Rais Magufuli: Nuru na Mkombozi wa Watanzania

Yakuza

Senior Member
May 22, 2011
114
43
Ukweli kuhusu Umakini na Uzalendo wa Rais Magufuli:
  1. Rais JPM anapigana vita ya dhati dhidi ya rushwa na walarushwa (zero tolerance to corruption). Kazi buti na tunakuombea sana Mhe. Rais;
  2. Amefanya reforms za dhati ndani ya chama chake cha CCM bila kuangalia sura. Kuna watu ndani ya CCM walidhani CCM ina wenyewe na waliozoea njia za mkato. Watu wanaisoma namba. Chaguzi zinazoendelea ndani ya CCM ni ushahidi tosha. Hongera sana Mhe. Mwenyekiti wa CCM Taifa;
  3. Watanzania tumeanza kulipa kodi. Wafanyabiashara wengi na hata wafanyakazi hawapendi kulipa kodi inayostahili. Waliozoea kutolipa kodi wanaona maisha ni magumu. Keep it up Mr. President!
  4. Kuna ongezeko kubwa la nidhamu kazini, hususani kwenye taasisi za Umma. Huu ni msingi mkubwa wa maendeleo wa taifa lolote. Hatuna cha kukupa Watanzania Mhe. Rais;
  5. Rais Magufuli anabana matumizi kwa nguvu zake zote. Katika awamu zilizopita tulikuwa tunapiga kelele kwa sababu ya matumizi yasiyo ya lazima. Safari za Mhe. Rais zinaenda na mahesabu. Siyo kweli kwamba Mhe. Rais hapendi kusafiri kwenda Ulaya na Amerika. Predisent yuko conscious na gharama za safari huko nje. Anaona bora hiyo hela inunue madawa mahospitalini. Mhe. Rais, Mungu akuongezee maisha marefu hapa duniani;
  6. Mhe. Rais tokea ameingia Ikulu Nov 2015, amepambana na mfumko wa bei. Hata hivyo thamani ya shilingi haijatulia sana...na hii ni kwa sababu ya visababishi vingi kutoka nje ya nchi (external factors). Mhe. Rais, unajenga uchumi imara. Chapa Mwendo Baba;
  7. Nchi haiwezi kuachwa ifanye siasa kuanzia mwanzo wa uchaguzi mmoja hadi mwingine, Januari hadi Desemba. HAIWEZEKANI. Na haipo popote duniani. Lazima ifikie mahala watanzania tulijue hilo na tufanye kazi kwa ajili ya maendeleo ya taifa letu tukitanguliza uzalendo mbele;
  8. Serikali ya JPM inafanya kazi usiku na mchana. Baraza la mawaziri halilali, wakuu wa mikoa na wengine wote wapo wanakimbia. Ni kweli, kuna baadhi ya watendaji wanatia doa Serikali. Kuonesha namna Serikali ya JPM inavyofanya kazi, subiria kidogo utawasikia hao wachache;
  9. Miradi mingi ipo inaanzishwa na mingine inaendelea. Mradi kama wa Standard Gauge Rail kama utakamilika, Tanzania itapiga hatua kubwa kiuchumi. Shinkanse (bullet train) ya Japan iliaza kujengwa miaka 1956 na kukamilika miaka kumi baadae. Japan ilijenga treni hiyo kwa mkopo kutoka benki ya dunia na wahisani wengine. Shinkanse anayoijenga JPM ndiyo iliwakomboa Wajapan kutoka taifa masikini hadi taifa lenye uchumi bora duniani. Hivi Watanzania, Mungu atupe nini?
  10. Katika kipindi cha takribani miaka 2 sasa, hakika Rais JPM amefanya mambo makubwa kwa nchi yetu. Pamoja na changamoto zilizopo kwenye elimu ya msingi na sekondari, ni mtanzania yupi hafahamu kuwa ni Rais JPM ndiye kamaliza tatizo la madawati nchini?. Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni. Hongera Mhe. Rais!

HITIMISHO: Watanzania ninaomba tuweke utaifa wetu mbele. Tanzania iwe kwanza kisha mengine yafuate. Hii ya kila kukicha kubeza, kutukana na kukebehi kazi nzuri inayofanywa na Mhe. Rais wetu na Serikali yake kamwe haiwezi kutuacha salama. Wanaokosoa Serikali waikosoe kwa lugha yenye staha na ukosoaji utanguliwe na uzalendo.

Ninafahamu kuna watu watatoa matusi juu ya mtazamo wangu huu kwa sababu walitaka wawe wao. Tayari nimewasamehe wote wependao kuwatusi na kuwadharau wenzao.

Ee Mwenyezi Mungu, ninakuomba umbariki sana Mpendwa wetu Rais J. P. Magufuli na tubariki watanzania wote.

Hakika, Rais Magufuli ni Nuru na Mkombozi wa Watanzania
 
FB_IMG_1503419393021.jpg
 
Mungu mwenyewe katupa JPM.
2015 tuliona watu waliotumia nguvu za kibinadamu lakini mwisho wa siku wakaangukia PUA.
Kwasababu ni mpango wa Mungu ndio maana kila shetani akiibuka ANAFELI.
Hakuna kama Magufuli hilo hata wapinzani wanajua.
Tuendelee kuwaelimisha juu ya uzalendo kwanza kwa sababu wamepanic hawajui la kufanya wanaona kabisa jinsi wanavyopotea kwenye anga la siasa kwa sababu ya utendaji mzuri wa Rais wetu(the choosen one) kwa hiyo wanatapatapa.
Tuwaombee.
 
