deonova
JF-Expert Member
- Apr 22, 2013
- 742
- 419
Habari wadau,
Naomba kuleta hii hoja kwenu tuijadili/munifumbue macho kidogo. Hii inahusu moja ya project kubwa za kimuziki zilizowahi kufanyika inaitwa 'OKOA HIP HOP'
Hii ni project kubwa iliyowahi kufanyika ikiwahusisha wasanii wote wa Hip Hop na kama nakumbuka vizuri walizunguka mikoa kadhaa ikiwemo Dar es Salaam na Arusha na wasanii nnaokumbuka haraka haraka waliozunguka ktk project hii ni Kala Pina na Kikosi cha mizinga, Nako 2 Nako soldiers, River Camp Soldiers, Chid benz, Ditto, Fid Q, Mapacha, Langa (R.I.P), Geez Mabovu (R.I.P) na wengineo wengi.
Sasa mimi hoja yangu iko hapa kuwa; kulingana na slogan ya project ilivyokuwa inasema Okoa Hip Hop maana yake ilikuwa ni harakati mahususi kwa ajili ya kuokoa muziki wa hip hop kutoka ktk hatari ya kupotea/kupotezwa. Inasemekana project hii ilikuja mahususi baada ya kuwepo kwa njama za makusudi za kuupoteza muziki huu wa hip hop.
Je ni nani/akina nani walikuwa nyuma ya hujuma hizi za kuuhujumu (sarbotage) huu muziki hadi wasanii hawa kuamua kuanzisha hatua za makusudi kuuokoa? Na hujuma zilikuwa za namna gani? Michango yenu itanipa uelewa mkubwa sana ktk hili.
Asanteni nawasilisha.
Naomba kuleta hii hoja kwenu tuijadili/munifumbue macho kidogo. Hii inahusu moja ya project kubwa za kimuziki zilizowahi kufanyika inaitwa 'OKOA HIP HOP'
Hii ni project kubwa iliyowahi kufanyika ikiwahusisha wasanii wote wa Hip Hop na kama nakumbuka vizuri walizunguka mikoa kadhaa ikiwemo Dar es Salaam na Arusha na wasanii nnaokumbuka haraka haraka waliozunguka ktk project hii ni Kala Pina na Kikosi cha mizinga, Nako 2 Nako soldiers, River Camp Soldiers, Chid benz, Ditto, Fid Q, Mapacha, Langa (R.I.P), Geez Mabovu (R.I.P) na wengineo wengi.
Sasa mimi hoja yangu iko hapa kuwa; kulingana na slogan ya project ilivyokuwa inasema Okoa Hip Hop maana yake ilikuwa ni harakati mahususi kwa ajili ya kuokoa muziki wa hip hop kutoka ktk hatari ya kupotea/kupotezwa. Inasemekana project hii ilikuja mahususi baada ya kuwepo kwa njama za makusudi za kuupoteza muziki huu wa hip hop.
Je ni nani/akina nani walikuwa nyuma ya hujuma hizi za kuuhujumu (sarbotage) huu muziki hadi wasanii hawa kuamua kuanzisha hatua za makusudi kuuokoa? Na hujuma zilikuwa za namna gani? Michango yenu itanipa uelewa mkubwa sana ktk hili.
Asanteni nawasilisha.