Rais Magufuli aipandisha hadhi Ikulu

Ashura9

JF-Expert Member
Oct 21, 2012
739
484
Magufuli arejesha Ikulu kuwa mahala patakatifu

24th January 2016




Raismagufuli.jpg

Rais wa John Magufuli


Mwaka mmoja uliopita ungeweza kuamini kuwa Mtanzania aliyetwaa tuzo ya Mwanasoka Bora wa Afrika kwa Wachezaji wa Ndani hatoitwa Ikulu na Rais Jakaya Kikwete kwa ajili ya kupongezwa?

Jibu la swali hilo ni hapana; hasa ukizingatia kuwa wapo wanamichezo na wasanii waliotwaa tuzo ndogo zaidi lakini wakaalikwa katika ofisi kuu hiyo ya nchi kwa ajili ya kukutana na Rais.

Mwaka mmoja baadaye, Rais wa Tano John Magufuli amejikita katika kushughulikia matatizo halisi ya Watanzania na kufunga milango kwa wageni wasio na shughuli muhimu kwenda Ikulu, gazeti hili limebaini.

Ikulu pia imekomesha tabia iliyokuwa imezoeleka ya wageni kujazana kila siku sehemu ya mapokezi kwa ajili ya kwenda kuomba misaada mbalimbali kwa Rais, kama ilivyokuwa imezoeleka kwenye serikali iliyopita.

Gazeti hili lilifanikiwa kufika Ikulu sehemu ya mapokezi na kukuta viti vikiwa vitupu tofauti na awamu iliyopita ambapo mapokezi ya Ikulu ilikuwa ikitaka kufanana na eneo la shughuli hiyo katika hospitali yoyote ya mkoa nchini.

Viti vilijaa hadi kufikia hatua ya wageni hao kukaa kwa kupokezana.

Wakati leo ametimiza siku ya 80 tangu alipoapishwa Novemba 5, mwaka jana, Rais Magufuli amekutana na kufanya mazungumzo na viongozi wachache muhimu, hali inayoashiria kuwa Ikulu sasa ni mahala patakatifu, kama ambavyo Baba wa Taifa, Hayati Julius Nyerere alipata kuusia katika moja ya hotuba zake za kukumbukwa, ya Mei Mosi 1995 jijini Mbeya.

Miongoni mwa viongozi ambao Rais Magufuli amekutana nao Ikulu tangu aingie madarakani ni Sheikh Mkuu, Aboubakar Zuberi, Rais wa awamu ya Pili, Alhaji Ali Hassan Mwinyi, Rais wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa na Kikwete.

Rais Magufuli pia alikutana na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Seif Sharif Hamad, Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein na Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar, Balozi Seif Idd kuzungumzia hali ya mkwamo wa kisiasa inayoendelea visiwani humo.

Wengine aliokutana nao kwa mazungumzo Ikulu hivi karibuni ni aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Katiba Mpya, Jaji Joseph Warioba, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi CCM Taifa, Abdalah Bulembo, Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Profesa Musa Jumma Assad na aliyekuwa Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba.

Kutoalikwa Ikulu kwa Samatta ndiko kumedhihirisha kwamba sasa milango ya kwenda kumuona Rais haiko wazi sana kama ilivyokuwa kwenye awamu hiyo ya nne.

Rais Magufuli pia amepokea hati za mabalozi mbali mbali wanaoiwakilisha nchi zao ambao walifika Ikulu kwa ajili ya kujitambulisha.

Januari 7, Samatta alinyakua tuzo hiyo ya pili kwa ubora kwa wachezaji wa Afrika, baada ya Mchezaji Bora wa Afrika ambayo ilikwenda kwa Pierre-Emerick Aubameyang wa Gabon.
Tuzo hizo hutolewa na Shirikisho la Soka Afrika (CAF).

Kama Samatta angetwaa tuzo hiyo mwaka mmoja uliopita kwa mfano, isingekuwa rahisi kupita wiki moja bila Mbwana Sammatta kualikwa na Rais Ikulu.

Rais mstaafu Kikwete, ambaye ni mwenyekiti wa CCM, ameshakutana na Samatta kwenye Ofisi Ndogo za chama hicho, Lumumba jijini.

Baada ya ushindi wake, Samatta alipokewa na Waziri wa Habari, Utamaduni, Michezo na Wasanii, Nape Nnauye, ambaye alimpa gari lake atumie kwa muda pia.

