Rais JPM ukipata uwenyekiti waCCM komesha rushwa kwenye kura za mapendekezo CCM

laurent Msembeyu

Senior Member
Oct 5, 2015
121
101
Mheshimiwa ukifanikiwa kupata uwenyekiti wa chama cha mapinduzi CCM tafadhari naomba ujitahidi kukomesha hii tabia ya rushwa katika kura za maoni CCM, tabia hii ni kama uwendawazimu Fulani na inaleta fedheha kubwa kwenye chama.
  • Utakuta mtu kwenye kura za maoni anapata kura nyingi kuliko kura katika uchaguzi mkuu, sasa hawa wanachama wengi katika jimbo wanatoka wapi?
  • Wanachama wanaompigia mtu mmoja kwenye kura za maoni ni wengi hadi mala tatu ya wanachama wote kwenye wilaya ambayo ina majimbo mawili hadi matatu ya uchaguzi, hebu angalia kura za mapendekezo alizopata mshindi katika jimbo la Kibakwe, Mtama na Chalinze. Wanachama kiasi hicho hawapo kwenye daftari la wanachama kwenye ofisi ya katibu wa chama wa wilaya.
  • Tabia hii inasababisha tunapata wabunge wabovu kabisa, wabunge wakiwa wabovu, hawana uwezo inasababisha kupata viongozi wabovu na pia mawaziri wabovu.
Mhshimiwa ukifanikiwa kupata uwenyekiti fanya taratibu kukomesha tabia hii ya rushwa inatia aibu sana kwenye chama.
 
Back
Top Bottom