Maisha yamekuwa magumu sana mtaani

KISHADA

JF-Expert Member
Oct 18, 2012
2,224
3,290
Mkuu wetu tumeona jitihada zako kuanzia kutumbuwa kule bandarini na kushughulikia wakwepa kodi,kushughulikia waliovamia viwanja na ubomoaji hapa Dar es Salaam, kuzuiya vibali vya kuagiza sukari nje na kubana matumizi ya serikali.Nadhani ilikuwa lengo ni kuimarisha maisha ya wananchi na kuleta maendeleo.Wataalamu mbali mbali na wanasiasa kila mmoja na uoni wake wengine wanaponda wengine wanasifia wengine wanatoa muda wanasema ni mapema.

Jambo moja mimi naliona rais wangu, WAKATI JITIHADA HIZO ZIKIENDELEA NI UKWELI ULIO WAZI KWAMBA MAISHA YA WANACHI YANAZIDI KUWA MAGUMU. Fedha imekuwa adimu na ngumu kupatikana, bidhaa zimekuwa ghali mno, biashara zimepwaya na baadhi ya bidhaa kuwa adimu kidogo (Sukari)

Ajira ni ngumu na misuguano ya kisiasa imeanza kuchipuka yote haya yanafanya maisha ya jumla ya wananchi kuwa magumu.Tunahitaji majibu sahihi maana wengine tulitarajia wakati jitihada hizi zikiendelea basi unafuu wa maisha uanze kupatikana sasa kuna nini huko tatizo nini?

Nafikiri kwa uoni wangu hili ni suali muhimu kwa rais wetu Dr Magufuli.

Kwanini maisha ya wananchi yanakuwa magumu licha ya jitihada hizi?

Asante.
 
Mimi nasubiri sukari ifike 2000 kwa kilo. Nasubiri mgao wa sukari bure kwa ile iliyokamatwa imefichwa. Mpemba ananiuzia kilo sh 4000. Rais wetu tusaidie ishuke hadi 2000 au 1500
 
Hizi zote ni jitihada za Bwana Raisi kufanya wote walioshi kama malaika waishi kama mashetani. Sasa kila anaepata ugumu ajijue keshaanza kuishi kama shetani. Tusubiri kuota pembe tu
 
Je pengine Ni Elimu bure? Ni jambo ambalo halikuwekewa mipango mathubuti Ni la ghafra sana?? Ebu tupige hesabu vizuri huenda ndio chanzi cha Hali kuwa ngumu ghafra..Shule NA msingi za serikali zipo ngapi Tanzania Nzima. shule za Serikali za secondary.

Sasa bila vyanzo vya mapato vya Uhakika Pesa iliyopo kwenda kulipa ada NA matumizi ya kawaida mashuleni huko Sio kwamba imechangia Hali NA Huduma sehemu zingine kukwama Mfano Madawa hospitalini,kusitishwa kwa ajira mpya,mikopo ya Elimu ya juu kutolewa kwa wanafunzi wachache?? Je Haiwezi ikawa Iyo ndio chanzo??

Kichwa kinauma kwa mawazooo. NA kama ndivyo ivyo. Tu naomba Mkuu wa Kaya arudishe Ada mashuleni ili Pesa zile zielekezwe Kwenye mambo mengine nyeti kama Mada wa hospitalini kulipa madeni ya watumishi pia NA Ajira mpya.Maana Hali nilipofika Ni Mbaya kuwai kutokea.

Elimu bure Ni nzuri Lakini Je imefanyika Research ya Uhakika kuendana nayo au ndio Sababu ya Hali kubadilika ghafra. Je, wewe mwananchi mwenzangu unadhani ghafra Pesa imekimbilia wapi au Ni nini Tatizo mbali Na niliyoandika.

Ufafanuzi kwa anayejua zaidi ya haya.
 
Yaani bora tulipe Ada . Naona elimu bure ni story tu. Kwanza inatulemaza. Ni bora mtu ukomae ujue kabisaa serikali haina msaada.

