Mkuu dagii nijuavyo kitufe cha kuwashia(power on/off), mara nyingi huwa kikubwa kuliko vingine japo pia kinaweza kuwa kidogo, huwa kinatengwa kidogo tofauti na vingine, hakiwekwagi katikati ila pembezoni mwa kifaa husika(redio). Kwa ujumla si kitufe rahisi kukikosa, jaribu tena au labda ina tatizo katika uwakaji wake au uunganishwaji. Ukishindwa kabisa jaribu kuweka picha watu wanaweza kukusaidia kabla mafundi hawajaenda kukutoa pesa ya kukuelekeza tu.
Wakuu hivi majuzi niliagiza gari kutoka Japan sasa kuliwasha na kutembelea si tatizo, tatizo ni hapo kwenye radio imeandikwa ki Japanes na tatizo ni kuiwasha sasa na mwezi sasa siisikilizi, kama kuna mjuzi tafadhali msaada wakuu.
Ingekuwa ni Tanzania tunatengeneza magari kwa ulimbukeni wetu tungeweka lugha za kiingereza.
Please ebu nijuze, hiyo tuition ya ki japani ipo wapi!Kama vipi jiunge na tuition ya lugha ubalozi wa Japan au toa hiyo ununue nyingine.