Rais Paul Biya anaongoza kwa 53% Matokeo ya awali Uchaguzi Cameroon

Rais Paul Biya anaongoza kwa 53% Matokeo ya awali Uchaguzi Cameroon

Richer

JF-Expert Member
Joined
Jun 9, 2025
Posts
1,446
Reaction score
2,093
Baada ya uchaguzi wa urais nchini Cameroon uliofanyika Oktoba 12, 2025 Tume ya Kitaifa ya Kuhesabu Kura imetoa matokeo ya awali yanayomuonyesha rais aliyeko madarakani, Paul Biya, akiongoza kwa zaidi ya asilimia 53 ya kura zote

Kwa mujibu wa tume hiyo, Biya amewashinda wapinzani wake, akiwemo Issa Tchiroma Bakary, ambaye amepata takriban asilimia 35

Hata hivyo, matokeo hayo yameibua utata mkubwa, kwani Tchiroma amekuwa akidai ushindi tangu siku chache baada ya kupiga kura

“Nataka kusema kwa uwazi na kwa uzito: wananchi wamefanya uamuzi wao, na uamuzi huo lazima uheshimiwe,” alisema Tchiroma kupitia taarifa yake siku mbili tu baada ya uchaguzi.

Oktoba 12, 2025 baada ya zoezi la kupiga kura kuisha mgombea huyo wa upinzani alianza kutoa matokeo yake binafsi, akidai kwamba ameshinda kwa zaidi ya asilimia 60 ya kura. Ameeleza kuwa takwimu zilizotolewa rasmi “si sahihi” na ameitaka tume ya uchaguzi kuonyesha uwazi zaidi katika mchakato mzima.

Soma pia Kiongozi wa Upinzani ajitangaza Mshindi wa Urais Cameroon, amuomba Rais Paul Biya akubali Matokeo

Mvutano kuhusu matokeo hayo umechochea vurugu kubwa nchini Cameroon, huku maandamano yakiripotiwa katika miji kadhaa. Baadhi ya waandamanaji wameishutumu serikali kwa wizi wa kura, na katika maeneo fulani, maandamano yamegeuka kuwa makabiliano kati ya wananchi na vikosi vya usalama

Soma Wananchi Cameroon waandamana wakitaka Matokeo halali ya Uchaguzi kuheshimiwa

Baraza la Katiba linatarajiwa kutangaza matokeo rasmi kabla ya tarehe 26 Oktoba.

Iwapo matokeo hayo yatathibitishwa, Paul Biya, mwenye umri wa miaka 92, ataendelea kuongoza taifa hilo kwa muhula mwingine, akiendeleza miaka 42 ya utawala wake, na kumfanya kuwa miongoni mwa viongozi waliodumu muda mrefu zaidi barani Afrika



Source: African news
 
Back
Top Bottom