PreGE2025 Rais nitakaemchagua!

PreGE2025 Rais nitakaemchagua!

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

Nomadiq

JF-Expert Member
Joined
Jan 5, 2025
Posts
7,924
Reaction score
20,912
Habari bandugu natumai ni kwema.

Kuelekea uchaguzi wa mwaka huu, kama ilivyo ada haki ya kila mtanzania alietimiza miaka18 kupiga kura. Aidha palipo na haki pana wajibu, wajibu wa kila mpiga kura ni kuzingatia taratibu zote za uchaguzi na kumchagua kiongozi anaefaa kulingana na yeye aonavyo/sera za mgombea.

Rais nitakaempa kura atakuwa na sifa hizi

~awe na akili timamu, za darasani na za kimaisha.
~anaezingatia maoni chanya ya wananchi, haki za binadamu, uwajibikaji na nidhamu za watumishi.
~awe na sera thabiti za kutatua matatizo yanayohusu huduma za maji, umeme, afya, usafiri na elimu.
~awe na nia ya kuleta ufumbuzi wa changamoto ya ajira kwa vijana.
~anaejali utu wa watanzania na waafrika kiujumla.
~asie na ubaguzi hasa wa kidini na kikabila.
~mwenye nia ya kulijenga taifa kiteknolojia (mf. akili mnemba, EVs) kiviwanda, na kisayansi.

Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Sifa ni nyingi lakini nitazingatia hayo katika kampeni zake na portfolio ya miaka iliyopita

Haijalishi ni wa chama gani nitampa kura yangu.
 
Rais Africa ni mmoja tu.
images (4).jpeg
 
Hata kama, lakini ameshakuwa kwenye utawala wa kiraia, kwa nini asivae tu kawaida suti kali. Nadhani ana ujana-utoto pia
Suti ndio vazi la maana ? Lina signify nini na kwanini ?; Yeye anaweza kusema anavaa kijeshi sababu bado yupo kwenye mapambano, vilevile mavazi who cares so long as au kama anatekeleza ambayo yalikuwa hayatekelezwi kabla ?

Pili Politics it's all about image na huenda anafanya hivyo kama Sinkara incarnated ingawa yeye alikuwa anavaa kofia ya kimapinduzi (appearance ina nafasi yake kwenye politics); Case in Point, Gandhi alivaa shuka akionyesha kuondokana na utegemezi wa Wakoloni na viwanda vyao...
 
Wewe Rais utakayepewa choice ya kumchagua ni yule utakayeletewa mezani umchague; Those who nominates, chooses....
 
Back
Top Bottom