Return Of Undertaker
JF-Expert Member
- Jun 12, 2012
- 4,572
- 26,868
Rais Magufuli amehoji hivi...
Je, nikiondoka leo reli itajengwa?
Je nikiondoka leo ndege zitanunuliwa?
Je nikiondoka leo vituo hivi vya Afya vitajengwa?
Mbona havikujengwa huko nyuma?Niondoke niwaache hawa watu?
Julius Kambarage Nyerere,nae hakufanya chochote?
1.Huduma za Afya bure kwa kila Raia
2.Elimu bure kuanzia msingi mpaka Chuo Kikuu,mbali na kutogharamia elimu wanafunzi walipewa Viatu,madaftari,Kalamu/Biki pamoja na Uji.
3.Vikajengwa viwanja vya michezo kila Mkoa
4.Vikajengwa Viwanda Karibu kila Mkoa (Nyuzi-Tabora,Nyama-Shinyanga,ZZK-Mbeya,Magunia-Iringa,Ngozi-Mwanza,Matairi-Arusha,Viatu-Dsm n.k.
5.Shirika la ndege likafikisha ndege 14
6.Huduma za Benki (NBC)zikatawanywa mpaka Vijijini.
7.Akajenga Vyuo vya kati na vya ufundi kila Mkoa.
8.SIDO zikajengwa kila Mkoa
9.Mashamba ya mifugo yakaanzishwa karibu kila Mkoa.
10.Wanafunzi wa Sekondari na Chuo Kikuu walilipiwa mpaka nauli za Treni ama
Mabasi na Serikali.
11.Barabara za ndani ya mikoa zilijengwa na watanzania wenyewe wakiongozwa na majeshi yetu.
12. Hotel kila mkoa
Haya ni kama asilimia 10 tu katika Yale aliyoyafanya Mwalimu Nyerere wakati akiwa Madarakani.
========
Kwa hisani ya MwanaHalisi Online:
RAIS John Magufuli amewataka Watanzania kuwaombea mawaziri, akisema kwamba wanafanya kazi kwa mateso makubwa.
Rais Magufuli ametoa wito huo leo tarehe 5 Oktoba 2019, akizungumza na wananchi kwenye ziara yake mkoani Songwe.
Rais Magufuli ameeleza kuwa, katika uongozi wake mawaziri hawafaidiki kiasi kwamba watu wanawaonea huruma.
Mkuu huyo wa nchi amesema, sio kwamba hawapendi mawaziri wake bali analazimika kufanya hivyo. Na kuwa, mawaziri wake hawana uhakika na kesho yao, kama wataendelea kuwa mawaziri.
“Unajiuliza vituo hivi (vya afya) 352 vimekamilika kujengwa, tumeokoa roho za watanzania wangapi masikini? Kweli niondoke niwaache hawa kwa sababu tu ya unafiki wangu, kwamba natakiwa niondoke nimechoka?
Hapo ndipo ninapopata nguvu ya kusema lazima niendelee kufanya kazi, na ndio maana ninawaomba sana wana Songwe na wenzangu muendelee kuniombea na kuwaambea viongozi wenzangu mawaziri wanafanya kazi sana,” amesema Rais Magufuli.
Rais Magufuli amesema hana imani kama akiondoka madarakani, miradi anayoitekeleza, kama itafanyiwa kazi na watakaokuja baada yake.
“Lakini saa nyingine ukishajiuliza mateso ya watu ambao wanayapata, inakubidi useme lazima mimi nifanye. Ilikuwa ni lazima nifanye mimi. Ukiangalia namna ukiicha nchi, je hii miradi kweli itatekelezwa? Je, nikiondoka leo Stiglers Gorge ijtajengwa? Nikiondoka leo Standard Gauge itajengwa?” amehoji Rais Magufuli na kuongeza;
“Je, nikiondoka leo ndege zitanunuliwa? Mbona hazikununuliwa miaka yote? Hapo ndipo ninapojisikia, ninasema lazima nifanye kazi.”
Je, nikiondoka leo reli itajengwa?
Je nikiondoka leo ndege zitanunuliwa?
Je nikiondoka leo vituo hivi vya Afya vitajengwa?
