Rais niliyekuwa namjua hapo mwaka 2005

Ndallo

JF-Expert Member
Oct 1, 2010
7,619
4,293
Nimeangalia TBC 1 leo usiku saa 2:00pm tarehe 7/01/2011 kwakweli mimi ni mtanzania na pia namjua raisi niliye mchagua mwaka 2005/sio mwaka 2011! lakini kwa sura niliyoiona ya JK kweli kabisa hana raha na maisha anayoishi pale ikulu hata sura ukiiangalia utaona kuna kitu kinamsuta na amenyong'onyea! kama wenzangu mmeangalia pale akiwa anapongezwa na wale mabalozi wa nnchi mbalimbali ambao JK aliwaalika utaona kuna taswira fulani kwenye macho yake! hakika si yule Jakaya Mrisho Kikwete niliye mjua mwaka 2005! natanguliza hoja wana JF!
 
kaka ndallo nakuunga mkono asilimia mia, mimi mwenyewe nilikua nacheki news na mther alizungumza maneno yaleyale unayosema kwamba kikwete anaonekana hana amani moyoni na hana furaha. Naamini sababu kubwa ni matokeo ya uchaguzi wa mwaka jana yanazidi kumtesa na kumuumiza kichwa. Anakumbuka jinsi alivyokua anakubalika mwaka 2005 na ushindi wa tsunami alioupata wa 80% bila kutoka jasho, anajiuliza amewakosea nini watanzania katika kipindi cha miaka hiyo mitano hata wamchukie kiasi hicho na kupata ushindi wa 61% tena unaotiliwa mashaka. Anakumbuka mwaka 2005 alipigiwa kura hata na wapinzani ambao wengine walidiriki kumpatia yeye kura za uraisi lakini wakapigia upinzani kwenye kura za ubunge. Miaka mitano baadae watu wanadiriki kusema kura ya rais kwa slaa ya mbunge kwa mwakyembe. wabunge wake hgii leo wanakubarika kuliko yeye mwenyewe aliyewabeba mwaka 2005. Kwa kweli hata kama ni wewe kaka ndallo lazima roho itakuuma na utakua na msongo wa mawazo. Kweli tangu matokeo yalipotangazwa rais wetu amekua hana furaha ile aliyoingia nayo mwaka 2005 ambapo alikua akifanya ziara kibao za kushtukiza kwenye maeneo ya hospitali, sokoni, misibani nk.
 
Angejiuzuluu kulinda heshima na historia isichafuke zaidi...hana jipya na usanii wake....uwezo wake mdogo namnaile anajuta kwa nini aliomba term ya pili!!!!aibuuu JK uwezo mdoogooo.... Hana hata fikra za kuandika katiba kuwa inakuwa ya kitaifa zaidii ya kuwateua wawajibike kwake yeye anataka uswahiba na kulipana fadhila kila kitu hata hajuii kwelii....sasa anajuaa nini kuvaa na kusafiri???
 
2005 kauli mbiu yake ilikuwa" ndugu zangu watanzania taifa letu ni tajiri sana_hakuna sababu ya kuishi maisha haya, tatizo kubwa lililopo serikalini ni udhibiti wa matumizi mabovu ya serikali na kuelekeza nguvu zaidi kwny huduma za kijamii" kiukwel kwa kaul hiyo wakati huo mi nilikuwa kule swanga_kiukwel nilijipa kaz ya ukada wa huyu ndugu, lakin amenidisapoent kwasasa nadhan kuliko mtanzania yeyote_yaan kaniboa na kunikatisha tamaa, cna namna ya kueleza_nadhan nimechoka kulivyoanvyoonekana yeye
 
Back
Top Bottom