Rais Magufuli kwa kutokwenda kuwaaga askari wetu waliouawa amenishangaza

Leo sitaki unafiki juu ya hili na naomba niwe mtetezi wa Mheshimiwa Rais Dkt. JPM juu ya lililotokea na simlazimishi yoyote kukubaliana nami.

Jamani tukumbukeni kuwa Urais ni Taasisi na siyo Magufuli kama Magufuli. Hivi inaingia akilini kweli kuwa ni Yeye ndiye aliyewaonea huruma Wanafunzi wa UDSM mwaka jana ndipo akaona awajengee Hostels zao na ambazo kiukweli zimemaliza tena kwa Kiwango kikubwa tu na ratiba yake ya uzinduzi ilishapangwa muda mrefu huku maandalizi yote ya Kiitifaki yakiwa yamekamilika halafu ifike kweli siku ya kuyazindua asiwepo?

Pili tusisahau pia kuwa ujenzi ule wa zile Hostels ni ' turufu ' kubwa sana ya Mheshimiwa Rais, Serikali yake na hata Chama chake cha CCM hasa ukizingatia kuwa aliowajengea ni ' Intellectuals ' wa baadae wa nchi na ambao pengine hata kimsingi wanaweza kuwa ' Mabalozi ' wake wazuri tu huko ' Makwao ' katika kumwombea ' Kura ' za kurudi awamu yake ya pili na ya mwisho ya Uongozi au Utawala wake.

Tatu tusishau kuwa msiba wa hawa Askari wetu umetokea ghafla tu juzi tena usiku kitu ambacho nina uhakika wa ' Kiprotokali ' kuwa tayari ratiba zote za Rais za kuwepo leo pale katika ' Uzinduzi ' wa zile Hostels zilikuwa zimepangwa kiasi kwamba ingekuwa ni ngumu mno kuzi ' adjust ' accordingly ili tu nae aweze ' kuhudhuria ' mazishi ya Askari wetu kutokana na ' timing ' na ' mazingira ' yake.

Hata hivyo kwenda kwa Waziri husika wa Wizara kuhudhuria hapo mazishini siyo jambo baya sana hasa ukizingatia kuwa uwepo wa Waziri Mwigulu Nchemba pale ni ' uwakilishi ' mzuri tu wa Mheshimiwa Rais wa JMT Dkt. Magufuli na huwezi jua anaweza Rais kama Rais asiwepo pale ILA ' rambi rambi ' zake za hali na mali zikawakilishwa vizuri sana kwa ' Wafiwa ' namaanisha wana Familia na kisiharibike kitu. Naamini kabisa wale wenye angalau a,b,c's za Protocols watakuwa wamenielewa vizuri sana.

Ukishakuwa katika Taasisi ya Urais ni lazima pia ujue kucheza na public psychology lakini pia mjue jinsi gani mtaweza kumsaidia Bosi wenu ambaye ni Rais ili aweze kuzichanga vizuri ' Karata ' zake kusudi azidi kuleta imani kwa Wananchi hasa wale wenye shida na mahitaji ya lazima hivyo hapa ndipo ile ' Principle ' ya Kiuchumi ya ' Opportunity Cost ' ndipo hutumika hasa kwamba Rais asiende katika ' Uzinduzi ' wa Hostels ambazo zitawafaidisha Wasomi wengi na kumfanya azidi kukubalika na wengi na aende ' Mazikoni ' tu kwa Askari nane ( 8 ) ambao Vifo vyao vimeshaleta ' taharuki ' katika Jamii na kuleta ' chuki ' dhidi ya Serikali yake. Hapa ' obvious ' Mtu anayejua ' kucheza ' vizuri na Siasa ataamua atume tu ' mwakilishi ' katika maziko ya Askari ila yeye ataenda kuzindua Hostels ili azidi kujiaminisha kwa Wasomi ambao ni wengi kuliko hata hao Askari nane ( 8 ) waliofariki.

Urais ni zaidi ya Magufuli jamani na si vibaya sasa tukaanza kujifunza maana hasa ya Taasisi ya Urais na dhana nzima ya Protokali hasa kwa Viongozi wakubwa wa mfano wake kuliko kuja tu ' mitandaoni ' kulalamika na kulaumu wakati kumbe hata bado hatujajiridhisha vizuri kwa mambo mengine.

Yangu ni hayo tu Mkuu.
Siungi mkono hoja yako imekaa kichama na kisiasa zaidi all in all acha siku ziende Mungu wa Israel yupo.
 
Nashukuru Mungu Sikumchagua, niko chini ya utawala wake kwasababu ya wachumiatumbo/timu bao la mkono fulani, mambumbumbu flani, wajingawajinga flani, na lundo la wakulima na wafugaji vijijini na porini.
 
Leo ndiyo wale askari polisi 8 waliowawa kule Pwani wameagwa pale police barracks

Askari wanane kufa kwa kupigwa risasi na watu ambao ni majambazi/magaidi ni msiba wa kitafa..

Hivi mh Rais uliona taabu gani kwenda kushirikiana na askari wako katika kuwaaga wale askari.

Mh Rais uzidunzi wa hostel ni mhimu kuliko kuwaaga askari wako!

