WCB ilim-boost sana kwa sababu, Ricjh alivuma sana halafu akapotea! Kenda kuwa under Kenyan Management wala hakuna cha maana alichokuwa amefanya! Alipoingia WCB ndipo nyota yake ikaanza kung'aa upya kabla hajakorofishana nao! Anachoshindwa kufahamu Mavoko ni kwamba kuna muziki na tasnia ya muziki! Inawezekana anaufahamu muziki sana lakini hana uelewa wa tasnia! Ni uelewa wa tasnia ndio unaoweza kumfanya hata average artist awe ana-shine kuliko talented artist! Hivi kuna anayeweza kupinga kwamba Rubby ni mkali mara 100 ya Nandy wakati ni Nandy ndie ana-shine kwenye game mara 100 ya Ruby! Sababu ndo ile ile, wakati Ruby anaujua muziki huku akiwa amezungukwa na watu wasioijua tasnia ya muziki; Nandy ni average lakini amezungukwa na watu wanaoijua tasnia ya muziki!
Watu aina ya Ruby na Mavoko wanakuwa na kiburi cha kujua, na matokeo yake ndo haya!!!