Mbona havikujengwa huko nyuma?Niondoke niwaache hawa watu?
Julius Kambarage Nyerere,nae hakufanya chochote?
1.Huduma za Afya bure kwa kila Raia
2.Elimu bure kuanzia msingi mpaka Chuo Kikuu,mbali na kutogharamia elimu wanafunzi walipewa Viatu,madaftari,Kalamu/Biki pamoja na Uji.
3.Vikajengwa viwanja vya michezo kila Mkoa
4.Vikajengwa Viwanda Karibu kila Mkoa (Nyuzi-Tabora,Nyama-Shinyanga,ZZK-Mbeya,Magunia-Iringa,Ngozi-Mwanza,Matairi-Arusha,Viatu-Dsm n.k.
5.Shirika la ndege likafikisha ndege 14
6.Huduma za Benki (NBC)zikatawanywa mpaka Vijijini.
7.Akajenga Vyuo vya kati na vya ufundi kila Mkoa.
8.SIDO zikajengwa kila Mkoa
9.Mashamba ya mifugo yakaanzishwa karibu kila Mkoa.
10.Wanafunzi wa Sekondari na Chuo Kikuu walilipiwa mpaka nauli za Treni ama
Mabasi na Serikali.
11.Barabara za ndani ya mikoa zilijengwa na watanzania wenyewe wakiongozwa na majeshi yetu.
12. Hotel kila mkoa
Haya ni kama asilimia 10 tu katika Yale aliyoyafanya Mwalimu Nyerere wakati akiwa Madarakani.
========
Kwa hisani ya MwanaHalisi Online:
RAIS John Magufuli amewataka Watanzania kuwaombea mawaziri, akisema kwamba wanafanya kazi kwa mateso makubwa.
Rais Magufuli ametoa wito huo leo tarehe 5 Oktoba 2019, akizungumza na wananchi kwenye ziara yake mkoani Songwe.
Rais Magufuli ameeleza kuwa, katika uongozi wake mawaziri hawafaidiki kiasi kwamba watu wanawaonea huruma.
Mkuu huyo wa nchi amesema, sio kwamba hawapendi mawaziri wake bali analazimika kufanya hivyo. Na kuwa, mawaziri wake hawana uhakika na kesho yao, kama wataendelea kuwa mawaziri.
Wakati huo huo, Rais Magufuli amesema hawezi akaondoka madarakani huku akiwaacha Watanzania hawana maendeleo.“Katika kipindi ambacho mawaziri hawakufaidika ni wakati wangu. Kwanza, hata wanapolala hajui hata kama kesho ataamka akiwa waziri. Najua watu wanawaonea huruma, lakini lazima nifanye hivyo. Sio kwamba siwapendi, wanafanya kazi kwa mateso makubwa na wao muwaombee sana,” amesema Rais Magufuli.
“Unajiuliza vituo hivi (vya afya) 352 vimekamilika kujengwa, tumeokoa roho za watanzania wangapi masikini? Kweli niondoke niwaache hawa kwa sababu tu ya unafiki wangu, kwamba natakiwa niondoke nimechoka?
Hapo ndipo ninapopata nguvu ya kusema lazima niendelee kufanya kazi, na ndio maana ninawaomba sana wana Songwe na wenzangu muendelee kuniombea na kuwaambea viongozi wenzangu mawaziri wanafanya kazi sana,” amesema Rais Magufuli.
Rais Magufuli amesema hana imani kama akiondoka madarakani, miradi anayoitekeleza, kama itafanyiwa kazi na watakaokuja baada yake.
“Lakini saa nyingine ukishajiuliza mateso ya watu ambao wanayapata, inakubidi useme lazima mimi nifanye. Ilikuwa ni lazima nifanye mimi. Ukiangalia namna ukiicha nchi, je hii miradi kweli itatekelezwa? Je, nikiondoka leo Stiglers Gorge ijtajengwa? Nikiondoka leo Standard Gauge itajengwa?” amehoji Rais Magufuli na kuongeza;
“Je, nikiondoka leo ndege zitanunuliwa? Mbona hazikununuliwa miaka yote? Hapo ndipo ninapojisikia, ninasema lazima nifanye kazi.”