Sekretarieti ya Ajira Katika Utumishi wa Umma
July 22, 2014 ·
MASWALI NA MAJIBU YA HOJA MBALIMBALI ZA WADAU
Awali ya yote Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma, inapenda kuwashukuru wadau wote waliotuandikia maoni pamoja na kuuliza maswali mbalimbali kwa kipindi chote cha mwezi Mei hadi Julai, 2014. Maswali yao yanasaidia sana pindi yanapotolewa majibu ya jumla kwa faida ya wasomaji wetu wengine katika kuelimishana kuhusu masuala yanayohusu uendeshaji wa mchakato wa ajira Serikalini.
SWALI
1. Nimekuwa mfuatiliaji wa Vyombo mbalimbali vya Habari ikiwemo mitandao ya kijamii na kuna wakati niliona baadhi ya wadau wenu wakilalamikia suala la kutumia transcript katika kutuma maombi ya kazi. Je, Sekretarieti ya Ajira mnalizungumziaje suala hilo?
JIBU
Kuhusu suala la matumizi ya “Transcript” katika kuwasilisha maombi ya kazi inakubalika ila kutegemeana na muda wa mhusika aliomaliza masomo/elimu yake. Kwa mfano mhusika amemaliza chuo miaka miwili iliyopita na chuo alichomaliza elimu/mafunzo yake bado hakijatoa vyeti kwa wahitimu wake, basi mwombaji anaweza kutumia transcript kuwasilisha maombi yake ya kazi. Ila endapo mwombaji atatumia transcript kuwasilisha maombi na chuo husika alichomaliza kilishatoa vyeti vya kuhitimu atatakiwa kuambatanisha na nakala ya cheti cha kuhitimu na siku ya usaili anapaswa kuja na nakala halisi zote za taaluma aliyonayo na si kuendelea kutumia transcript peke yake. Aidha, ni muhimu waombaji wakafahamu kuwa endapo cheti cha kuhitimu hakijatoka chuoni na mhusika ameona tangazo na kutuma maombi kwa kuwasilisha transcripts zilizoandikwa provisional, au provisional results hazitakubaliwa.
MWENYE UELEWA NA HILI NAOMBA ANISAIDIE