Miongoni mwa wageni waalikwa wa mara kwa mara wa Kikwete Ikulu ni pamoja na mwanamuziki maarufu wa zamani Ray C ambaye Desemba 10, 2012 alikwenda kumshukuru kwa kumsaidia tiba ya matumizi ya madawa ya kulevya.

Habari ambazo Nipashe inazo, Ray C bado anaendelea kupata tiba ya kuacha dawa za kulevya katika Hospitali ya Mwananyamala jijini Dar es Salaam.

Diamond Platnumz amewahi kualikwa mara kadhaa Ikulu, hata pale alipotwaa tuzo ndogo ambazo zilikabidhiwa kwenye hata klabu za usiku nje ya nchi.

Timu ya Azam imewahi kualikwa Ikulu baada ya kutwaa kwa mara ya kwanza Kombe la Kagame la Afrika Mashariki na Kati, taji ambalo Simba na Yanga zimelichukua jumla ya mara 11 katika historia.

Wachambuzi wa mambo walisema hali hiyo inadhihirisha kwamba Rais Magufuli amejikita katika kushughulikia matatizo ya msingi ya nchi, hasa vita dhidi ya ufisadi wa rasilimali za taifa, upatikaji wa huduma za jamii na uimarishaji wa miundombinu.

Dalili kwamba Ikulu sasa ni mahali patakatifu ilianza kujidhihirisha wakati wa kuapishwa kwa Baraza la Mawaziri mwishoni mwa mwaka jana.

Mawaziri hao waliapishwa bila mbwe mbwe wala shamra shamra kama ilivyozoeleka kwenye awamu ya nne, wahusika wakifika Ikulu bila kuambatana na utitiri wa ndugu na jamaa ambao chini ya Kikwete waliwalaki kwa maua na mashada baada ya kuapishwa.

Kwenye awamu ya nne, baadhi ya wateule walikuwa wakienda kuapishwa Ikulu na wake au waume zao, watoto, ndugu, majirani na jamaa zao na kupata fursa ya kupiga picha na Rais mara baada ya zoezi la kuapishwa.

Utaratibu huo umefutika baada ya Rais Magufuli kuonekana kujikita kwenye masuala ya msingi kama kupanga safu ya uongozi wake kwa kuwafuta kazi watendaji ambao anaona hawawezi kwenda na kasi yake.

Aidha, punde baada ya kuingia Ikulu Novemba 5, mwaka jana Rais Magufuli alifuta kitengo cha mapokezi ya wageni kwenye lango kuu la Ikulu na kuagiza watendaji wa serikali katika ngazi zote kutatua kero za wananchi mahala walipo ili kuwapunguzia usumbufu.

Kitengo cha Lishe kilichokuwepo Ikulu wakati wa serikali ya awamu ya nne kilivunjwa na watendaji wake kurudishwa kwenye Wizara mama walizotoka.

SOURCE: NIPASHE JUMAPILI
 
Ni jambo la maana sana ikiwa wanajamii wanatambua kuwa Ikulu ni ofisi kubwa kuliko zote nchini. Huwezi ukawa unazungukwa na watu kirahisi tu halafu uwepo wa watu hao ushindwe kuleta negative influence katika utendaji wako wa kazi. Marais wote ambao ni rahisi kwao kukaribiana na watu, urafiki wao hutumiwa vibaya na wapambe. Na marais wenye hulka hizo wake zao wana sifa ya kuanzisha mifuko mbalimbali, kupitia ukaribu wa first lady watu wenye nia chafu wanapata mwanya wa kumkaribia rais. Simuoni Mama watoto wa rais wetu akiwa na hamu ya kuanzisha biashara au mfuko fulani wenye kufadhiliwa na mataifa makubwa. Rais alisema tumuombee, na alikuwa sahihi kwani mafisadi wanazo njia nyingi za kuwaingia marais popote pale duniani. Ikulu ni mahali patakatifu, lakini utakatifu wa sehemu hiyo huanza na uwezo wa rais kuikwepa mitego yote ya wafanya biashara.
 
Rais kukutana na wasanii wanamichezo sio jambo baya hata kidogo. Labda Itakuwa tabia na malezi aliyopitia yanamfanya awe hivyo lakini ndo kwanza siku themanini na kitu tangu kuapishwa.
 
