Renewing Tanzanian passport abroad

Renewing Tanzanian passport abroad

bmpingo

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2011
Posts
343
Reaction score
197
Kama wengi mjuavyo, Passport zetu hizi mpya (latest) zilianza kutolewa mwaka 2005 na kwa sasa miaka kumi karibu inafika . Mie yangu imejaa na hivyo inabidi kuibadilisha. Kwa kuwa niko nje na ubalozini hawatoi mpya naomba ushauri kwa waliofanikiwa kufanya hivyo muda sio mrefu kwani nimeona vitu vingi vinavyonitoa moyo kama vile kukosekana kwa online forms za passport mpya, kukosekana na clear information kwenye website nyingi za balozi zetu abroad, kukosa clear directive kutoka embassy personnel (I was told, you just come we will help you with anything here, but write an application to head of migration :angry:-can I know a name-!!! asking to be issued new passport). But the fact is , I am paying almost $300.00 to visit the Embassy: early flight in and late flight home and can't pass the night since next day I need to be at work. Please, any advise how to avoid underwater traps will be highly appreciated. I don't mind receiving your comments by emails on blackmpingo (at) gmail (dot) com
 
Baadhi ya balozi za Tz wanatuma passport home na baada ya muda unaenda kuchukua...sijui kama ni utaratibu wa kila balozi au ni effort binafsi za specific balozi...

Niwe honest sikumbuki kama waliituma au walichukua details ila nilipewa passport mpya toka Tz thru ubalozi...

Lakini mbona naona wanakupa ushirikiano...kama wamekwambia nenda watakupa passport what else do you need from them...

You are not supposed to write individual names when writing an official letter...wewe andika cheo cha huyo boss mkuu wa migration...

Ila hakuna balozi inayotoa passport, processing inakuwa TZ...wao wana facilitate tu
 
Thank you nyumba kubwa. Ni kweli in 2005 Embassy delegated an official to our city to take fingerprints, pictures and collect payment. Then, after 3 or 4 months they came back with new passports. This time I presumably, will have to fill up the forms, scan the pictures and fingers, get all endorsements from the Embassy and later, I, on personal cost, will DHL all these documents to Dar. I pray that all run smooth.
 
I really appreciate all who sent me private message on my email. By re-phrasing a common saying: a Tanzanian in need is a Tanzanian indeed. Keep it up guys.
 
Ila watakuwa na ukiritimba...finger prints za nini kama unataka ku replace old passport na new one? si wanazo fingerprints zako...


I really appreciate all who sent me private message on my email. By re-phrasing a common saying: a Tanzanian in need is a Tanzanian indeed. Keep it up guys.
 
Thank you nyumba kubwa. Ni kweli in 2005 Embassy delegated an official to our city to take fingerprints, pictures and collect payment. Then, after 3 or 4 months they came back with new passports. This time I presumably, will have to fill up the forms, scan the pictures and fingers, get all endorsements from the Embassy and later, I, on personal cost, will DHL all these documents to Dar. I pray that all run smooth.

Huko nchi gani?
 
Ila watakuwa na ukiritimba...finger prints za nini kama unataka ku replace old passport na new one? si wanazo fingerprints zako...

Siyo ukiritimba, wanachukua alama za vidole kulinganisha na zile zilizopo kwenye database yao, kuhakikisha kuwa ni mtu yule yule.
 
Kiingereza cha nini? labda wanakutilia mashaka na utaifa wako ndio maana wanakusumbua,ongea nao kiswahili na hapa andika kiswahili tu nadhani watakusaidia haraka sana.
Nalog off
 
Kwani wakitumia za kwenye data base kutengeneza passport na wewe si yule yule si unaumbuka ukipita kwenye machine za kuchekia finger prints mpakani?

Siyo ukiritimba, wanachukua alama za vidole kulinganisha na zile zilizopo kwenye database yao, kuhakikisha kuwa ni mtu yule yule.
 
