Kwa heshima kubwa ninakusalimu na nakupa pole kwa kazi ngumu ulionayo, Mh.Rais kuna mfanyabiashara ameifanya hii halmashauri shamba la bibi kwa miaka mingi na hakuna kiongozi aliyewahi thubutu kumdhibiti, huyu bwana ameshindikana, ana mizizi mirefu sana laikini naamini haijafika hapo Ikulu.
Huyu bwana amewachoma sindano ya ganzi viongozi wengi sana maeneo haya ndo maana hata magari yake yakikamatwa kwa kutorosha mazao bila kulipa ushuru yaani utakaelikamata utapata taabu sana na utapigiwa simu na boss wako mara moja kwamba liachiwe na utapata maonyo ya kutosha, nakuomba Mh. Rais fuatilia hili kwa namna unayojua ili halmashauri iweze kukusanya mapato yake.
Huyu bwana amewachoma sindano ya ganzi viongozi wengi sana maeneo haya ndo maana hata magari yake yakikamatwa kwa kutorosha mazao bila kulipa ushuru yaani utakaelikamata utapata taabu sana na utapigiwa simu na boss wako mara moja kwamba liachiwe na utapata maonyo ya kutosha, nakuomba Mh. Rais fuatilia hili kwa namna unayojua ili halmashauri iweze kukusanya mapato yake.