Roho ya kukataliwa

Lukaku marata

JF-Expert Member
Joined
Dec 4, 2019
Posts
448
Reaction score
752
Habari za humu wanajamvi,natumaini mpo poa kabisa.Mimi nikijana wa umri miaka 27 mkazi wa hapa Dar es salaam.
Ningependa kushare na nyie hii hali ya kuwa kama nina roho ya kukataliwa hadi najiona mnyonge sana na mwenye mawazo mara nyingi nikiwa natoa mchango wangu either wa mawazo au kitu wazo langu au kitu changu hakipokelewi bali kitachukuliws cha mwingine kabisa.. Hii hali imenitokea ofisini kiasi kwamba nina mawazo tele,ni hivi kuna kazi ambayo boss wangu ofisini alinipa niifanye sasa baadae akasema hii kazi akabidhiwe mtu mwingine kimsingi huyo mtu ni junior wangu aifanye kuimarisha zaidi sasa baada ya yule junior kufanya ile kazi naona maboss wameipenda kila nikijaribu kutoa kasoro ndo kwanza wanaisifia yaani naonekana useless nabaki nawaza tu,nimeona niwashikishe wadau humu kwa ushauria au kama na nyie mnapitia hali kama hizi na mna manage vipi
 
Kama ulivyosema ROHO ya kukataliwa; kwaiyo mambo ya rohoni yanamalizana ROHONI huko huko so tafuta solution kwa kwenda church kuomba roho iyo iishe..
 
Sasa kwanini ukosoe kitu kizuri jamani,

Nimesoma nikaishia kucheka, kwani ukiwa senior au mkongwe kazn ndio huwez kupitwa na ma junior, mbona kawaida tu maofisini jamani, labda ungetueleza scenario zaid zilizowai kukutokea adi kukufanya ugeneralize kukataliwa, otherwise kilichotokea ni kawaida kwa ofcn na kazi ikishafanyika ikakubalika na aliyeitoa(boss) huna haja ya kuikosoa tena labda kushauri tu ikiwa utaombwa kufanya hivyo, vinginevyo tulia fanya kazi usije kujitengenezea mazingira magumu ya kazi bure. Saingine jifunze kuchukulia mambo kama unavyo yaona, usiende deep ili usijiumize bure.
 
Jiandae kisaikolojia kwa huyo junior wako kazini kuwa boss wako.kuna mambo huwezi kushindana nayo sababu ni either nguvu za Mungu,or za shetani zimetumika ili MTU kufikia malengo yake kama sio juhudi binafsi.

Kama ni nguvu za Mungu huna budi kuwa mpole tu na kushirikiana nae.kama ni nguvu za shetani kama hutojali madhara yatakayotokea or kulipa gharama unaweza shindana nae ukashinda.

Kama ni uwezo binafsi basi boss wako ameshakusoma kuwa una uwezo mdogo wa kiundaji kuliko huyo junior wako,na kweli iko hivyo.so hapo cha kufanya ni kuonyesha ushirikiano na huyo junior ili busara yako ikusaidie kuendelea kupata heshima kuwa ww ulikuwa ni senior wake kazini japo sio guarantee.

By the way usipende sana mambo ya usenior na ujunior kazini hayana tija sana angalia mpunga ndio kitu cha muhimu na ndicho kitu kilichokuleta hapo.
 
Yaani anakazana kukosoa wkt wenzake woote wameshamjua km hataki wachini wafanye vzr.Hawa ni wale najua miye tuu wengine noooo.
 
Hakuna kitu kinaitwa kukataliwa

USSR
 
Kupata tu hiyo kazi inaonesha huna roho ya kukataliwa......ni hofu yako tu mkuu....

Watu wameachwa, hawana kazi, Wanachukiwa hadi na wazazi wao, kila msala wanarushiwa wao, hawapendwi hadi na watoto zao wa kuwazaa...hao ndio wanahaki kusema wanaroho ya kukataliwa...

Usitumie nguvu kubwa sana kushindana na huyo junior wako itafanya uharibu kazi....take it simple kwenye kujifunza kubali mabadiliko
 
Muone kaka mkubwa mshana jr....ipo dawa imechanganywa na upupu unapaka kwenye mpododo kabla ya kwenda kazini..
 

You are not up to speed!!! JIONGEZE ama sivyo utaendelea kudhalilika na mwisho utafukuzwa kazi!!!
 

Kumbe ndo maana watu wanaroga makazini aisee,sasa akiwa senior wangu mbona ntakuwa sina amani na kumleta kazini nimemleta mwenyewe
 
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…