Kwani wakitumia za kwenye data base kutengeneza passport na wewe si yule yule si unaumbuka ukipita kwenye machine za kuchekia finger prints mpakani?

Siyo wote wanatoka mipakani, wengine wameshafika.
 
Ninaishi nchi ambayo haina ubalozi wa Tanzania, kwa kubadilisha passport ilibidi nitumie uliokuwepo nchi jirani. Nilichofanya, kwanza niliwasiliana na ofisi za ubalozi kwa njia ya simu, wakaniambia kwa kipindi hicho fomu za maombi ya passport ziliisha kwa hiyo wanasubiri watumiwe kutoka Tanzania. Hivyo niliendelea kuwapigia simu karibu kila wiki kujua kama fomu hizo zimeshafika. Ilichukua takriban miezi sita ndio fomu ziliwasili. Baada ya hapo nilisafiri kwenda ubalozini, nilipofika hakukua na usumbufu, nilijaza fomu, nikachukuliwa alama za vidole, nikalipia na kuacha picha. Lakini maelezo niliyopewa ni kwamba hawajui lini nitapata passport yangu kwasababu siku hizi zinatolewa Tanzania tu. Na fomu zangu za maombi haziwezi kutumwa zenyewe tu, watasubiri mpaka wapate maombi mengine matano au ikipita muda bila kupokea maombi watatuma na vitu vingine kutoka hapo ofisini kwao. Hii nayo ilichukua takriban miezi kadhaa nikawa nawapigia simu kila wiki ndio wakaniambia fomu zimetumwa Tanzania.
Baada kama miezi miwili mingine, mtu niliyekuwa nawasiliana naye kwa simu akawa honest kabisa na mimi, akaniambia kama ninasubiri passport yangu itumwe ubalozini itachukua muda na akanielekeza njia nyingine ya kufanya. Niliandika barua ya maelezo kwa passport control officer wa Dar es salaam, kwamba nimemruhusu mama yangu kunichukulia pass yangu ya kusafiria. Kwahiyo niliipata passport yangu kupitia DHL.
Unatakiwa kuwa mvumilivu kwenye vitu kama hivi, kwasababu ofisi za ubalozi hata ziwe Washington, wafanyakazi bado ni watanzania, na operesheni nzima inafanywa kitanzania.

 
Kiingereza cha nini? labda wanakutilia mashaka na utaifa wako ndio maana wanakusumbua,ongea nao kiswahili na hapa andika kiswahili tu nadhani watakusaidia haraka sana.
Nalog off
Sawa mkuu. Nitajirekebisha. Juu ya uraia wangu sidhani kama kuna shaka kwani tuko nao bega kwa bega na hata wakati wa visafari vya nyumbani tunapeana visenti vya kuwapelekea ndugu na jamaa. Mbali ya hapo, kuna facts ambazo ukimwambia mtu hatakuwa tena na wasiwasi na uraia wako. Vitu kama JKT, scholarships enzi za Nyerere na migomo ya Topping Up Allowances kwa wanafunzi wa Eastern Block.
 

Sawa mkuu. Nitajirekebisha. Juu ya uraia wangu sidhani kama kuna shaka kwani tuko nao bega kwa bega na hata wakati wa visafari vya nyumbani tunapeana visenti vya kuwapelekea ndugu na jamaa. Mbali ya hapo, kuna facts ambazo ukimwambia mtu hatakuwa tena na wasiwasi na uraia wako. Vitu kama JKT, scholarships enzi za Nyerere na migomo ya Topping Up Allowances kwa wanafunzi wa Eastern Block.

Pamoja kiongozi,waibie mautundu hao KGB uje uimwage Tanzania ili na sie tuwe na uwezo wa kumwekea kibesi Mmarekani.
Nalog off
 
.... wakaniambia kwa kipindi hicho fomu za maombi ya passport ziliisha kwa hiyo wanasubiri watumiwe kutoka Tanzania. Hivyo niliendelea kuwapigia simu karibu kila wiki kujua kama fomu hizo zimeshafika. Ilichukua takriban miezi sita ndio fomu ziliwasili.....


