Wakati anafurahia kukaa chamwino, akumbuke kuwa maelfu ya wafanyakazi wa ngazi ya chini watakaohamia DODOMA hawatakuwa na pa kuishi.
Kwa kuwa Tangazo lake limeongeza ghafla bei za viwanja na nyumba za kupanga, ingekuwa vema akawawezesha wafanyakazi wanaoenda DODOMA kwa mambo mawili, mosi kwa kuhakikisha wizara ya ardhi, inawaauzia viwanja vya gharama nafuu kwenye maeneo yaliyotengwa na yaliyopimwa, ili waanze ujenzi mara moja. Serikali iwadhamini kupata mikopo ya gharama nafuu,kama sehemu ya relocation allowances zao.
Yakifanyika hayo kwenda DODOMA kutagombaniwa na kila public servant, kwani itakuwa ticket ya neema. Itamsaidia Zaidi magufuli kufanikiwa kwa mgongo wa wafanyakazi watakaokuwa motivated.
Asiwatazame mawaziri na makatibu wakuu, hawa wengi wana uwezo, na idadi yao ndogo sana kuleta impact, atazame wafanyakazi wa kada za kati kurudi chini. Kama hawa wakijengewa uwezo mzuri wa kuhama. Sera yake itafanikiwa sana, kwa gharama nafuu na ufanisi wa hali ya juu.