Rais Magufuli amteuwa Prof. Ignas Rubaratuka kuwa mwenyekiti wa bodi ya mamlaka ya bandari (TPA)

R.B

JF-Expert Member
May 10, 2012
6,296
2,575

Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano imemtangza Mwenyekiti Mpya wa atakayesimamia Bodi ya bandari ya Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) katika kipindi cha miaka mitatu.

Akitangaza mbele ya wanahabari mapema leo Juni 15, Katibu Mkuu (Uchukuzi) wa Wizara hiyo, Dkt. Leonard Chamuriho ameeleza kuwa, kwa mujibu wa sharia namba 17 ya Mwaka 2004 ya Mamlaka ya Usimamizi wa bandari Tanzania (TPA), kifungu 6 (2) (A)

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ndie mwenye mamlaka ya kuteua Mwenyekiti wa Bodi, ambapo amemteua Profesa Ignas Aloys Rubaratuka kuwa Mwenyekiti wa Bodi hiyo ya TPA kwa muda wa kipindi cha miaka 3.

Prof. Rubaratuka ni Mhadhiri Mwandamizi wa chuo kikuu cha Dar es Salaam.

Aidha, Waziri Mwenye dhamana ya sekta ya uchukuzi, Mh. Prof. Makame Mbarawa (MB) kwa mamlaka aliyopewa amewateua wajumbe wa bodi hiyo ya TPA kuanzia jana Juni 14.2016 kwa kipindi cha miaka mitatu (3).

Wajumbe wapya wa Bodi ya TPA:

Wajumbe hao ni pamoja na Jayne Kezir Nyimbo (Mtaalam wa Rasilimali watu na Meneja Uendeshaji, CARTECK,Tanznaia), Dkt. Francis Michael (Mhadhiri Mwandamizi Chuo kikuu cha Dar es Salaam), Bw. Azizi Massala Kilonge (Mkurugenzi Mtendaji na Mshahuri mwelekezi, AMAK Consulting).

Wengine ni Bwana Masanja Kungu Kadogosa (Kaimu Mkurugenzi Mkuu Kampuni ya Reli Tanzania-TRL), Jabiri Kuwe Bakari (Mtendaji Mkuu, Wakala wa Serikali Mtandao, Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala bora), Eng. Deusdedit Conatus Vitali Kakoko (Meneja Miradi, TANROADS) na Bwana Jaffeer Salim Machano (Mkurugenzi wa Mipango na Huduma Tanzania Investment Bank).

DSC_7681.jpg

Katibu Mkuu (Uchukuzi) Dkt. Leonard Chamuriho akitangaza wajumbe wajumbe na Mwenyekiti mpya wa Bodi hiyo ya TPA
 
Hivi wajumbe wa hii bodi iliyopita wamechukuliwa hatua gani?
Mana Tuliaa nae alikuwa mmoja wapo.
 
Ile iliyovunjwa kwa ukiukwaji taratibu za bandari ,mmoja wa wajumbe alikuwa dk tulia,naibu spika
 
Naona Wahadhiri UDSM wanazidi kuula..
Sijui kama kila mtu anaona nachokiona.. kuna mkakati wa makusudi kuhamishia 'Power base' Kanda ya Ziwa.. Walianza kwa kusema Mwanza inaongoza kwa mikoa masikini zaidi TZ..
 
Hongera zao na wakafanye kazi kitaaluma maana ni wasomi...hongera pia Rais wetu mpendwa KPM kwa uteuzi makini.
 
Mimi nawatakia kila la kheli .
Zidi natarajia kuona ufanisi, maana naona ni wasomi kwelikweli hao walioteuliwa.
Sio sisi kuwa na wsomo ila utendaji wao unakuwa hadi unajihoji ni yeye kweli au siyo ni jina linafanana na lake?

Ila ukileta mchina hata hajui darasa lilipo anafanya maajabu kwa wiki moja kwa kutekeleza kazi vizuri mf. nasikia wachina wengi wanaoletwa Afrika ni wakosefu [wafungwa] kule kwao. Badala ya kulishwa na serikali wanaletwa kufanya kazi huku Afrika [sina uhakika sana nilisikia simulizi ya jamaa mmoja huku ugaibhuni, akisema]

Sasa, basi wafanye kazi na wadhihirishie umma kuwa kweli wao ni wasomi na wamtunzie Rais heshima kwa kuwaamini na kuwapatia taasisi/mamlaka nyeti kama hizo mfano Bandari=TPA.

"Mungu Ibariki Tanzania"
 
Naona Wahadhiri UDSM wanazidi kuula..
Sijui kama kila mtu anaona nachokiona.. kuna mkakati wa makusudi kuhamishia 'Power base' Kanda ya Ziwa.. Walianza kwa kusema Mwanza inaongoza kwa mikoa masikini zaidi TZ..
Hao wa UDSM wote makada
 
Teuzi zote za sasa zimeegemea sehemu moja ya Nchi,kanda ya ziwa kuna sehemu naona hakuna wataalamu wanaoweza kuongoza ktk nyadhifa hizo! Kama mambo yenyewe ndiyo hayo bora kuwe ma mpokezano wa kila kanda kwenyr uongozi wa nchj
 
Teuzi zote za sasa zimeegemea sehemu moja ya Nchi,kanda ya ziwa kuna sehemu naona hakuna wataalamu wanaoweza kuongoza ktk nyadhifa hizo! Kama mambo yenyewe ndiyo hayo bora kuwe ma mpokezano wa kila kanda kwenyr uongozi wa nchj
Teuzi zote za sasa zimeegemea sehemu moja ya Nchi,kanda ya ziwa kuna sehemu naona hakuna wataalamu wanaoweza kuongoza ktk nyadhifa hizo! Kama mambo yenyewe ndiyo hayo bora kuwe ma mpokezano wa kila kanda kwenyr uongozi wa nchj
Labda ndiyo kuna wasomi na watu wenye uwezo zaidi kuliko maeneno mengine ya nchi hii
 
Back
Top Bottom