Magufuli arejesha Ikulu kuwa mahala patakatifu

24th January 2016




Raismagufuli.jpg

Rais wa John Magufuli


Mwaka mmoja uliopita ungeweza kuamini kuwa Mtanzania aliyetwaa tuzo ya Mwanasoka Bora wa Afrika kwa Wachezaji wa Ndani hatoitwa Ikulu na Rais Jakaya Kikwete kwa ajili ya kupongezwa?

Jibu la swali hilo ni hapana; hasa ukizingatia kuwa wapo wanamichezo na wasanii waliotwaa tuzo ndogo zaidi lakini wakaalikwa katika ofisi kuu hiyo ya nchi kwa ajili ya kukutana na Rais.

Mwaka mmoja baadaye, Rais wa Tano John Magufuli amejikita katika kushughulikia matatizo halisi ya Watanzania na kufunga milango kwa wageni wasio na shughuli muhimu kwenda Ikulu, gazeti hili limebaini.

Ikulu pia imekomesha tabia iliyokuwa imezoeleka ya wageni kujazana kila siku sehemu ya mapokezi kwa ajili ya kwenda kuomba misaada mbalimbali kwa Rais, kama ilivyokuwa imezoeleka kwenye serikali iliyopita.

Gazeti hili lilifanikiwa kufika Ikulu sehemu ya mapokezi na kukuta viti vikiwa vitupu tofauti na awamu iliyopita ambapo mapokezi ya Ikulu ilikuwa ikitaka kufanana na eneo la shughuli hiyo katika hospitali yoyote ya mkoa nchini.

Viti vilijaa hadi kufikia hatua ya wageni hao kukaa kwa kupokezana.

Wakati leo ametimiza siku ya 80 tangu alipoapishwa Novemba 5, mwaka jana, Rais Magufuli amekutana na kufanya mazungumzo na viongozi wachache muhimu, hali inayoashiria kuwa Ikulu sasa ni mahala patakatifu, kama ambavyo Baba wa Taifa, Hayati Julius Nyerere alipata kuusia katika moja ya hotuba zake za kukumbukwa, ya Mei Mosi 1995 jijini Mbeya.

Miongoni mwa viongozi ambao Rais Magufuli amekutana nao Ikulu tangu aingie madarakani ni Sheikh Mkuu, Aboubakar Zuberi, Rais wa awamu ya Pili, Alhaji Ali Hassan Mwinyi, Rais wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa na Kikwete.

Rais Magufuli pia alikutana na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Seif Sharif Hamad, Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein na Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar, Balozi Seif Idd kuzungumzia hali ya mkwamo wa kisiasa inayoendelea visiwani humo.

Wengine aliokutana nao kwa mazungumzo Ikulu hivi karibuni ni aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Katiba Mpya, Jaji Joseph Warioba, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi CCM Taifa, Abdalah Bulembo, Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Profesa Musa Jumma Assad na aliyekuwa Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba.

Kutoalikwa Ikulu kwa Samatta ndiko kumedhihirisha kwamba sasa milango ya kwenda kumuona Rais haiko wazi sana kama ilivyokuwa kwenye awamu hiyo ya nne.

Rais Magufuli pia amepokea hati za mabalozi mbali mbali wanaoiwakilisha nchi zao ambao walifika Ikulu kwa ajili ya kujitambulisha.

Januari 7, Samatta alinyakua tuzo hiyo ya pili kwa ubora kwa wachezaji wa Afrika, baada ya Mchezaji Bora wa Afrika ambayo ilikwenda kwa Pierre-Emerick Aubameyang wa Gabon.
Tuzo hizo hutolewa na Shirikisho la Soka Afrika (CAF).

Kama Samatta angetwaa tuzo hiyo mwaka mmoja uliopita kwa mfano, isingekuwa rahisi kupita wiki moja bila Mbwana Sammatta kualikwa na Rais Ikulu.

Rais mstaafu Kikwete, ambaye ni mwenyekiti wa CCM, ameshakutana na Samatta kwenye Ofisi Ndogo za chama hicho, Lumumba jijini.

Baada ya ushindi wake, Samatta alipokewa na Waziri wa Habari, Utamaduni, Michezo na Wasanii, Nape Nnauye, ambaye alimpa gari lake atumie kwa muda pia.

Miongoni mwa wageni waalikwa wa mara kwa mara wa Kikwete Ikulu ni pamoja na mwanamuziki maarufu wa zamani Ray C ambaye Desemba 10, 2012 alikwenda kumshukuru kwa kumsaidia tiba ya matumizi ya madawa ya kulevya.

Habari ambazo Nipashe inazo, Ray C bado anaendelea kupata tiba ya kuacha dawa za kulevya katika Hospitali ya Mwananyamala jijini Dar es Salaam.

Diamond Platnumz amewahi kualikwa mara kadhaa Ikulu, hata pale alipotwaa tuzo ndogo ambazo zilikabidhiwa kwenye hata klabu za usiku nje ya nchi.

Timu ya Azam imewahi kualikwa Ikulu baada ya kutwaa kwa mara ya kwanza Kombe la Kagame la Afrika Mashariki na Kati, taji ambalo Simba na Yanga zimelichukua jumla ya mara 11 katika historia.

Wachambuzi wa mambo walisema hali hiyo inadhihirisha kwamba Rais Magufuli amejikita katika kushughulikia matatizo ya msingi ya nchi, hasa vita dhidi ya ufisadi wa rasilimali za taifa, upatikaji wa huduma za jamii na uimarishaji wa miundombinu.

Dalili kwamba Ikulu sasa ni mahali patakatifu ilianza kujidhihirisha wakati wa kuapishwa kwa Baraza la Mawaziri mwishoni mwa mwaka jana.

Mawaziri hao waliapishwa bila mbwe mbwe wala shamra shamra kama ilivyozoeleka kwenye awamu ya nne, wahusika wakifika Ikulu bila kuambatana na utitiri wa ndugu na jamaa ambao chini ya Kikwete waliwalaki kwa maua na mashada baada ya kuapishwa.

Kwenye awamu ya nne, baadhi ya wateule walikuwa wakienda kuapishwa Ikulu na wake au waume zao, watoto, ndugu, majirani na jamaa zao na kupata fursa ya kupiga picha na Rais mara baada ya zoezi la kuapishwa.

Utaratibu huo umefutika baada ya Rais Magufuli kuonekana kujikita kwenye masuala ya msingi kama kupanga safu ya uongozi wake kwa kuwafuta kazi watendaji ambao anaona hawawezi kwenda na kasi yake.

Aidha, punde baada ya kuingia Ikulu Novemba 5, mwaka jana Rais Magufuli alifuta kitengo cha mapokezi ya wageni kwenye lango kuu la Ikulu na kuagiza watendaji wa serikali katika ngazi zote kutatua kero za wananchi mahala walipo ili kuwapunguzia usumbufu.

Kitengo cha Lishe kilichokuwepo Ikulu wakati wa serikali ya awamu ya nne kilivunjwa na watendaji wake kurudishwa kwenye Wizara mama walizotoka.

SOURCE: NIPASHE JUMAPILI
Habari nzuri ila imerefushwa bila sababu
 
Sijaelewa......kutokutana na Samatta ikulu ndio pamekuwa patakatifu?
 
Hivi umejiuliza kwanini hii post yako haichangiwi? Sababu watu wamechoka unafiki.
 
Magufuli arejesha Ikulu kuwa mahala patakatifu

24th January 2016




Raismagufuli.jpg

Rais wa John Magufuli


Mwaka mmoja uliopita ungeweza kuamini kuwa Mtanzania aliyetwaa tuzo ya Mwanasoka Bora wa Afrika kwa Wachezaji wa Ndani hatoitwa Ikulu na Rais Jakaya Kikwete kwa ajili ya kupongezwa?

Jibu la swali hilo ni hapana; hasa ukizingatia kuwa wapo wanamichezo na wasanii waliotwaa tuzo ndogo zaidi lakini wakaalikwa katika ofisi kuu hiyo ya nchi kwa ajili ya kukutana na Rais.

Mwaka mmoja baadaye, Rais wa Tano John Magufuli amejikita katika kushughulikia matatizo halisi ya Watanzania na kufunga milango kwa wageni wasio na shughuli muhimu kwenda Ikulu, gazeti hili limebaini.

Ikulu pia imekomesha tabia iliyokuwa imezoeleka ya wageni kujazana kila siku sehemu ya mapokezi kwa ajili ya kwenda kuomba misaada mbalimbali kwa Rais, kama ilivyokuwa imezoeleka kwenye serikali iliyopita.

Gazeti hili lilifanikiwa kufika Ikulu sehemu ya mapokezi na kukuta viti vikiwa vitupu tofauti na awamu iliyopita ambapo mapokezi ya Ikulu ilikuwa ikitaka kufanana na eneo la shughuli hiyo katika hospitali yoyote ya mkoa nchini.

