoa kauli kali dhidi ya vyama mabalimbali vya siasa kwa kile anachokiita "kwenda kinyume na taratibu za kidemokrasia". Mfano mzuri ni kipindi Tendwa alipokuwa mkali dhidi ya CHADEMA kuwa chama hiko kimekuwa hakifuati sheria zilizopo nchini.
Lakini tangu kuanza kwa chaguzi za ndani katika chama cha mapinduzi CCM hatujasikia kauli yoyote ya karipio kutoka kwa msajili huyu wa vyama vya siasa nchini. Rushwa hizo zimeshuudiwa wazi kuanzia katika chaguzi za mikoani, UWT, UVCCM na hata mwelekeo wa jumuiya ya wazazi. Jana Mheshimiwa Zungu amekamatwa na TAKUKURU lakini tendwa bado yupo kimya. Sasa Tunajiuliza kazi kubwa ya Tendwa ni kukemea na kuvitisha vyama vya upinzani pekee?? Kwanini anafumbia macho rafu zinazofanyika ndani ya chama tawala? u kwavile mwajiri wake yupo kwenye chama hicho? Dhambi ya unafiki itammaliza Tendwa
 
Huyo Mzee ni janga la demokrasia na wasipomuondoa mapema nchi inaweza kuingia jkatika vita ya wenyewe kwa wenyewe.
 
Akiwakemea watamnyima kugombea ubunge pindi atakapo staafuu
 
Tena kweli aisee, haka kazee kako wapi?
 
Msajili kivuli hakuna ki2 hapo,ameshapokea mlungula wake huwezi kumuona analembua tena kwenye luninga kama mashi!
 
Jamani jamani, Tendwa yupo kwenye fungate na washiri, na bado anasikiliza ilikuwaje wakashindwa kumfyeka Lema.

BTW Tendwa si wa kumchukilia siriazi ki hivyo, ni kama ngoma inayosubiri kupigwa na mmiliki (CCM) ndipo itoe sauti.
 
Hata jana nimemsikia mtangazaji James Range wa Star TV, kwenye kipindi cha tuongee asubuhi kuwa walimwalika lakini kaingia mitini kwani siku moja kabla (yaan juzi) ndo ilikuwa wafanye naye kipindi lakini akawaomba iwe jana na jana akatokomea kusikojulikana na maada ilikuwa inahusu rushwa kwenye chaguzi.

Kimsingi mzee hana jipya kazeka vibaya, anaumbuka kwani si muda mrefu upite tangu aonyeshe makali ya matamko kwa CHADEMA, lakini kwa hili yupo kimya.
 
Msajili wa vyama vya siasa nchini Mheshimiwa John Tendwa amekuwa mstari wa mbele kutoa kauli kali dhidi ya vyama mabalimbali vya siasa kwa kile anachokiita "kwenda kinyume na taratibu za kidemokrasia". Mfano mzuri ni kipindi Tendwa alipokuwa mkali dhidi ya CHADEMA kuwa chama hiko kimekuwa hakifuati sheria zilizopo nchini.
Lakini tangu kuanza kwa chaguzi za ndani katika chama cha mapinduzi CCM hatujasikia kauli yoyote ya karipio kutoka kwa msajili huyu wa vyama vya siasa nchini. Rushwa hizo zimeshuudiwa wazi kuanzia katika chaguzi za mikoani, UWT, UVCCM na hata mwelekeo wa jumuiya ya wazazi. Jana Mheshimiwa Zungu amekamatwa na TAKUKURU lakini tendwa bado yupo kimya. Sasa Tunajiuliza kazi kubwa ya Tendwa ni kukemea na kuvitisha vyama vya upinzani pekee?? Kwanini anafumbia macho rafu zinazofanyika ndani ya chama tawala? u kwavile mwajiri wake yupo kwenye chama hicho? Dhambi ya unafiki itammaliza Tendwa

Naomba nikurekebishe kidogo hapo kwenye RED, sio vyama mbalimbali ila CDM, hapo anatamani taarifa hizi zingehusu CDM agesha waka
 
Back
Top Bottom