Redio One: Tumshaurini msichana!

Ngekewa

JF-Expert Member
Jul 8, 2008
7,705
1,288
Hii imetoka Redio One: NI hivi: Msichana mrembo ambae alikuwa akifuatwa na wanaume wengi aliamuwa kukubali kuanguka kwa kijana alieonekana amenona. Mapenzi yakanawiri na Kijana akitowa vyake ikiwa pamoja na Gari la Kifahari. Bahati mbaya kijana kashitakiwa kwa wizi kwenye kampuni yake na akawekwa ndani na hali haionyeshi kuwa atatoka karibuni.
Msichana kwa kuthamini penzi lake na la mwenziwe akaamuwa kumuhakikishia kuwa yuko pamojanae ndani ya shida. Akakubali kuvaa pete ya uchumba iliyoshuhudiwa na marafiki wachache wakiwa kule detention. Msichana akawaakienda kule kizuizini huku akimpelekea mchumba wake mahitaji.
Kilichotokea baadae ni kuwa msichana anapokwenda kizuizini anakutana na wazee wa yule kijana na wazee wanaonekana kumyanyapaa msichana.
Anachofikiri msichana na hali hii nzima ni kuwa;
1. Yeye ni mrembo na wengi walishamfuata sasa kwanini asumbuliwe, jee aachane nae atafute mwengine?
2. Jee awambie wazee wa kijana kuwa wao ni wachumba? lakini hii itasaidia kitu iwapo uhusiano wenyew uko hivyo?
Wana JF nini mtazamo wenu?
 
Yani wazo lake la kwanza ni kuwa "Yeye ni mrembo na wengi walishamfuata'!!!!

Namshauri tu amwache huyo jamaa maana inaonekana huyo mdada hana mapenzi ya kweli, bali anajali urembo wake...

Kama anadhani urembo mali, mwambie aende Jolly na Ambience, akawaulize wale warembo kule kwa nini wanajiuza... pambaf...
 
Hii imetoka Redio One: NI hivi: Msichana mrembo ambae alikuwa akifuatwa na wanaume wengi aliamuwa kukubali kuanguka kwa kijana alieonekana amenona. Mapenzi yakanawiri na Kijana akitowa vyake ikiwa pamoja na Gari la Kifahari. Bahati mbaya kijana kashitakiwa kwa wizi kwenye kampuni yake na akawekwa ndani na hali haionyeshi kuwa atatoka karibuni.
Msichana kwa kuthamini penzi lake na la mwenziwe akaamuwa kumuhakikishia kuwa yuko pamojanae ndani ya shida. Akakubali kuvaa pete ya uchumba iliyoshuhudiwa na marafiki wachache wakiwa kule detention. Msichana akawaakienda kule kizuizini huku akimpelekea mchumba wake mahitaji.
Kilichotokea baadae ni kuwa msichana anapokwenda kizuizini anakutana na wazee wa yule kijana na wazee wanaonekana kumyanyapaa msichana.
Anachofikiri msichana na hali hii nzima ni kuwa;
1. Yeye ni mrembo na wengi walishamfuata sasa kwanini asumbuliwe, jee aachane nae atafute mwengine?
2. Jee awambie wazee wa kijana kuwa wao ni wachumba? lakini hii itasaidia kitu iwapo uhusiano wenyew uko hivyo?
Wana JF nini mtazamo wenu?

Hapo kwenye bold ndipo panapoleta matatizo. Mbona kijana hana kosa lolote? Kumuacha ni kuzidi kumtia unyonge kijana.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom