Rished Bade: Taarifa ya makusanyo ya kodi

Hii pesa bado ni ndogo ukilinganisha na wizi unaofanywa bandarini! Haya malengo bado hayashabiani na kiasi halisi kinacho patikana hapo!

Bado kabisa kufikia malengo yaliyo wekwa hakumaanishi hakuna ukwepaji wa kodi!
 
Kama nilisikia vizuri Magufuli alisema serikali inakusanya kodi chini ya kiwango kwa miaka 3 sasa. Sielewi hii taarifa ya TRA kama ni sahihi
 

Wewe umenikuna katika post yako mama!hayo maswali yako mengi ndio majibu!Natamani januari kuwe na bunge jipya la bajeti then tuweke malengo ya kukusanya trilioni 5 kwa mwezi!Kama bil 80 zimepigwa kwa siku chini 2 (achana na ambazo hazijastukiwa) vipi kwa mwezi!?
 
Pale mwisho angeandika "bila kumuonea mtu huruma." Hakuna mtu anaonewa Mr. Bade. Ni vijisenti tu bilioni 80 vinatafutwa.
 
Pamoja na upigaji wote huo twafika kiwango icho am sure uyu mpya anaweza fika 1.5tril kwa mwezi
 
Hawa wapewe 2tril target na wizi wote huu wanafika 100%
 
Kama hayo malengo ya makusanyo wanajipangia wenyewe, basi ni usanii tu hapo..
 
Hivi lengo la makusanyo lkinapangwa vipi? Maana tusiwe tunasifiana kwa kuvuka malengo kumbe tumeweka malengo ya kuruka sufuria wakati tulikuwa na uwezo wa kuruka pipa au hata simtank lita 10,000!
That is also my question....
Kuna kuweka standard za chini ili ku forge mafanikio...
Je hiyo ndio ilikuwa optimum capacity?
 
naona un bashiri mapungufu
Sio hivyo mkuu. Hii nchi imekubuhu kwa ukwepaji wa kodi na nakumbuka Basil Mramba alifanya kazi kubwa sana kutambua wigo wa kodi na kuingiza walipa kodi zaidi kupitia mfumo wa TIN. Hadi sasa wanasema kama mfumo wa kodi ungelikuwa wa haki na usawa ingeliwezekana kabisa VAT kuwa 12%, PAYE 6% na walipaji kuwa na moyo zaidi wa kulipa kwa hiari.
Cha kushangaza TRA wanasema 'wamefikia malengo', na ndio maana nikasema wangelimuuliza vizuri labda angeliwapa ufafanuzi niliouweka lakini kwa hali ya sasa ilitakiwa aseme wamefikia 40% ya kinachotakiwa ili wananchi wanaoelewa ukubwa wa tatizo waje kumuonyesha ni vipi anaweza kuifikia hiyo 98% ya ukweli!

 
Nina hakika hata hayo malengo waliyojiwekea ni madogo mno.Kwa nchi kubwa na tajiri kama Tanzania kukusanya billioni 850 tu kwa mwezi ni utani.Hawa wamejiwekea malengo madogo ili waibe.Ni lazima kuwe na very independent bodies za kuhakiki malengo yao.Tusiwaamini hao,si mmeona wameshatuingiza mkenge.
 
hawa jamaa wakijiwekea lengo la kukusanya trillion 12 ujue kuna trilion 10 hazijakusanywa zipo mikononi mwa wakwepa kodi.
wao wenyewe wanakuwa wametia hasara ya trilion 5.
 

Great thinker Nginana uko right kwa 100%, kujisifia ukusanyaji wa 13% ya GDP ni kidogo sana kwa taifa lililodhamiria kukusanya kodi... point of reference Burundi wanakusanya 17.5% ya GDP, Kenya 18.4%, Ghana 21%, South Africa 26%, Swaziland 39%, Lesotho 42%. JPM anayo nafasi ya kutufikishia makusanyo ya 25% ndani ya miaka 10 akiamua. Go JPM, go....!
 
Tusubiri taarifa ya mwaka ujao
tutalinganisha....

Tuanzie kwanza na assessment ya kuweka malengo, malengo yanawekwa based on previous perfomances au capacities? Nimewahi kuchunguza kampuni moja ambayo uwezo wake kuzalisha (Capacity and opportunities) ulikuwa mkubwa sana lakini kutokana na operational inefficiencies nyingi ikawa hawafikii malengo yake, viongozi wakaamua kukaa na kujiwekea malengo madogo kuendana na walichokuwa wanakipata, laiti kama wangeboresha mambo kadhaa tu basi wangefikia malengo yao makubwa at full potential. Tuchunguze, TRA katika ubora wake wanaweza kukusanya kiasi gani ndio iwe target!
 
Wanaweka malengo kidogo ili wafikie na kuiba nyingi,wapuuzi tu ,
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…