Dr leader
JF-Expert Member
- Jun 28, 2016
- 1,080
- 1,448
Dhiki
1 Naomba kuwauliza, majibu yawe mezani
Hayano ndoyaniliza, sijui nimekosani
Yataka kunimaliza, mwenzenu nitaabani
Rafiki niliyenae, katu ataki niwata
2 Amenigomea hasa, hunitoka na kurudi
Ngozi yake kama kasa, aniumiza fuadi
Nataka kufanya masa, nione lake kusudi
Rafiki niliyenae, katu ataki niwata
3 Namsema asikie, tena kwa jina mujue
Huko mkasimulie, na nataka nimuue
Dhiki 'sinishikilie, angalau nipumue
Rafiki niliyenae, jina lake ndilo dhiki
[emoji2399]Abuuabdillah[emoji3578]
Omari Juma Kimweri
0744883353
1 Naomba kuwauliza, majibu yawe mezani
Hayano ndoyaniliza, sijui nimekosani
Yataka kunimaliza, mwenzenu nitaabani
Rafiki niliyenae, katu ataki niwata
2 Amenigomea hasa, hunitoka na kurudi
Ngozi yake kama kasa, aniumiza fuadi
Nataka kufanya masa, nione lake kusudi
Rafiki niliyenae, katu ataki niwata
3 Namsema asikie, tena kwa jina mujue
Huko mkasimulie, na nataka nimuue
Dhiki 'sinishikilie, angalau nipumue
Rafiki niliyenae, jina lake ndilo dhiki
[emoji2399]Abuuabdillah[emoji3578]
Omari Juma Kimweri
0744883353