PSPF tuwalipe wastaafu mafao yao, wanateseka sana

PSPF tuwalipe wastaafu mafao yao, wanateseka sana

mugajwale

Senior Member
Joined
Feb 19, 2015
Posts
105
Reaction score
23
Wapo wengi wamestaafu tangu mwezi wa 4 mpaka leo Disemba hawajalipwa mafao. Wazee wamekuwa ombaomba, mnawadhalilisha sana, walipeni.
 
wapo wengi wamestaafu tangu mwezi wa 4 mpk leo dec hawajalipwa mafao,wazee wamekua ombaomba,mnawadharirisha sana,walipen

Inauma Sana, Sasa Fedha Wamepeleka Wapi? Watapata Wanachama Wapya Kweli?
 
Wahusika chondechonde wafanyie mpango bila ya kuwachelewesha, msijishau nyie kwa kuwa matumbo yenu yamejaa.

Wafikirieni wenzenu, mkumbuke hiyo ni haki yao kwa kulitumikia Taifa hili
 
Aiseee sasa upi mfuko bora ikiwa hata huu unaojinasibu kuwa ndio mfuko bora kila uchwao unafanya hivi
 
Duh ctaki kuamini kama pspf ndo wanaovimbisha majipu namna hiyo...kwa nn wazurumu haki za watu!!!?
 
Hii mifuko yote ni shida Hata LAPF nao ni ugonjwa wa Moyo. Nadhani itungwe sheria Ya kuwatoza faini
 
Serikali haijaileta pesa za 15% contribution ya mwajiri kutoka hazina tangu mwezi May 2015 hadi sasa kwa mifuko yote ya pension. Kindly be informed. ..
 
Hakuna mfuko wa kipuuzi kama pspf, wazee wamestaa tangu mwezi wa kwanza lakini wanazungushwa tu, muogopeni Mungu
 
mm ni victim.Mkurugenzi njoo hapa unieleze ni vipi unadi viwanja na ujenzi wa nyumba za kuuza wakati tunanyimwa haki zetu.Waziri wa dhamana ya mfuko huo njoo anzia pspf tunakufa tafadhari.
 
ila hawa watu wanazingua sana... hela za kujenga magorofa nchi nzima wanazo ila kuwalipa wanachama wao hawana!!! magufuli bora angeanzia na huku
 
Huyu mkurugenzi mkuu alikuwa anakesha angani hata JK alikuwa cha mtoto.
 
Usikute walalamishi hapa ndio walioipa ccm kura tena kwa mbwebwe. Wapinzani wangechukua nchi yote haya yangefumuliwa. Maskini Pombe, kasha pigwa mkwara na kamati kuu ya ccm majuzi kati!!
 
Mifuko ya Hifadhi za Jamii ni Majipu yanahitaji kutumbuliwa haraka iwezekanavyo.
 
Nasikia serikali ilikopa fedha nyingi kutoka mifuko hii wakasahau kuwa fedha hiyo ni makato ya mishahara ya members wanaochangia ziwasaidie wakistaafu wengi wao ni wazee waliolitumikia taifa hili kwa muda mrefu kutokana na uzee nguvu zimewaishia tegemeo lao ni michango waliyokuwa wanakatwa kutoka mishahara yao sasa serikali imechukua fedha yao hii ni dhuruma kwa wazee wetu
 
Hivi hawa si ndio wanajinadi kwa jengo refu dsm?
Kwa hiyo badalabya kulipa wastaafu wakaamua wajenge??
 
Tatizo la PSPF bila shaka linaanzia pale mfuko ulipoanzishwa kisiasa na kiuuaji zaidi bila kuzingatia maslahi ya umma. Mfuko huu ulianzishwa na kupewa jukumu la kulipa pension na mafao bila mfuko kuwa na mfumo wa uchangiaji. Kwa maneno mengine watumishi wa serikali walihamishiwa kwenye mfuko huu bila kuwepo michango yao ya pension. Sasa malipo ya pension yamekuwa mzigo mzito sana. Na kiukweli PSPF hawana fedha za kutosha. Wanachosubiri sasa ni serikali iwape conditional bond itakayowawezesha kulipwa coupon semi annually ili warescue that bad situation. Haya ni baadhi ya maamuzi ya serikali ya Mzee Mkapa ambayo consequences zake ndiyo zinaonekana sasa. Let's hope for the best ila PSPF mmmmmm hali siyo yenyewe
 
Serikali haijaileta pesa za 15% contribution ya mwajiri kutoka hazina tangu mwezi May 2015 hadi sasa kwa mifuko yote ya pension. Kindly be informed. ..

bila shaka hiyo haiwezi kuwa sababu
 
Hii kero hii mifuko ya jamii walipeni wazee wetu ambao wametumikia nchi kwa uaminifu
 
Back
Top Bottom