MTINGIJOLI
JF-Expert Member
- Aug 19, 2014
- 1,358
- 1,324
Leo nimeamka na mood, ya kusikiliza mziki mzuri, basi katika kusikiliza kwangu nikajikuta namsikiliza huyu gwiji wa Bongo fleva Q Chillah {Q Chief] jamani jamaa anajua, hachoshi masikioni mwako.
Tangu anaanza mziki hadi alipo sasa hivi, namsikiliza hadi machozi yanataka kunitoka, kama hii nyimbo yake inaitwa maua, ni nzuri balaa ila kwenye vituo vya radio sijawahi kuisikia, sijui kama wanayo.
Cha kusikitissha Q Chillah hayupo kwenye ramani ya mziki kabisa, nyimbo za ajabu ajabu ndio zinapata air time na ndio zinatamba, kweli Mungu akunyime vyote lakini asikunyime bahati.
Unaweza upo vizuri lakini huonekani, hakuna hata mmoja anaekutazama, hiki ndio kinachomkuta huyu ndugu yetu leo hii, ila level zake ni nyingine kabisa.
Tangu anaanza mziki hadi alipo sasa hivi, namsikiliza hadi machozi yanataka kunitoka, kama hii nyimbo yake inaitwa maua, ni nzuri balaa ila kwenye vituo vya radio sijawahi kuisikia, sijui kama wanayo.
Cha kusikitissha Q Chillah hayupo kwenye ramani ya mziki kabisa, nyimbo za ajabu ajabu ndio zinapata air time na ndio zinatamba, kweli Mungu akunyime vyote lakini asikunyime bahati.
Unaweza upo vizuri lakini huonekani, hakuna hata mmoja anaekutazama, hiki ndio kinachomkuta huyu ndugu yetu leo hii, ila level zake ni nyingine kabisa.