Ratiba ya Ligi Kuu Bara ni kichekesho

Ratiba ya Ligi Kuu Bara ni kichekesho

Ulimakafu

JF-Expert Member
Joined
Mar 18, 2011
Posts
31,701
Reaction score
13,671
Ratiba iliyotolewa na TFF majuzi ya Ligi Kuu Tz Bara, ligi inatarajiwa kutimka hapo Agosti 24 mwaka huu mpaka Novemba 3 itakapo simama kwa takribani miezi mitatu mpaka Januari 25, 2014 mzunguko wa pili utakapoanza.Hivi TFF huwa wanafikiria nini timu kukaa muda wote huo wakiwa mapumziko wengi wakilewa na kucheza ndondo mtaani?Inaovyoonyeaha pia kuna kipindi watacheza mechi mbili ndani ya wiki moja,kwa nini ligi isingeendelea kama vile wafanyavyo England na Ulaya kwa jumla,sana sana wanaweza pumzika wiki 2-3 basi ili wachwezaji wasipoteze 'match fitness'?
 
Labda wakubwa wa TFF watalifikiria...............
 
Ukata wa vilabu nao unafikiriwa, kuitunza timu kwa miezi tisa mfululizo huku ikiwa inacheza mechi ni jambo gumu. Pia wanachukua advantage ya mazingira, kwamba ukienda Kanda ya Ziwa umalizane na timu zote za huko, au wa mikoani wakija Dar wanamalizana na timu zote za huku, ndio maana vioja vya timu fulani kuanza ugenini mechi zao zote havyeshi...
Haya yatakuwa sawa endapo timu zote zitakuwa na uwezo wa kuhudumia timu kwa kipindi chote cha mwaka na kusafiri kwa kutumia ndege, usafiri ambao hauchoshi.
 
Ukata wa vilabu nao unafikiriwa, kuitunza timu kwa miezi tisa mfululizo huku ikiwa inacheza mechi ni jambo gumu. Pia wanachukua advantage ya mazingira, kwamba ukienda Kanda ya Ziwa umalizane na timu zote za huko, au wa mikoani wakija Dar wanamalizana na timu zote za huku, ndio maana vioja vya timu fulani kuanza ugenini mechi zao zote havyeshi...
Haya yatakuwa sawa endapo timu zote zitakuwa na uwezo wa kuhudumia timu kwa kipindi chote cha mwaka na kusafiri kwa kutumia ndege, usafiri ambao hauchoshi.

hata wakiwa wanacheza kila baada ya wiki 2 ni poa kuliko kukaa sana naona kuhusu ukata ni kujiendekeza kwani unapocheza ligi kuu kwa sasa inabidi uwe na hela na pia hata tff waache kuzihujumu timu zenye mkwanja wa kawaida hii itasaidia zaidi na ukifanya mfululizo itafanya viongozi wa timu kuwa wanafikria jinsi gani ya kupata hela kuliko kuwafanya wakae miezi 8 tu ya kutafuta hela ya kuendeshea vilabu..
 
jamani huyu jamali malinzi anaujua mpira toka lini, mi najua ye na golf ndo perfect match; nahisi akiwa raisi huyu ni mkenge wa kufa mtu
 
jamani huyu jamali malinzi anaujua mpira toka lini, mi najua ye na golf ndo perfect match; nahisi akiwa raisi huyu ni mkenge wa kufa mtu

Jamaa yuko vizuri tu..,si lazima kuwa alicheza soka kwa kiwango cha juu.......
 
hili swala angelijibu ze next prezda wa tff Jamal Malinzi tujue atasolve vip kama akiwa rais

Hakuna kitu hapo, ni wale wale tu. Kama amedumu kwenye mfumo wa kula akiwa anacheka na kula pamoja ndo ataweza nini? UNgeniambia Wambura ningekuelewa...
 
Last edited by a moderator:
Hakuna kitu hapo, ni wale wale tu. Kama amedumu kwenye mfumo wa kula akiwa anacheka na kula pamoja ndo ataweza nini? UNgeniambia Wambura ningekuelewa...

Wambura huyu huyu????No way...ni mbovu kabisa huyo mshona cherehani.......
 
Back
Top Bottom