Viti vilijaa hadi kufikia hatua ya wageni hao kukaa kwa kupokezana.

Wakati leo ametimiza siku ya 80 tangu alipoapishwa Novemba 5, mwaka jana, Rais Magufuli amekutana na kufanya mazungumzo na viongozi wachache muhimu, hali inayoashiria kuwa Ikulu sasa ni mahala patakatifu, kama ambavyo Baba wa Taifa, Hayati Julius Nyerere alipata kuusia katika moja ya hotuba zake za kukumbukwa, ya Mei Mosi 1995 jijini Mbeya.

Miongoni mwa viongozi ambao Rais Magufuli amekutana nao Ikulu tangu aingie madarakani ni Sheikh Mkuu, Aboubakar Zuberi, Rais wa awamu ya Pili, Alhaji Ali Hassan Mwinyi, Rais wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa na Kikwete.

Rais Magufuli pia alikutana na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Seif Sharif Hamad, Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein na Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar, Balozi Seif Idd kuzungumzia hali ya mkwamo wa kisiasa inayoendelea visiwani humo.

Wengine aliokutana nao kwa mazungumzo Ikulu hivi karibuni ni aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Katiba Mpya, Jaji Joseph Warioba, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi CCM Taifa, Abdalah Bulembo, Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Profesa Musa Jumma Assad na aliyekuwa Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba.

Kutoalikwa Ikulu kwa Samatta ndiko kumedhihirisha kwamba sasa milango ya kwenda kumuona Rais haiko wazi sana kama ilivyokuwa kwenye awamu hiyo ya nne.

Rais Magufuli pia amepokea hati za mabalozi mbali mbali wanaoiwakilisha nchi zao ambao walifika Ikulu kwa ajili ya kujitambulisha.

Januari 7, Samatta alinyakua tuzo hiyo ya pili kwa ubora kwa wachezaji wa Afrika, baada ya Mchezaji Bora wa Afrika ambayo ilikwenda kwa Pierre-Emerick Aubameyang wa Gabon.
Tuzo hizo hutolewa na Shirikisho la Soka Afrika (CAF).

Kama Samatta angetwaa tuzo hiyo mwaka mmoja uliopita kwa mfano, isingekuwa rahisi kupita wiki moja bila Mbwana Sammatta kualikwa na Rais Ikulu.

Rais mstaafu Kikwete, ambaye ni mwenyekiti wa CCM, ameshakutana na Samatta kwenye Ofisi Ndogo za chama hicho, Lumumba jijini.

Baada ya ushindi wake, Samatta alipokewa na Waziri wa Habari, Utamaduni, Michezo na Wasanii, Nape Nnauye, ambaye alimpa gari lake atumie kwa muda pia.

Miongoni mwa wageni waalikwa wa mara kwa mara wa Kikwete Ikulu ni pamoja na mwanamuziki maarufu wa zamani Ray C ambaye Desemba 10, 2012 alikwenda kumshukuru kwa kumsaidia tiba ya matumizi ya madawa ya kulevya.

Habari ambazo Nipashe inazo, Ray C bado anaendelea kupata tiba ya kuacha dawa za kulevya katika Hospitali ya Mwananyamala jijini Dar es Salaam.

Diamond Platnumz amewahi kualikwa mara kadhaa Ikulu, hata pale alipotwaa tuzo ndogo ambazo zilikabidhiwa kwenye hata klabu za usiku nje ya nchi.

Timu ya Azam imewahi kualikwa Ikulu baada ya kutwaa kwa mara ya kwanza Kombe la Kagame la Afrika Mashariki na Kati, taji ambalo Simba na Yanga zimelichukua jumla ya mara 11 katika historia.

Wachambuzi wa mambo walisema hali hiyo inadhihirisha kwamba Rais Magufuli amejikita katika kushughulikia matatizo ya msingi ya nchi, hasa vita dhidi ya ufisadi wa rasilimali za taifa, upatikaji wa huduma za jamii na uimarishaji wa miundombinu.

Dalili kwamba Ikulu sasa ni mahali patakatifu ilianza kujidhihirisha wakati wa kuapishwa kwa Baraza la Mawaziri mwishoni mwa mwaka jana.

