Mimi ni kijana mdogo tuu ambaye mara nyingi hujishughulisha na kilimo na ufugaji.
Sasa mwaka huu baada ya kuvuna alizeti na vimahindi vyangu nikaona isiwe tabu ngoja nifungue kabiashara ka kupumzikia tu kiangazi hiki.
Nikatafta fremu nikafungua biashara na hapo kwenye biashara ndio kwenye mtihani.
Kwenye hilo fremu kuna wapangaji wenzangu (frem +vyumba vya hiyo nyumba) wapatao 8 ambapo hao nane kuna watatu ni wanawake single mamiis na wawili ni wanawake walioolewa Sasa kinachofanyika kinatiaa aibu yani hawa viumbe wananishindania japo Mimi huwa najifanya zuzu kabisa sielewi.
Siku ya kwanza moja namba ya mmiliki wa fremu akasema simu yake Haina chaji nimwachie yangu chaajabu baada ya dakika 2 akanipigia sikupokea halafu akanitumia SMS akaanza stori zingine.
Hawa wanawake wote angalau wananizidi miaka 5+ lakini chaajabu treatment zao zinaonesha dhahiri wananitaka kimapenzii
Achana nao hao wanataka kukufilisi.
Samahani naomba kuuliza, je ulitumia mbegu ipi ya alizeti? Inatoa gunia ngapi kwa eka? Je gharama ya kulima eka moja mpaka kuvuna ni bei gani? Alizeti huko uliuza kwa bei gani?
Unajishughulisha na BIASHARA gani nje ya kilimo na upo mkoa gani mkuu huenda nikaja kukuungisha bidhaa zako mkuu ila hongera kijana mdogo unayejishugulisha