Rais John Magufuli amewagomea baadhi ya wabunge waliopendekeza Tabora kugawanywa kwa kuanzisha mkoa mpya wa Nzega.
Wabunge hao ni Naibu Waziri wa Afya, Dk Hamisi Kigwangalla ambaye pia ni mbunge wa Nzega Vijijini, Hussein Bashe (Nzega Mjini) na Seif Gulamali wa Manonga.
Akizungumza na wakazi wa mji wa Nzega ambako wabunge hao walitoa ombi hilo, Magufuli alisema hana mpango wa kugawa mkoa wala wilaya kwa kuwa kufanya hivyo ni kuongeza gharama za uendeshaji wa shughuli za Serikali.
Badala yake alisema fedha ambazo zingetumika kuanzisha mikoa na wilaya mpya zitaelekezwa kutekeleza miradi ya maendeleo.
Ni kweli kuongeza mkoa/wilaya kunaongeza gharama lakini pia kunasaidia serikali kuwa karibu na wananchi. Kama population imeongezeka ina mana resources zinatakiwa ziongezeke na zisimamiwe vizuri. Raisi asingekataa mbele ya wananchi badala yake angetafakari kwanza ombi la wabunge. Mshauri wa Raisi ni either anamuogopa au kazi imemshinda haiwezekani mtu anatoa matamko tu bila kushauriwa.