Hawa jamaa walikuwa wanataka njia tu ya kuingia Whitehouse lakini hawana msaada kwetu kabisaa. Ndo yale mtu alisoma buree kuanzia chakula mpaka pesa ya kumpelekea bibiyake anaporudi likizo leo anakyja na majibu ya vijana kutumia pesa vibaya kwa kununua TV na ulevi. Anauhakika hivyo vitu watu wanafanya kwa pesa ya mkopo???.

Huko vyuoni tunakutana na watu toka familia/mataifa mbali mbali je wote wanakipato sawa??. Isijekuwa wanaona watoto wa wakulu alafu wanakuja kuumiza watoto wa maskini. Kweli kabisa it's not fair
 
Duh!!!! Kweli maisha yamekuwa magumu kwako, yaani usiku mnene wote huu huna usingizi na unaanzisha thread, pole sana aiseee, kaza utatusua tu mdogo wangu.
 
swala la Elimu bure ni mh Lowassa na ukawa ndio wanajua jins ya kuwapa elimu bure sio hao ccm wanaiga tu kisha wanashindwa kutekeleza ILANI YA UKAWA.

SWISSME
 
Maisha yamekua magumu sababu pesa za madili/misheni town zimebanwa, kodi inalipwa, sheria zimekazwa na kufuatwa. Kwa waliokua wanafanya mambo kienyeji Lazima waone maisha magumu.
 
Maisha yamekua magumu sababu pesa za madili/misheni town zimebanwa, kodi inalipwa, sheria zimekazwa na kufuatwa. Kwa waliokua wanafanya mambo kienyeji Lazima waone maisha magumu.
Kusema ukweli mnavyosemaga madili hata sielewi ni madili gani hayo mnayafanyaga yaliyokua yanawasave.....em nipe mfano...
 
Kusema ukweli mnavyosemaga madili hata sielewi ni madili gani hayo mnayafanyaga yaliyokua yanawasave.....em nipe mfano...
Pesa nyingi ilikua inazunguka bila kuwa taxed. Mfano mimi mwenyewe nimewahi kutoa mashine bandarini kwa 3mil wakati ilibidi nilipe 8mil hiyo yote iliwezekana sababu nilikua nafahamiana na wahusika pale
 
Maisha yamekua magumu sababu pesa za madili/misheni town zimebanwa, kodi inalipwa, sheria zimekazwa na kufuatwa. Kwa waliokua wanafanya mambo kienyeji Lazima waone maisha magumu.
Ko hizo pesa za misheni town ndo zilikuwa zikitumika kununulia dawa hospitalini, kutoa mikopo kwa wanafunzi, kuajiri watumishi na kupandisha madaraja watumishi siyo?
 
Pesa nyingi ilikua inazunguka bila kuwa taxed. Mfano mimi mwenyewe nimewahi kutoa mashine bandarini kwa 3mil wakati ilibidi nilipe 8mil hiyo yote iliwezekana sababu nilikua nafahamiana na wahusika pale
Anha nimeelewa...ila naitaji mfano mwingine
 
Nashangazwa sana Na majibu ya Kejeri anayoyatoa Bibi.Huyu.Sijui kwa kuwa aliyepotea sio ndugu yake sio Mtanzania mwenzake Jirani yake basi yeye anaRopoka tu.

Wewe FAIZA kwa kuwa hukubaliani ka Ben Kapotea.Naomba Onyesha alipo ka ni Chadema weka wazi.Maana unajua.Kuna wakati tuweke vyama pembeni linapokuja Suala la Uhai wa MTU.Baba mzazi unaona anavyohangaika.Wewe unaleta Fitina.Chuki.Uzandiki???? Nina shaka kama uliwahi hata Olewa Wewe. Mwanaume gani atataka MTU mwenye chuki ya wazi hivi.Mrudishe Ben Wetu.

Ko hizo pesa za misheni town ndo zilikuwa zikitumika kununulia dawa hospitalini, kutoa mikopo kwa wanafunzi, kuajiri watumishi na kupandisha madaraja watumishi siyo?
Swali zuri sana.
 
Back
Top Bottom