Maajabu haya, fomu ziliisha?! Makaratasi wanayo kwa nini wasi print?
 
Maajabu haya, fomu ziliisha?! Makaratasi wanayo kwa nini wasi print?

Ndugu yangu, walisema hizo fomu lazima zitumwe kutoka wizara ya mambo ya ndani, Tanzania, nafikiri zinachapishwa kwa makaratasi maalum. Kama nilivyosema hapo juu, process nzima iko kitanzania zaidi. Kama una haraka na mambo yako unaweza kukwama, kwahiyo bora kuchukua tahadhari mapema.
 
Ndugu yangu, walisema hizo fomu lazima zitumwe kutoka wizara ya mambo ya ndani, Tanzania, nafikiri zinachapishwa kwa makaratasi maalum. Kama nilivyosema hapo juu, process nzima iko kitanzania zaidi. Kama una haraka na mambo yako unaweza kukwama, kwahiyo bora kuchukua tahadhari mapema.

Naungana na wewe kabisa. Fomu hizo zimechapishwa kwa karatasi za kawaida ila kila fomu ina namba maalum (serial number) ambayo inaonyesha ni kama vile kuna mtu maalum anagonga muhuri huku akiongeza namba kwenye kila form. Mbili, mambo yanakwenda kibongo bongo tu. Story nyingi na kazi haiendi. Almost siku nzima nimetumia hapo. Cha kutisha zaidi nilidaiwa shahada ya kuzaliwa. Mie mara ya mwisho nilikiona mwaka 1981 wakati natengeneza passport ya kwanza. Nikamweleza kuwa sina na akadai mtanzania yeyote anaweza kuthibitisha kuwa mimi ni mtanzania. Ila anahitajika hakimu au wakili. Passport zangu sita zilizoisha/jaa na kubadilishwa haziwezi kuthibitisha kuwa mimi ni mbongo. Na mara zote walikuwa wanaitaji DN number tu.
 
Naungana na wewe kabisa. Fomu hizo zimechapishwa kwa karatasi za kawaida ila kila fomu ina namba maalum (serial number) ambayo inaonyesha ni kama vile kuna mtu maalum anagonga muhuri huku akiongeza namba kwenye kila form. Mbili, mambo yanakwenda kibongo bongo tu. Story nyingi na kazi haiendi. Almost siku nzima nimetumia hapo. Cha kutisha zaidi nilidaiwa shahada ya kuzaliwa. Mie mara ya mwisho
nilikiona mwaka 1981 wakati natengeneza passport ya kwanza. Nikamweleza kuwa sina na akadai mtanzania yeyote anaweza kuthibitisha kuwa mimi ni mtanzania. Ila anahitajika hakimu au wakili. Passport zangu sita zilizoisha/jaa na kubadilishwa haziwezi kuthibitisha kuwa mimi ni mbongo. Na mara zote walikuwa wanaitaji DN number tu.

Fomu na passport kutolewa kutolewa Dar-es-salaam tu, wanadai ni njia ya kuzicontrol kirahisi, japo sijaelewa hilo lakini tuachie hapo tu. Lakini kuhusu kuwa na cheti cha kuzaliwa ndio ubadilishiwe passport si kweli, au labda kuna sababu nyingine. Mimi nilikwenda na pass yangu, picha na pesa tu, nikapewa fomu kujaza.
Ndio maana mi nafikiri ukiwa nyumbani kwa likizo, hata passport yako imebakiza mwaka na nusu ni bora kubadilisha kabisa kukwepa usumbufu wa kwenye ofisi za kibalozi. Kwenye zile ofisi kuna wafanyakazi wengine wastaarabu tu, lakini wapo wengine huwa nawashangaa kabisa, ukipiga simu au ukienda ofisini kwao hawana moyo wa kusaidia na wana viburi kama ofisi za baba zao.
Hata huwa nashangaa wamewekwa pale kwa sababu gani.
 
Back
Top Bottom