Chiep politics ni kuitisha press na kuleta udaku.
Udaku upi wakati hata msemaji mkuu wa serikali amekiri kwamba bombadia yetu pendwa imewekwa kizuizini?
Cha kushangaza yule mwenyekiti wa ccm musukuma anashangaa eti ndege inayodaiwa kukamatwa bado iko kiwandani! Yaani alitarajia jamaa waichukue wapeleke nyumbani?
 
Non sense
Miradi ipi hiyo????Taja hata mmoja tu uliofanikiwa zaidi ya kuliingiza taifa kwenye matatizo makubwa
Shule hazina vitabu,maabara etc
Mahospitali hayana dawa
Kodi zote zinaenda kupendezesha chato
 
Udaku upi wakati hata msemaji mkuu wa serikali amekiri kwamba bombadia yetu pendwa imewekwa kizuizini?
Cha kushangaza yule mwenyekiti wa ccm musukuma anashangaa eti ndege inayodaiwa kukamatwa bado iko kiwandani! Yaani alitarajia jamaa waichukue wapeleke nyumbani?

Bombardier...Bombardier....is it really the issue for discussion? Yes, tunadaiwa na kama Taifa tutalipa. Hivi watanzania tunaona fahari gani kunanga taifa letu na kushabekia kukamatwa kwa ndege yetu? Tunafaidi nini? Pengine hao wanaoshabekia wanadhani ni hoja ya kupandia.....Tafuteni hoja nyingine siyo hii ya Bombardier.
 
Na Tanzania imeshakuwa nchi ya uchumi wa viwanda...... hili ni la muhimu sana, sielewi kwa nini mleta uzi amesahau kulitaja.
 
Bombardier...Bombardier....is it really the issue for discussion? Yes, tunadaiwa na kama Taifa tutalipa. Hivi watanzania tunaona fahari gani kunanga taifa letu na kushabekia kukamatwa kwa ndege yetu? Tunafaidi nini? Pengine hao wanaoshabekia wanadhani ni hoja ya kupandia.....Tafuteni hoja nyingine siyo hii ya Bombardier.
Hatufaidi chochote na ndio maana tunashangaa mnavyojaribu kukwepa kulipa kwa miaka yote hiyo hadi bilioni 40 zimeongezeka kuwa 87.

Huu si mkopo, ni adhabu. Na kadiri tunavyochelewa kulipa, faini zinaongezeka. Sasa wewe mzalendo niambie ni kwa nini hamkutaka kulipa hili deni hadi walipotishia kukamata ndege yetu? Ni ubabe wa serikali ya CCM au?
 
Hatufaidi chochote na ndio maana tunashangaa mnavyojaribu kukwepa kulipa kwa miaka yote hiyo hadi bilioni 40 zimeongezeka kuwa 87.

Huu si mkopo, ni adhabu. Na kadiri tunavyochelewa kulipa, faini zinaongezeka. Sasa wewe mzalendo niambie ni kwa nini hamkutaka kulipa hili deni hadi walipotishia kukamata ndege yetu? Ni ubabe wa serikali ya CCM au?

Tanzania siyo nchi ya kwanza kudaiwa duniani na siyo mara ya kwanza kudaiwa sisi kama taifa.

Jiulize: Mbona hayo yote yametokea baada ya kuzuia makinikia yetu? Kama Taifa huru lazima tulinde mali zetu kwa nguvu zote. Hata wangekamata majengo tunayomiliki ya balozi zetu kwao wao (....), bado tutaendelea kumuunga mkono Rais wetu na tupo tayari kumpigania usiku na mchana. Enough is enough.......na hao vibaraka wao wajue dhambi ya usaliti haijwahi kumuacha mtu yeyote salama.
 
Mungu mwenyewe katupa JPM.
2015 tuliona watu waliotumia nguvu za kibinadamu lakini mwisho wa siku wakaangukia PUA.
Kwasababu ni mpango wa Mungu ndio maana kila shetani akiibuka ANAFELI.
Hakuna kama Magufuli hilo hata wapinzani wanajua.
Tuendelee kuwaelimisha juu ya uzalendo kwanza kwa sababu wamepanic hawajui la kufanya wanaona kabisa jinsi wanavyopotea kwenye anga la siasa kwa sababu ya utendaji mzuri wa Rais wetu(the choosen one) kwa hiyo wanatapatapa.
Tuwaombee.
Kumbe hata Mpango wa Mungu unausikiaga tu kasome bibilia wapi Neno linalosema kua Mungu atajitwalia viongozi Miongoni mwa mataifa

Usopotoshe weerevu kama ni Mpango wa Mungu mambo anayoyafanya ni haki? Acha Dhambi ya uongo maana waongo na waoga makazi yao ni katika ziwa liwakalo Moto wa kiberiti.

Mungu gani huyo? labda mungu huyo kiongozi aliyesema HAJARIBIWI ikiwa Yesu aliye kristo alijaribiwa sebuse yeye?

Tusiwe watu wa kushabikia tu kwa sababu ya mapenzi fulani tena kama unasali na unaamini kua mwisho upo hebu tafakari kuhusu Neno UPENDO halafu ujiulize je kwa mienendo yako ya kuona wengine wanaishi kwa kuonewa ni sawa?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom