sifa za rais ajae---2015.
Watanzania changamkieni kutoa ushauri kwenye rasimu ya katiba mpya ili iwe yenye faida kwa wote isinufaishe kikundi fulani kama ya hivi sasa inavyowanufaisha chama tawala cha ccm. Katiba mpya iendane na malekebisho makubwa katika taasisi ya urais, bila kufanya marekebisho katika taasisi hii basi hata katiba mpya itakuwa ni bure kabisa kwa maana haitakuwa na uwezo wa kuboresha mastakabali (future) wa taifa letu.
Msitakabali wa watoto wetu na wajukuu zetu unategemea jinsi tutavyojipanga kuchagua rais atakae toa maamuzi ambayo yatawalinda mbeleni, tusijiangalie sisi tu, ndio maana wanzetu nchi za inje kama marekani, china au japan wanatushinda kila nyanja kiuchumi, kiutamaduni, kisiasa hata kijeshi kwa sababu wanaangalia mbele miaka mia moja au hata miaka mia mbili, sisi hatuna utamaduni huo ambao sasa inabidi au inatulazimu tuanze.
Kwa mstakabali mzuri wa taifa letu rais ajae awe na sifa nyingi , mbili kati ya hizo ni:_
1. Rais ajae awe na sifa ya ujasili wa kuvunja mkataba wa kuuza tanesco umeme iliowekwa na makampuni ya richmund. Dowans na iptl. Mkataba huu ukiachwa uendelee huko mbeleni utasababisha maafa makubwa sana kwa sababu gharama za umeme mpaka sasa ni kubwa sana na tunaambiwa bado shirika linaendeshwa kihasara, kikubwa zinatakiwa fedha nyingi kuwalipa hawa jamaa wanaouzia umeme tanesco. Madhara yake sasa. Gharama kubwa za nishati ya umeme zinasababisha jamii ijikite katiak utumiaji wa mkaa wa mimea au miti, wanajamii ngazi zote mahala popote wanatumia mkaa kupikia ili hali wajiko ya umeme wanayo lakini wameyaweka uvunguni kukwepa gharama, watumishi wa serikali waalimu, polisi, wanasiasa wanatumia mkaa kupikia. Wanasiasa wabunge,wakuu wa mikoa na wilaya wanatumia mkaa kupikia katika familia zao, wafanyabiashara wahindi, waarabu, wasomali sehemu za kariakoo , kisutu wote wanatumia mkaa kupikia kukwepa gharama kubwa za nishati za umeme, pia sisi walala hoi tunatumia kuni au mkaa kupikia suala la umeme hatuliwaziii kabisa. Gharama za umeme zingekuwa chini wakundi mengine yote niliyoyataja hapo juu yangetumia nishati ya umeme, ni sisi walala hoi tu tungeendelea kutumia mkaa na kuni sasa hebu jiulize hali hii ikiendelea miaka 30 ijayo itakuwaje kimazingira ? Milima , vyanzo vya maji vitasalimika kweli? Je kutakuwa na mvua ya kutosha itayowezesha sera ya kilimo kwanza. Ni wazi kabisa hali ya mikataba kama huu wa dowans ukiendelea miaka 50 ijayo taifa la tanzania litapotea katika uso wa dunia. Nini kifanyike. Tunahitaji rais ambae atalinusuru taifa kwa kuliwezesha kutumia umeme utaofuliwa na gesi yetu ambao ni nyingi sana, gesi hii itumike kufua umeme tuachane na umeme wa kununua wa iptl na dowans ili gharama za umeme zipunguwe makundi mengine yatumie umeme watuachie sisi walala hoi tutumie mkaa na kuni. Watu wa mtwara wanahitaji elimu ya uraia tu wataelewa wanashindwa kuelewa kwa sababu viongozi wanaoenda kuwahabarisha hawana maadili.
2. Sifa kuu ya pili ya rais ajae awe na uwezo wa kuvunja mkataba wa mtoto wa mfalme wa saudia wa kukodisha kipande cha ardhi ya loliondo na kutumia kuwindia kwa miaka 30. Makataba huu ni mbovu na unatia aibu ni sawa mtu anakuwa na ubia na mke wako nay eye anakuwa na haki ya kulala nae , mikataba kama hii wajukuu hawataweza kutuelewa, ni sawa na ule mkataba wa kikoloni uliowekwa mwaka 1928 eti nchi za maziwa makuu zilinyimwa ruhusa kutumia maji ya ziwa victoria ruksa hiyo ikapewa misri pekee kutumia maji hayo kupita mto nile si mnaona wenyewe akina lowasa walivyoushitukia mkataba huu pale walipoanza project ya kupeleka maji shinyanga?
Kwa hiyo lowassa ,sijui membe,wasira hawana sifa hizi, watanzania anzeni kutafuta rais ataewasaidia nyie watoto wenu na wajukuu zenu.
Rais atayeweza kifanya haya haraka iwezekanavyo uzalendo wake hauna shaka yoyote kama mlivyoongea vijana, maana kila moja atajiita mzalendo lakini nini kipimo cha uzalendo? Vipimo ndiyo hivyo.
Ebaeban tel.aviv