Acha Mkwara Pape, ukishafanya research ukapata matokeo utayapeleka wapi? Manake ukienda huko wizara ya nishati na pengine wanaposhughulikia mambo ya nishati utakuta report za kila aina za utafiti na mapendekezo mazuri kwelikweli ya kuboresha utoaji wa huduma ya nishati nchini. Lakini wa kuimplement hayo mapendekezo ni nani? Na unaimplement vipi kama hujawezeshwa?
Kuna utafiti umefanyika kuhusu matumizi ya solar power, na umeonyesha kwamba solar power zinaweza kusaidia kupunguza tatizo la nishati nchini kwa zaidi ya asilimia 40. Je kuna intiatives gani zinafanyika kujenga uwezo wa wananchi kutumia solar power? Kujiunga kufanya utafiti huo bila malipo hailipi kwa kuwa hakuna faida nitakayopata. Nitapoteza muda wangu, na wala taifa sitakuwa nimelisaidia. Otherwise uweke wazi hapa kwamba implementation plan yako ipoje. Na sustainability yake ipoje?