Kweli kabisa Mwigulu afike wew usifike? hilo suala la hostel kwa nin hukunuachia RC Makonda na waziri LUKUVI au ukahailisha kama uliona lazma uwepo

Mh. Rai umenishangaza sana...!
Ni hoja nzito lakini Raisi haendi kila mahali na kuna watu wa kupima hali ya mambo kabla ya Raisi kwenda.Tusimlaumu moja kwa moja mengine tuyaache.
 
Mbona wewe hujaenda kuwaaga upo kwenye keyboards unalia lia au ulidhani kuna kadi ya mwaliko. Jana JPM ametuma salamu za rambirambi na leo amewakilishwa na Waziri wa Wizara Husika hii inafahamika kama Delegations of Power.
Kwenda zako nawe derigation ndio nini
 
Kwani kipindi cha kampeni naomba kura nilisema nitaleta Majambazi Majambazi ayajaletwa na CCM unakumbuka Bukoba yeye akuleta tetemeko
 
Leo ndiyo wale askari polisi 8 waliowawa kule Pwani wameagwa pale police barracks

Askari wanane kufa kwa kupigwa risasi na watu ambao ni majambazi/magaidi ni msiba wa kitafa..

Hivi mh Rais uliona taabu gani kwenda kushirikiana na askari wako katika kuwaaga wale askari.

Mh Rais uzidunzi wa hostel ni mhimu kuliko kuwaaga askari wako!

Kweli kabisa Mwigulu afike wew usifike? hilo suala la hostel kwa nin hukunuachia RC Makonda na waziri LUKUVI au ukahailisha kama uliona lazma uwepo

Mh. Rai umenishangaza sana...!

Matukio kama haya hayana kiki, na hasa ukizingatia tetemeko kwa kagera aliharibu ndio kabisaaa.
Hang on a minute, labda kasahau anadhani ye no Waziri wa Ardhi na makazi nini, mana alishakuwa huko ati.
 
acheni upotoshaji na uchochezi rais hafanyi mambo kwa ghafla ghafla. ratiba ya kuzindua hosteli ilishapangwa. waziri alikuwepo pale na viongozi wengine. jamani sio kila kitu kipo kwenye level yetu ya kukosoa.
 
Hivi alikuwepo Mwakilishi yeyote wa vyama vya upinzani pale angalau nimeona serikali imewakilishwa na Mwigulu na haohao CCM walitoa hata pole Ijumaa kupitia kwa Polepole ila sijasikia upinzani wakitoa pole kwa tukio hili! only wanaharakati wamelaani this event au upinzani haliwahusu!
Mkuu hukumsikia lema akilaani kitendo cha askari wetu kuuwawa au masikio upande wa upinzani hayasikii?
 
Mkuu hukumsikia lema akilaani kitendo cha askari wetu kuuwawa au masikio upande wa upinzani hayasikii?
Nadhani Lema alilaani as an individual parliamentarian,nilidhani ingefaa sana chama kikubwa kama Chadema ku condemn tukio hili hadharani hata kupitia idara yao ya habari hii ingeonyesha utashi kamili wa kisiasa kwenye suala hili la kitaifa!
 
Mbona wewe hujaenda kuwaaga upo kwenye keyboards unalia lia au ulidhani kuna kadi ya mwaliko. Jana JPM ametuma salamu za rambirambi na leo amewakilishwa na Waziri wa Wizara Husika hii inafahamika kama Delegations of Power.

unazungumzia deligation of power wakati ni askari wetu na yy ndiyo amiri jeshi mkuu, kama ni swala la deligation of power angewaachia kina bashite na mh. lukuvi wakazindue hosteli. Binafsi nimemshangaa sana magu.
 
Ni hoja nzito lakini Raisi haendi kila mahali na kuna watu wa kupima hali ya mambo kabla ya Raisi kwenda.Tusimlaumu moja kwa moja mengine tuyaache.
hivi makamu wa rais alienda? waziri mkuu je? waziri wa ulinzi? CDF? mda mwingine mtumiage na akili, haya mambo ya usalama yanawenyewe acheni kudandia hovyo.
 
Nashukuru Mungu Sikumchagua, niko chini ya utawala wake kwasababu ya wachumiatumbo/timu bao la mkono fulani, mambumbumbu flani, wajingawajinga flani, na lundo la wakulima na wafugaji vijijini na porini.
Mkuu wa kikundi cha Uchakachuaji cha CCM kwa kushirikiana na Tume ya Uchaguzi ndiyo wa kulaumiwa kwani bila wizi wa kura leo hii Wasukuma wawili wasingekuwa ikulu wakiwasumbua watanzania na vyeti feki.
 
hivi makamu wa rais alienda? waziri mkuu je? waziri wa ulinzi? CDF? mda mwingine mtumiage na akili, haya mambo ya usalama yanawenyewe acheni kudandia hovyo.
Amiri jeshi mkuu ni Rais ndiyo alipaswa awepo pale hao wengine ni muhimu pia lakini Rais kwenda kufungua jengo na kudharau msiba ni Aibu kubwa na kama unaulizia makamu wa Rais kwa nini yeye asingeenda kufungua hostel kisha magufuli aende kuwaaga marehemu? Mungu hapendi na Bashite hizo kafara zake zinaenda kumuumbua mda si mrefu licha ya kujivunia utitiri wa Waganga wa kienyeji.
 
Back
Top Bottom