Rais wangu Magufuli, kituo cha polisi Manyoni kinanuka Rushwa

Tajiri la Bitcoin

JF-Expert Member
Apr 9, 2017
1,139
707
Wanajamvi habari!
Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Manyoni Bwana Ismail Maulid mkazi wa kijiji cha Mwanzi amethibitika kukamatwa na Ng`ombe wawili wa wizi wenye thamani ya Tsh Mil 3,600,000/= Chanzo cha ndani kinatanabaisha kuwa mwenyekiti huyu ni mwizi wa muda mrefu sasa, amekuwa akilindwa kwa ukaribu na viongozi wa Wilaya akiwemo mkuu wa Kituo cha Police Manyoni mijini.

Ukistaajabu ya Mussa utayaona ya Firauni, Hata baada ya kukamatwa mwenyekiti huyo aliachiliwa baada ya masaa machache huku akiamuliwa kulipa ng`ombe hao ambao tayari alishawauza kwa mfanyabiashara mmoja wa Nyama katika Soko kuu la mjini Manyoni( Jina tunalihifadhi).

Mwenyekitu huyu ameonekana akijigamba hadharani kuwa yeye ndio serikali na hakuna wakumfanya chochote, Taarifa zinasema kuwa jambo hili limekuwa ni kawaida kwa baadhi ya viongozi wa CCM Wilaya ya Manyoni kiasi kwamba wanachi sasa wanaichukia sana serikali ya CCM.

Je adhabu ya kuiba ng`ombe nikulipa ng`ombe?
Je? Kwasasa kituo cha Polisi Manyoni kimegeuka Mahakama?

Wanajamvi ninaendelea kufuatilia na nitawajuza kila kitu kwa uwazi, kama kuna Polisi wamepewa Rushwa nitawaanika hapahapa kwa majina na kiasi walichopewa.
 
sawa kwa taarifa, uchunguzi utafanywa ila hakikisha kuwa umetoa taarifa za ukweli na si vinginevyo
 
Kwanini rais badala ya IGP

Sasa ni nini kazi ya IGP maana hicho kituo cha polisi na huyo kamishna yupo chini ya IGP ,

kidogo rais hebu haya matatizo mpeni IGP ,mnalalamika mnataka rule of law halafu nyie ndio mnaivunja hiyo rule of law ,hili tatizo ni ya kutatuliwa na IGP au kamanda wa mkoa

Aah nimesahau I wish I could be an IGP
 
Wanajamvi habari!
Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Manyoni Bwana Ismail Maulid mkazi wa kijiji cha Mwanzi amethibitika kukamatwa na Ng`ombe wawili wa wizi wenye thamani ya Tsh Mil 3,600,000/= Chanzo cha ndani kinatanabaisha kuwa mwenyekiti huyu ni mwizi wa muda mrefu sasa, amekuwa akilindwa kwa ukaribu na viongozi wa Wilaya akiwemo mkuu wa Kituo cha Police Manyoni mijini.

Ukistaajabu ya Mussa utayaona ya Firauni, Hata baada ya kukamatwa mwenyekiti huyo aliachiliwa baada ya masaa machache huku akiamuliwa kulipa ng`ombe hao ambao tayari alishawauza kwa mfanyabiashara mmoja wa Nyama katika Soko kuu la mjini Manyoni( Jina tunalihifadhi).

Mwenyekitu huyu ameonekana akijigamba hadharani kuwa yeye ndio serikali na hakuna wakumfanya chochote, Taarifa zinasema kuwa jambo hili limekuwa ni kawaida kwa baadhi ya viongozi wa CCM Wilaya ya Manyoni kiasi kwamba wanachi sasa wanaichukia sana serikali ya CCM.

Je adhabu ya kuiba ng`ombe nikulipa ng`ombe?
Je? Kwasasa kituo cha Polisi Manyoni kimegeuka Mahakama?

Wanajamvi ninaendelea kufuatilia na nitawajuza kila kitu kwa uwazi, kama kuna Polisi wamepewa Rushwa nitawaanika hapahapa kwa majina na kiasi walichopewa.
Umesema aliachiwa saa chache baada kukatwa,je wewe ulitaka akae saa ngapi?
Kama alitimiza masharti ya dhamana bado ulitaka aendelee kushikiliwa
Umeonana na kiongozi yeyote mf.uongozi wa jeshi la polisi kumwelezea hiyo ishu bila msaada??
Umeonana na mpelelezi wa jalada ukiwa kama mlalamikaji na alikupa majibu gani?
 
Umesema aliachiwa saa chache baada kukatwa,je wewe ulitaka akae saa ngapi?
Kama alitimiza masharti ya dhamana bado ulitaka aendelee kushikiliwa
Umeonana na kiongozi yeyote mf.uongozi wa jeshi la polisi kumwelezea hiyo ishu bila msaada??
Umeonana na mpelelezi wa jalada ukiwa kama mlalamikaji na alikupa majibu gani?


Ninachokisema nakieelewa vizuri na kama hawatafanya uchunguzi mimi nitarudi tena hapa kutoa habari zaidi.
 
Back
Top Bottom