Mawaziri hao waliapishwa bila mbwe mbwe wala shamra shamra kama ilivyozoeleka kwenye awamu ya nne, wahusika wakifika Ikulu bila kuambatana na utitiri wa ndugu na jamaa ambao chini ya Kikwete waliwalaki kwa maua na mashada baada ya kuapishwa.

Kwenye awamu ya nne, baadhi ya wateule walikuwa wakienda kuapishwa Ikulu na wake au waume zao, watoto, ndugu, majirani na jamaa zao na kupata fursa ya kupiga picha na Rais mara baada ya zoezi la kuapishwa.

Utaratibu huo umefutika baada ya Rais Magufuli kuonekana kujikita kwenye masuala ya msingi kama kupanga safu ya uongozi wake kwa kuwafuta kazi watendaji ambao anaona hawawezi kwenda na kasi yake.

Aidha, punde baada ya kuingia Ikulu Novemba 5, mwaka jana Rais Magufuli alifuta kitengo cha mapokezi ya wageni kwenye lango kuu la Ikulu na kuagiza watendaji wa serikali katika ngazi zote kutatua kero za wananchi mahala walipo ili kuwapunguzia usumbufu.

Kitengo cha Lishe kilichokuwepo Ikulu wakati wa serikali ya awamu ya nne kilivunjwa na watendaji wake kurudishwa kwenye Wizara mama walizotoka.

SOURCE: NIPASHE JUMAPILI
Hivi unaandika huu ujinga kwa manufaa ya nani?
 
panakuwaje patakatifu wakati mazombie wanatumia kila mbinu chafu kuingia madarakani !
 
Sasa kumuacha Samatta na kumkaribisha Bulembo ndio utakatifu huo? Mkuu hebu wasaidie hawa watu kuelewa, au viwavi vinawalevya?
Mkuu hayo ndio madhara ya viwavi hasa wa rangi za kijani
 
Najua kwamba nia sio mbaya,ila naomba tuwe makini na matumizi ya maneno.Kitu hakiwezi kuwa kitakatifu.Mtu ndiye anayeweza kuwa mtakatifu kutegemea uhusiano wake na Mungu wa mbinguni ulivyo.Kama anatimiza mapenzi ya Mungu,huyo ni mtakatifu.Kwa sababu hiyo Ikulu ya Magufuli sio takatifu,ila inaheshimika au ni mahali pa heshima.
Ni jambo la maana sana ikiwa wanajamii wanatambua kuwa Ikulu ni ofisi kubwa kuliko zote nchini. Huwezi ukawa unazungukwa na watu kirahisi tu halafu uwepo wa watu hao ushindwe kuleta negative influence katika utendaji wako wa kazi. Marais wote ambao ni rahisi kwao kukaribiana na watu, urafiki wao hutumiwa vibaya na wapambe. Na marais wenye hulka hizo wake zao wana sifa ya kuanzisha mifuko mbalimbali, kupitia ukaribu wa first lady watu wenye nia chafu wanapata mwanya wa kumkaribia rais. Simuoni Mama watoto wa rais wetu akiwa na hamu ya kuanzisha biashara au mfuko fulani wenye kufadhiliwa na mataifa makubwa. Rais alisema tumuombee, na alikuwa sahihi kwani mafisadi wanazo njia nyingi za kuwaingia marais popote pale duniani. Ikulu ni mahali patakatifu, lakini utakatifu wa sehemu hiyo huanza na uwezo wa rais kuikwepa mitego yote ya wafanya biashara.
 
Sijaelewa......kutokutana na Samatta ikulu ndio pamekuwa patakatifu?
Sijui utakatifu umebadilika maana !? ........Ikulu inakuwaje patakatifu !? Kuna ibada gani inafanyika Ikulu, wenye kukaa Ikulu ni watakatifu !?
Ujinga mwingine bhaana ! ......ndo maana mitume wengi siku hizi !
 
Najua kwamba nia sio mbaya,ila naomba tuwe makini na matumizi ya maneno.Kitu hakiwezi kuwa kitakatifu.Mtu ndiye anayeweza kuwa mtakatifu kutegemea uhusiano wake na Mungu wa mbinguni ulivyo.Kama anatimiza mapenzi ya Mungu,huyo ni mtakatifu.Kwa sababu hiyo Ikulu ya Magufuli sio takatifu,ila inaheshimika au ni mahali pa heshima.
Wewe unazo akili nyingi kuliko waasisi wa taifa, namaanisha mwalimu Nyerere?
 
Back
Top Bottom