Naanto Mushi
JF-Expert Member
- Oct 16, 2015
- 6,236
- 15,602
Hichi ndo kipindi Rais anatakiwa kuonesha ukomavu wa fikra, weledi, na kufanya maamuzi ya manufaa. Baada ya tamko la USA jana ni dhahiri lazima serikali iseme kitu ama la ifanye maamuzi ya kimkakati.
Kama ingalikuwa sisi ni 'Russia' tungekwenda jino kwa jino (tungevimba), ikiwa na maana na sisi pia tungepiga travel ban kwa afisa yoyote wa USA mwenye ushawishi. Ila kwa sababu sisi sio 'Russia' yafaa Rais afanye tathmini ya ni vipi amezipokea hizi taarifa na ni vip anazifanyia kazi.
Busara kubwa kwa sasa ni viongozi wa serikali kujizuia kutoa maneno yoyote ya jazba dhidi ya USA. Kumtolea jazba ama kejeli USA litakuwa kosa moja kubwa sana kufanywa na utawala. Huwezi kuitolea jazba USA tena kwa tamko lililotolewa na Secretary of State 'Michael Pompeo' huko ni sawa na kucheza na moto na tukifanya hivo tutaungua.
Busara hapa ni kujishusha, Rais ajishushe ikibidi ili kuonesha ameguswa na tamko, amuondoe hata Makonda kwenye ukuu wa mkoa.
Kinyume na hapo, kuvimba maana yake ni kwamba tunaenda kuwa Zimbabwe mpya. Ukweli usemwe kwa reserve hii ya Dola bilioni 5 hapo BOT tukipigwa sanction leo uchumi wetu hauta survive hata miezi 4. It will be dead than abyss.
Rais na serikali yako, toa tamko.. jishushe jishushe jishushe jishushe ukivimba Tanzania itapasuka.
Kama ingalikuwa sisi ni 'Russia' tungekwenda jino kwa jino (tungevimba), ikiwa na maana na sisi pia tungepiga travel ban kwa afisa yoyote wa USA mwenye ushawishi. Ila kwa sababu sisi sio 'Russia' yafaa Rais afanye tathmini ya ni vipi amezipokea hizi taarifa na ni vip anazifanyia kazi.
Busara kubwa kwa sasa ni viongozi wa serikali kujizuia kutoa maneno yoyote ya jazba dhidi ya USA. Kumtolea jazba ama kejeli USA litakuwa kosa moja kubwa sana kufanywa na utawala. Huwezi kuitolea jazba USA tena kwa tamko lililotolewa na Secretary of State 'Michael Pompeo' huko ni sawa na kucheza na moto na tukifanya hivo tutaungua.
Busara hapa ni kujishusha, Rais ajishushe ikibidi ili kuonesha ameguswa na tamko, amuondoe hata Makonda kwenye ukuu wa mkoa.
Kinyume na hapo, kuvimba maana yake ni kwamba tunaenda kuwa Zimbabwe mpya. Ukweli usemwe kwa reserve hii ya Dola bilioni 5 hapo BOT tukipigwa sanction leo uchumi wetu hauta survive hata miezi 4. It will be dead than abyss.
Rais na serikali yako, toa tamko.. jishushe jishushe jishushe jishushe ukivimba Tanzania itapasuka.