Chakaza
JF-Expert Member
- Mar 10, 2007
- 39,798
- 71,218
Kuna kundi dogo la wazee ambao bado wako hai wanaolipwa pension na Hazina limesahauliwa sana.
Wazee hao wachache ni wale waliokuwa wamestaafu kabla mifuko ya jamii haijaanzishwa na walikuwa watumishi wa serikali.
Inasikitisha kumuona Meja wa jeshi au Daktari mstaafu akilipwa shilingi laki moja leo na huku hali yake ikiwa Hoi bin taaban.
Pension ya wazee hawa wachache ambao bado wako hai ni ndogo mno kwani viwango vya mishahara wakati wanastaafu vilikuwa vya chini na pension zao hazijapandishwa kwa miaka mingi sana.
Mama wakumbuke hawa wazee waliotumikia taifa kwa uadilifu mkubwa na wengine wamelipigania taifa hili katika vita.
Wazee hao wachache ni wale waliokuwa wamestaafu kabla mifuko ya jamii haijaanzishwa na walikuwa watumishi wa serikali.
Inasikitisha kumuona Meja wa jeshi au Daktari mstaafu akilipwa shilingi laki moja leo na huku hali yake ikiwa Hoi bin taaban.
Pension ya wazee hawa wachache ambao bado wako hai ni ndogo mno kwani viwango vya mishahara wakati wanastaafu vilikuwa vya chini na pension zao hazijapandishwa kwa miaka mingi sana.
Mama wakumbuke hawa wazee waliotumikia taifa kwa uadilifu mkubwa na wengine wamelipigania taifa hili katika vita.