Rais Magufuli tunaomba uingilie kati hapa

Nini maoni yako juu ya eneo la hifadhi ya Ngorongoro.

  • Manongi abaki

    Votes: 0 0.0%

  • Total voters
    9
  • Poll closed .

Monasha

JF-Expert Member
Apr 2, 2011
561
422
1153131

Kwa miaka ya hivi karibuni, eneo la bonde la Ngorongoro limekuwa likikumbwa na migogoro ya aina mbalimbali hasa ya migongano ya maslahi. Maslahi haya ni kati ya wenyeji waishio katika eneo hili na hifadhi ikiongozwa na Mamlaka ya hifadhi ya eneo hili. Kumekuwa na uibukaji wa sheria mbalimbali za kuwabana weenyeji hawa katika eneo lao hili ambalo ndo hutegemea kwa maendeleo yao. Uongozi wa sasa umeanzisha sheria ya kuwazuia wenyeji kutofika na kufanya shughuli yeyote katika baadhi maeneo (NO GO ZONE).
Kuanzishwa kwa No Go Zone siyo tatizo, tatizo ni pale uongozi husika unapoamua kuanzisha makatazo bila ya ushirikishwaji. Ikumbukwe kwamba wenyeji hawa wana viongozi wao wa kiserikali na viongozi wa kimila. Katika uongozi wa awamu zilizopita, hakujawahi kutokea ubabe wa aina hii wa kuwapuuza wenyeji katika ushirikishwaji wa mambo mbalimbali yahusiyo eneo lao. Daima kumekuwepo na ushirikishwaji ulioleta usawa katika kufanya maamuzi juu eneo hili. Lakini cha kushangaza, uongozi uliopo ukiongozwa na Fredy Manongi (Mhifadhi Mkuu) umekuwa ukifanya maamuzi bila ya ushirikishaji kabisa. Hili limeleta mtafaruku na taharuki kubwa sana miongoni mwa wananchi hawa.
Jana tarehe 13/07/2019 jamii ilikutana kuyaongelea haya kuonyesha msimamo wao hasa juu ya uongozi wa bwana Manongi ambapo kiuhalisia bila kumumunya maneno, Manongi na uongozi wake hawahitajiki katika eneno lile. Na wakiendelea kuwepo basi watahatarisha maisha na shughuli za eneo la bonde la Ngorongoro. Ifike mahali Rais aliingilie hili kati maana licha ya viongozi wa chama tawala kufika katika eneo hili mara kwa mara, bado hakuna suluhisho lililopatikana. Suluhisho pekee tunaloliona kwa sasa ni Rais kutoa tamko juu ya matendo ya uongozi uliopo katika eneo hili.
Tunaomba sana, kwakuwa Rais Magufuli toka aingie madarakani hajawahi kulitembelea eneo hili na kujionea yanayoendelea, hakika afike siku moja na ninaimani kwamba atajiuliza kwanini hakufanya maamuzi ya kulitembelea eneo lile mapema sana.

Hapa unaweza kuona malalamiko toka viongozi wa kimila kuhusu uongozi wa Manongi. Kikubwa utagundua kwamba mahusiano kati ya managementi ya NCAA na wananchi inapungua mwaka hadi mwaka. Ndio maana tunataka angalau kiongozi wa nchi aliingilie hili kati ingali mapema maana tunakoelekea ni kubaya sana.
Kama ni kwamba wenyeji hawa hawatakiwi tena katika eneo lile basi liwekwe wazi na siyo kuendelea kuwanyanyasa. Hawa ni wananchi kama walivyo wananchi wa maeneo mengine Tanzania. Wanahitaji huduma zote za kibanadmu katika maendeleo yao. Fikiria mpaka wananyimwa kujenga shule na miundo mbinu zingine hata kwa nguvu yao wenyewe. Je vizazi vyao vijavyo vitaishi vipi?
 
Wenyeji mlitakiwa muwe mbali kabisa na kreta, kwasababu mmepafanya kuwa sio hifadhi. Mmeacha zile nyumba za asili sasa mmejenga majengo ya kisasa
Ndungu unaposema mbali, mfano maeneo gani hasa. Na nyumba za kisasa unazozisema ni zipi maana sisi pale hatuna ruhusa ya kujenga nyumba za kisasa?
 
Ndungu unaposema mbali, mfano maeneo gani hasa. Na nyumba za kisasa unazozisema ni zipi maana sisi pale hatuna ruhusa ya kujenga nyumba za kisasa?
Kwan eneo hilo ndo lile ambalo muarab yule amehodhi au
 
Ndungu unaposema mbali, mfano maeneo gani hasa. Na nyumba za kisasa unazozisema ni zipi maana sisi pale hatuna ruhusa ya kujenga nyumba za kisasa?
Zile nyumba za bati upande wa magharibi mwa kreta sio zenu?
 
Hahaha to cast vote kwa kitu tusichokifahamu?! Kwanini tu vote, what is going on,, since when vyeo vya kuteuliwa mmeanza kuvitolea maoni?!
 
Huyo jamaa atakuwa anazungumzia zile ofisi za NCAA zikizopo pale magharibi njiapanda ya Serengeti na Endulen!
Hapo njia panda ya Endulen kuelekea kule Amberway ukisogea mbele kuna majengo japo siyo ya kisasa ila ni nyumba nzuri kama zilizopo mjini fully solar.

Kikubwa hapa hii jamii ya maasai itengenezewe utaratibu badala ya ubabe, nakumbuka kule font ikoma kulikuwa na sheria kwa askali aliye pale na familia kijana akimaliza shule iliyopo pale mzazi unatakiwa kumpeleka nje ya kambi.

Hii ilitokana na sababu maalumu iliyokuwepo eneo lile.
 
Back
Top Bottom