upupu255
JF-Expert Member
- Sep 4, 2024
- 341
- 476
Kwenye harambee ya Ukarabati wa jengo la kanisa Parokia ya Bikira Maria Msaada wa Daima Kome iliyoandaliwa na Muhashamu Askofu Flaviani Katindi Kasala wa Jimbo Katoliki la Geita, kwa kushirikiana na Baba Paroko Padri Japheth Masalu wa Parokia ya Bikira Maria Msaada wa Daima Kome, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Saidi Mtanda ameahidi kutoa Tsh. Milioni 5 kama mchango wa awamu ya kwanza.