Lyaule Kitundu
JF-Expert Member
- May 25, 2011
- 758
- 1,024
Ndugu nakushutumu wewe ndio mwizi wa kukuwangu, then unaniambia kuwa nilete kwako wewe wewe kesi ya kuibiwa kuku wangu?Kilichoongelewa ni kuzushia vyombo vya ulinzi uongo kwamba ndio wanaoteka na kuua watu bila ya kuwa na ushahidi! Kuzushia vyombo vya usalama uongo!
Msibadilishe - kuzushia vyombo vya ulinzi wetu uongo ndicho kinacho katazwa na mkiendelea mtapata cha mtema kuni.
Kuumizwa na waliotekwa na waliopotea na waliokufa hiyo rukhsa, hakuna aliyekukataza. Sote tunaumizwa na hilo - lakini kusingizia mtu au chombo chochote bila ya kuwa na ushahidi, na pia ushahidi huo bila ya kuuwasilisha kwenye vyombo vinavyo husika, basi ukikamatwa usimlaumu mtu. Umetaka mwenyewe. Muwe wepesi wa kuelewa kilichosemwa.
Yani wananchi wanalalamika vyombo vya dola kuhusika na utekaji then wananchi hao hao wanatakiwa kupeleka ushahidi kwa vyombo hivyo hivyo vinavyoshutumiwa kwa utekaji. Hii equation inakuingia akilini kweli unaweza kuisolve bila kutoa character yoyote hapo?
Sent using Jamii Forums mobile app